< Éxodo 39 >
1 De azul, púrpura y escarlata, hicieron las prendas de vestir finamente trabajadas para ministrar en el lugar santo, e hicieron las vestiduras sagradas para Aarón, como Yahvé le ordenó a Moisés.
Kutokana na nyuzi za rangi ya buluu, ya zambarau na nyekundu akatengeneza mavazi yaliyofumwa kwa ajili ya kuhudumu katika mahali patakatifu. Pia akamshonea Aroni mavazi matakatifu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
2 Hizo el efod de oro, azul, púrpura, escarlata y lino fino.
Akatengeneza kisibau cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kitani iliyosokotwa vizuri.
3 El oro lo batieron en láminas finas y lo cortaron en hilos, para trabajarlo con el azul, la púrpura, la escarlata y el lino fino, obra del artesano hábil.
Akafua vipande vyembamba vya dhahabu kwa nyundo na kutengeneza nyuzi nyembamba ili kuzifuma pamoja na hizo nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu na kitani safi, kazi ya fundi stadi.
4 Le hicieron correas para los hombros, unidas entre sí. Se unió por los dos extremos.
Akatengeneza vipande vya mabegani vya kisibau, vilivyoshikizwa kwenye pembe zake mbili ili kukifungia kisibau.
5 La banda tejida con destreza que lo cubría, con la cual se sujetaba, era de la misma pieza, como su obra: de oro, de azul, de púrpura, de escarlata y de lino fino torcido, como Yahvé le ordenó a Moisés.
Mshipi wa kiunoni uliofumwa kwa ustadi ulifanana nacho: ulikuwa kitu kimoja na hicho kisibau, nao ulitengenezwa kwa dhahabu na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na kwa kitani iliyosokotwa vizuri, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
6 Trabajaron las piedras de ónice, encerradas en engastes de oro, grabadas con los grabados de un sello, según los nombres de los hijos de Israel.
Akatengeneza vito vya shohamu vilivyowekwa katika vijalizo vya dhahabu, navyo vilichorwa na majina ya wana wa Israeli kama vile muhuri huchorwa.
7 Las puso en los tirantes del efod, para que fueran piedras conmemorativas de los hijos de Israel, tal como el Señor se lo había ordenado a Moisés.
Kisha akavifungia kwenye vipande vya mabega ya kisibau kuwa vito vya ukumbusho kwa wana wa Israeli, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
8 Hizo el pectoral, obra de un hábil artesano, como la obra del efod: de oro, de azul, de púrpura, de escarlata y de lino torcido.
Akafanyiza kifuko cha kifuani, kazi ya fundi stadi. Akakitengeneza kama kile kisibau: cha dhahabu, na nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na za rangi nyekundu, cha kitani safi iliyosokotwa.
9 Era cuadrado. Hicieron el pectoral doble. Su longitud era de un palmo, y su anchura de un palmo, siendo doble.
Kifuko hicho kilikuwa cha mraba, chenye urefu wa shibiri moja na upana wa shibiri moja, nacho kilikunjwa mara mbili.
10 Colocaron en él cuatro hileras de piedras. Una hilera de rubí, topacio y berilo era la primera hilera;
Kifuko hicho kilipambwa kwa safu nne za vito vya thamani. Safu ya kwanza ilikuwa na akiki, yakuti manjano na zabarajadi;
11 y la segunda hilera, una turquesa, un zafiro, y una esmeralda;
safu ya pili ilikuwa na almasi, yakuti samawi na zumaridi;
12 y la tercera hilera, un jacinto, una ágata y una amatista;
safu ya tatu ilikuwa na hiakintho, akiki nyekundu na amethisto;
13 y la cuarta hilera, un crisolito, un ónice y un jaspe. Estaban encerradas en engastes de oro.
katika safu ya nne ilikuwa na krisolitho, shohamu na yaspi. Vito hivyo vilitiwa kwenye vijalizo vya dhahabu.
14 Las piedras eran según los nombres de los hijos de Israel, doce, según sus nombres; como los grabados de un sello, cada uno según su nombre, para las doce tribus.
Palikuwa na vito kumi na viwili, kila kimoja kikiwa na jina mojawapo la wana wa Israeli; kila kimoja kilichorwa kama muhuri kikiwa na jina mojawapo la yale makabila kumi na mawili.
