< 2 Corintios 6 >

1 Trabajando juntos, os rogamos también que no recibáis la gracia de Dios en vano.
Basi, tukiwa wafanyakazi pamoja na Mungu, tunawasihi msikubali ile neema mliyopokea kutoka kwa Mungu ipotee bure.
2 Porque él dice, “En un momento aceptable te escuché. En un día de salvación te ayudé”. He aquí, ahora es el tiempo aceptable. He aquí, ahora es el día de la salvación.
Mungu asema hivi: “Wakati wa kufaa nimekusikiliza, wakati wa wokovu nikakusaidia.” Basi, sasa ndio wakati wa kufaa, sasa ndiyo siku ya wokovu!
3 No damos ocasión de tropiezo en nada, para que no se reproche nuestro servicio,
Kusudi tusiwe na lawama yoyote katika utumishi wetu, hatupendi kumwekea mtu yeyote kizuio chochote.
4 sino que en todo nos encomendamos como siervos de Dios en gran resistencia, en aflicciones, en dificultades, en angustias,
Badala yake, tunajionyesha kuwa kweli watumishi wa Mungu kwa kila kitu: kwa uvumilivu mwingi wakati wa mateso, shida na taabu.
5 en golpes, en cárceles, en disturbios, en trabajos, en vigilias, en ayunos,
Tumepigwa, tumetiwa gerezani na kuzomewa hadharani; tumefanya kazi tukachoka; tumekesha na kukaa bila kula.
6 en pureza, en conocimiento, en perseverancia, en bondad, en el Espíritu Santo, en amor sincero,
Tunajionyesha kuwa watumishi wa Mungu kwa usafi wa moyo, elimu, uvumilivu na wema; kwa Roho Mtakatifu, kwa upendo usio na unafiki,
7 en la palabra de verdad, en el poder de Dios, con la armadura de la justicia a la derecha y a la izquierda,
kwa ujumbe wa kweli na kwa nguvu ya Mungu. Uadilifu ndiyo silaha yetu upande wa kulia na upande wa kushoto.
8 en la gloria y en la deshonra, en la mala y en la buena fama, en el engaño y en la verdad,
Tuko tayari kupata heshima na kudharauliwa, kulaumiwa na kusifiwa. Twadhaniwa kuwa waongo, kumbe twasema kweli;
9 en el desconocimiento y en la fama, en la muerte y en la vida, en el castigo y en la muerte,
kama wasiojulikana, kumbe twajulikana kwa wote, kama waliokufa, lakini mwonavyo, sisi ni wazima kabisa.
10 en la tristeza y en la alegría, en la pobreza y en la riqueza, en la carencia y en la posesión de todas las cosas.
Ingawa tumeadhibiwa, hatukuuawa; ingawa tunayo huzuni, twafurahi daima; ingawa tu maskini hohehahe, lakini twatajirisha watu wengi; twaonekana kuwa watu tusio na chochote, kumbe tuna kila kitu.
11 Nuestra boca se ha abierta para vosotros, Corintios. Nuestro corazón se ensancha.
Ndugu Wakorintho, tumezungumza nanyi kwa unyofu; mioyo yetu iko wazi kabisa.
12 Ustedes no están restringidos por nosotros, sino que están restringidos por sus propios afectos.
Kama mnaona kuna kizuizi chochote kile, kizuizi hicho kiko kwenu ninyi wenyewe, na si kwa upande wetu.
13 Ahora, a cambio — hablo como a mis hijos —, abrid también vosotros vuestros corazones.
Sasa nasema nanyi kama watoto wangu, wekeni mioyo yenu wazi kama nasi tulivyofanya.
14 No os unáis en yugo desigual con los incrédulos, porque, ¿qué comunión tienen la justicia y la iniquidad? ¿O qué comunión tiene la luz con las tinieblas?
Msiambatane na watu wasioamini. Je, wema na uovu vyapatana kweli? Mwanga na giza vyawezaje kukaa pamoja?
15 ¿Qué acuerdo tiene Cristo con Belial? ¿O qué parte tiene un creyente con un incrédulo?
Kristo anawezaje kupatana na Shetani? Muumini ana uhusiano gani na asiyeamini?
16 ¿Qué acuerdo tiene el templo de Dios con los ídolos? Porque tú eres un templo del Dios vivo. Así como Dios dijo: “Habitaré en ellos y caminaré en ellos. Yo seré su Dios y ellos serán mi pueblo”.
Hekalu la Mungu lina uhusiano gani na sanamu za uongo? Maana sisi ni hekalu la Mungu aliye hai. Kama Mungu mwenyewe alivyosema: “Nitafanya makao yangu kwao, na kuishi kati yao; Nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.”
17 Por eso “‘Sal de entre ellos’, y sepárense”, dice el Señor. ‘No toques ninguna cosa impura’. Te recibiré.
Kwa hiyo Bwana asema pia: “Ondokeni kati yao, mkajitenge nao, msiguse kitu najisi, nami nitawapokea.
18 Yo seré para vosotros un Padre. Seréis para mí hijos e hijas’. dice el Señor Todopoderoso”.
Mimi nitakuwa Baba yenu, nanyi mtakuwa watoto wangu, waume kwa wake, asema Bwana Mwenye Uwezo.”

< 2 Corintios 6 >