< Salmos 88 >

1 Una canción. Un salmo de los descendientes de Coré. Para el director del coro. Al son de “Mahalath Leannoth”. Un masquil por Hemán el ezraíta Señor, Dios de mi salvación, clamo a ti de día y de noche.
Wimbo. Zaburi ya wana wa Kora. Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi leanothi. Utenzi wa Hemani Mwezrahi. Ee Bwana, Mungu uniokoaye, nimelia mbele zako usiku na mchana.
2 Por favor escucha mi oración; escucha mis palabras de súplica.
Maombi yangu yafike mbele zako, utegee kilio changu sikio lako.
3 Mi vida está llena de problemas, y mi muerte se acerca. (Sheol h7585)
Kwa maana nafsi yangu imejaa taabu, na maisha yangu yanakaribia kaburi. (Sheol h7585)
4 Soy contado entre los moribundos; un hombre sin fuerzas.
Nimehesabiwa miongoni mwa wale waendao shimoni, niko kama mtu asiye na nguvu.
5 Soy abandonado entre los muertos, tendido como un cadáver en la tumba, olvidado y dejado a tu cuidado.
Nimetengwa pamoja na wafu, kama waliochinjwa walalao kaburini, ambao huwakumbuki tena, ambao wamekatiliwa mbali na uangalizi wako.
6 Me has puesto en un pozo profundo, entre las penumbras.
Umenitupa katika shimo lenye kina kirefu sana, katika vina vya giza nene.
7 Tu hostilidad me maltrata; me estás ahogando entre tus olas abrumadoras. (Selah)
Ghadhabu yako imekuwa nzito juu yangu, umenigharikisha kwa mawimbi yako yote.
8 Has hecho que mis enemigos me eviten, haciéndome repulsivo a sus vistas. Estoy atrapado, no puedo huir.
Umenitenga na rafiki zangu wa karibu na kunifanya chukizo kwao. Nimezuiliwa, wala siwezi kutoroka;
9 Señor, he llorado suplicándote cada día por ayuda, extendiendo mis manos hacia ti.
nuru ya macho yangu imefifia kwa ajili ya huzuni. Ee Bwana, ninakuita kila siku, ninakunyooshea wewe mikono yangu.
10 ¿Haces milagros entre los muertos? ¿Se levantan los muertos para alabarte? (Selah)
Je, wewe huwaonyesha wafu maajabu yako? Je, wale waliokufa huinuka na kukusifu?
11 Tu gran amor, ¿Se menciona en la tumba? Tu fidelidad, ¿Es discutida en lugar de destrucción?
Je, upendo wako hutangazwa kaburini, uaminifu wako katika Uharibifu?
12 ¿Las cosas maravillosas que haces son conocidas en las tinieblas? ¿Tu bondad es conocida en la tierra del olvido?
Je, maajabu yako hujulikana mahali pa giza, au matendo yako ya haki katika nchi ya usahaulifu?
13 Pero clamo a ti pidiendo ayuda; cada mañana oro a ti.
Lakini ninakulilia wewe, Ee Bwana, unisaidie; asubuhi maombi yangu huja mbele zako.
14 Señor, ¿Por qué me rechazas? ¿Por qué te alejas de mí?
Ee Bwana, kwa nini unanikataa na kunificha uso wako?
15 He estado enfermo desde que era joven, a menudo estuve a las puertas de la muerte. He tenido que soportar las cosas terribles que me has hecho. ¡Estoy desesperado!
Tangu ujana wangu nimeteseka, nikakaribia kifo; nimepatwa na hofu zako, nami nimekata tamaa.
16 Tu ira me ha vencido; las cosas terribles que haces me han destruido.
Ghadhabu yako imepita juu yangu; hofu zako zimeniangamiza.
17 Ellos me rodean constantemente como aguas de una inundación, succionándome.
Mchana kutwa zinanizunguka kama mafuriko; zimenimeza kabisa.
18 Has hecho que mi familia y mis amigos se alejen. La oscuridad es mi única amiga.
Umeniondolea marafiki na wapendwa wangu; giza limekuwa ndilo rafiki yangu wa karibu kuliko wote.

< Salmos 88 >