15 Hicieron en el pectoral cadenas como cordones, de oro puro trenzado.
Kwa ajili ya kile kifuko cha kifuani akakitengenezea mikufu ya dhahabu safi, iliyosokotwa kama kamba.
16 Hicieron dos engastes de oro y dos anillos de oro, y pusieron los dos anillos en los dos extremos del pectoral.
Akatengeneza vijalizo viwili vya dhahabu na pete mbili za dhahabu, na kuzifungia pete hizo kwenye pembe mbili za hicho kifuko cha kifuani.
17 Pusieron las dos cadenas trenzadas de oro en los dos anillos de los extremos del pectoral.
Akafunga hiyo mikufu miwili ya dhahabu kwenye hizo pete katika pembe za hicho kifuko cha kifuani,
18 Los otros dos extremos de las dos cadenas trenzadas los pusieron en los dos engastes, y los pusieron en los tirantes del efod, en su parte delantera.
nazo zile ncha nyingine za mkufu akazifunga kwenye vile vijalizo viwili, na kuzishikamanisha na vile vipande vya mabega vya kile kisibau upande wa mbele.
19 Hicieron dos anillos de oro y los pusieron en los dos extremos del pectoral, en su borde, que estaba hacia el lado del efod, hacia adentro.
Akatengeneza pete mbili za dhahabu na kuzishikamanisha kwenye pembe mbili za chini, upande wa ndani wa kifuko cha kifuani karibu na kisibau.
20 Hicieron otros dos anillos de oro y los pusieron en los dos tirantes del efod por debajo, en su parte delantera, cerca de su acoplamiento, por encima de la banda hábilmente tejida del efod.
Kisha akatengeneza pete nyingine mbili za dhahabu na kuzishikamanisha sehemu ya chini ya vipande vya mabega upande wa mbele wa kile kisibau, karibu na pindo juu kidogo ya mshipi wa kiunoni wa kisibau.
21 Luego unieron el pectoral por sus anillos a los anillos del efod con un cordón de color azul, para que quedara sobre la banda hábilmente tejida del efod, y para que el pectoral no se desprendiera del efod, tal como el Señor lo había ordenado a Moisés.
Akafunga pete za hicho kifuko cha kifuani kwenye pete za kisibau kwa kamba ya buluu, wakiziunganisha na ule mshipi wa kiunoni, ili kifuko cha kifuani kisisogee kutoka kwenye kile kisibau, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
22 Hizo el manto del efod de tela, todo de color azul.
Akashona joho la kisibau lote kwa kitambaa cha rangi ya buluu tupu, kazi ya mfumaji,
23 La abertura del manto en el centro era como la abertura de una cota de malla, con una cinta alrededor de la abertura, para que no se rompiera.
na lilikuwa na nafasi ya shingo katikati ya joho lile iliyofanana na ukosi, na utepe ulioshonwa kuizunguka nafasi hiyo ili isichanike.
24 Hicieron en las faldas del manto granadas de color azul, púrpura, escarlata y lino torcido.
Akatengeneza makomamanga ya nyuzi za rangi ya buluu, za zambarau, na nyekundu na ya kitani iliyosokotwa vizuri kuzunguka pindo la hilo joho.
25 Hicieron campanas de oro puro, y pusieron las campanas entre las granadas alrededor de los faldones del manto, entre las granadas;
Kisha akatengeneza vikengele vya dhahabu safi na kuvishikamanisha kuzunguka pindo hilo kati ya hayo makomamanga.
26 una campana y una granada, una campana y una granada, alrededor de los faldones del manto, para ministrar, como Yahvé le ordenó a Moisés.
Hivyo vikengele na makomamanga vilipishana kuzunguka upindo wa joho ili livaliwe kwa kuhudumu, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
27 Hicieron las túnicas de lino fino de obra tejida para Aarón y para sus hijos,
Pia akamtengenezea Aroni na wanawe makoti ya kitani safi, kazi ya mfumaji,
28 el turbante de lino fino, las cintillos de lino fino, los pantalones de lino fino,
na kilemba cha kitani safi, tepe za kichwani za kitani, na nguo za ndani za kitani iliyosokotwa vizuri.
29 el fajín de lino fino, azul, púrpura y escarlata, obra del bordador, como Yahvé mandó a Moisés.
