< Amós 3 >
1 Escuchen esta palabra que Yahvé ha pronunciado contra ustedes, hijos de Israel, contra toda la familia que hice subir de la tierra de Egipto, diciendo
Sikilizeni neno hili alilosema Bwana dhidi yenu, enyi watu wa Israeli, dhidi ya jamaa nzima niliowapandisha toka Misri:
2 “Sólo a ti te he elegido de entre todas las familias de la tierra. Por eso te castigaré por todos tus pecados”.
“Ni ninyi tu niliowachagua kati ya jamaa zote za dunia; kwa hiyo nitawaadhibu kwa ajili ya dhambi zenu zote.”
3 Caminan dos juntos, ¿a menos que se hayan puesto de acuerdo?
Je, watu wawili hutembea pamoja wasipokubaliana kufanya hivyo?
4 Rugirá un león en la espesura, cuando no tiene presa? ¿Grita un león joven fuera de su guarida, si no ha cogido nada?
Je, simba hunguruma katika kichaka wakati hana mawindo? Aweza kuvuma katika pango wakati ambao hajakamata chochote?
5 ¿Puede un pájaro caer en una trampa en la tierra, donde no se le tiende una trampa? ¿Surge una trampa del suelo, cuando no hay nada que atrapar?
Je, ndege aweza kuanguka kwenye mtego ulio ardhini ambapo hajategewa chambo? Je, mtego unaweza kufyatuka toka ardhini wakati ambapo hakuna chochote cha kunasa?
6 Suena la alarma de la trompeta en una ciudad, sin que la gente tenga miedo? El mal le sucede a una ciudad, ¿y Yahvé no lo ha hecho?
Je, tarumbeta inapopigwa mjini kujulisha hatari, watu hawatetemeki? Mji upatwapo na maafa, je, si Bwana amesababisha?
7 Ciertamente el Señor Yahvé no hará nada, a menos que revele su secreto a sus siervos los profetas.
Hakika Bwana Mwenyezi hatafanya neno lolote bila kuwafunulia watumishi wake manabii siri yake.
8 El león ha rugido. ¿Quién no temerá? El Señor Yahvé ha hablado. ¿Quién puede sino profetizar?
Simba amenguruma: je, ni nani ambaye hataogopa? Bwana Mwenyezi ametamka: je, ni nani awezaye kukosa kutoa unabii?
9 Proclamad en los palacios de Asdod, y en los palacios de la tierra de Egipto, y digan: “Reúnanse en los montes de Samaria, y ver qué malestar hay en ella, y qué opresión hay entre ellos”.
Tangazeni katika ngome za Ashdodi na katika ngome za Misri: “Kusanyikeni juu ya milima ya Samaria; angalieni wingi wa wasiwasi ulio ndani yake, na uonevu ulio miongoni mwa watu wake.”
10 “Ciertamente, no saben hacer el bien”, dice Yahvé, “Que acaparan el saqueo y el botín en sus palacios”.
Bwana asema: “Hawajui kutenda lililo jema, wale ambao hujilundikia nyara na vitu vilivyotekwa katika ngome zao.”
11 Por eso dice el Señor Yahvé: “Un adversario invadirá la tierra; y derribará tus fortalezas, y sus fortalezas serán saqueadas”.
Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana Mwenyezi: “Adui ataizingira nchi; ataangusha chini ngome zenu na kuteka nyara maboma yenu.”
12 Yahvé dice: “Como el pastor rescata de la boca del león dos patas, o un trozo de oreja, así serán rescatados los hijos de Israel que se sientan en Samaria en la esquina de un sofá, y en los cojines de seda de una cama”.
Hili ndilo asemalo Bwana: “Kama vile mchungaji aokoavyo kinywani mwa simba vipande viwili tu vya mfupa wa mguu au kipande cha sikio, hivyo ndivyo Waisraeli watakavyookolewa, wale wakaao Samaria kwenye kingo za vitanda vyao, na katika Dameski kwenye viti vyao vya fahari.”
13 “Escuchen y den testimonio contra la casa de Jacob”, dice el Señor Yahvé, el Dios de los Ejércitos.
“Sikia hili na ushuhudie dhidi ya nyumba ya Yakobo,” asema Bwana, Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote.
14 “Porque el día en que yo visite las transgresiones de Israel sobre él, También visitaré los altares de Betel; y los cuernos del altar serán cortados, y caen al suelo.
“Siku nitakapomwadhibu Israeli kwa sababu ya dhambi zake, nitaharibu madhabahu za Betheli; pembe za madhabahu zitakatiliwa mbali na kuanguka chini.
15 Golpearé la casa de invierno con la de verano; y las casas de marfil perecerán, y las grandes casas tendrán un final”. dice Yahvé.
Nitabomoa nyumba ya wakati wa masika, pamoja na nyumba ya wakati wa kiangazi; nyumba zilizonakshiwa kwa pembe za ndovu na majumba makubwa ya fahari yatabomolewa,” asema Bwana.