Mshipi ulikuwa wa kitani iliyosokotwa vizuri ya rangi ya buluu, na zambarau, na nyekundu, kazi ya mtarizi, kama Bwana alivyomwagiza Mose.
30 Hicieron la placa de la corona sagrada de oro puro, y escribieron en ella una inscripción, como los grabados de un sello: “SANTIDAD A YAHWEH”.
Kisha akatengeneza lile bamba, taji takatifu, kwa dhahabu safi na kuchora juu yake maneno haya kama vile muhuri huchorwa: Mtakatifu kwa Bwana.
31 Le ataron un cordón de color azul, para sujetarlo al turbante de arriba, como Yahvé le ordenó a Moisés.
Kisha wakalifunga kwa kamba ya rangi ya buluu ili kulishikamanisha na kile kilemba kama Bwana alivyomwagiza Mose.
32 Así quedó terminada toda la obra del tabernáculo de la Tienda de Reunión. Los hijos de Israel hicieron conforme a todo lo que Yahvé ordenó a Moisés; así lo hicieron.
Kwa hiyo kazi yote ya maskani, Hema la Kukutania ikakamilika. Waisraeli wakafanya kila kitu sawasawa kama vile Bwana alivyomwagiza Mose.
33 Llevaron el tabernáculo a Moisés la tienda, con todos sus muebles, sus broches, sus tablas, sus barras, sus pilares, sus bases,
Ndipo wakaleta maskani kwa Mose: hema pamoja na vifaa vyake vyote, vibanio vyake, mihimili yake, mataruma yake, nguzo na vitako vyake;
34 la cubierta de pieles de carnero teñidas de rojo, la cubierta de pieles de vaca marina, el velo de la pantalla,
kifuniko cha ngozi za kondoo dume kilichotiwa rangi nyekundu, kifuniko cha ngozi za pomboo, pazia la kufunikia;
35 el arca del testimonio con sus postes, el propiciatorio,
Sanduku la Ushuhuda pamoja na mipiko yake na kiti cha rehema,
36 la mesa, todos sus utensilios, el pan de la proposición,
meza pamoja na vyombo vyake vyote na mikate ya Wonyesho;
37 el candelabro puro, sus lámparas, todos sus utensilios, el aceite para la luz,
kinara cha taa cha dhahabu safi, safu zake za taa pamoja na vifaa vyake vyote pamoja na mafuta kwa ajili ya taa;
38 el altar de oro, el aceite de la unción, el incienso aromático, la cortina para la puerta de la Tienda,
madhabahu ya dhahabu, mafuta ya upako, uvumba wenye harufu nzuri na pazia la ingilio la hema;
39 el altar de bronce, su reja de bronce, sus varas, todos sus vasos, la pila y su base,
madhabahu ya shaba, pamoja na wavu wa shaba, nguzo zake na vyombo vyake vyote, sinia, na tako lake;
40 las cortinas del atrio, sus columnas, sus bases, la cortina para la puerta del atrio, sus cuerdas, sus clavijas, y todos los instrumentos del servicio del tabernáculo, para la Tienda de Reunión,
mapazia ya ua pamoja na nguzo na vitako vyake, pia na pazia kwa ajili ya ingilio la kwenye ua; kamba zake na vigingi vya hema kwa ajili ya ua; vyombo vyote vilivyohitajiwa kwa ajili ya maskani, Hema la Kukutania;
41 las vestimentas finamente trabajadas para ministrar en el lugar santo, las vestimentas sagradas para el sacerdote Aarón y las vestimentas de sus hijos, para ministrar en el oficio del sacerdote.
na mavazi yaliyofumwa yanayovaliwa wakati wa huduma katika mahali patakatifu, yaani mavazi matakatifu ya kuhani Aroni na mavazi kwa ajili ya wanawe watakapokuwa wakihudumu katika kazi ya ukuhani.
42 Conforme a todo lo que Yahvé mandó a Moisés, así hicieron los hijos de Israel todo el trabajo.
Waisraeli walikuwa wamefanya kazi yote sawasawa na vile Bwana alivyokuwa amemwagiza Mose.
43 Moisés vio toda la obra, y he aquí que la habían hecho como Yahvé había ordenado. Así lo habían hecho; y Moisés los bendijo.
Mose akakagua kazi na kuona kuwa walikuwa wameifanya sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa ameagiza. Kwa hiyo Mose akawabariki.