< Salmos 76 >

1 Para el director del coro: Un Salmo de Asaf. Un canto. Acompañamiento con instrumentos de cuerda. Dios tiene honra en Judá. Su nombre es grande en todo Israel.
Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Asafu. Wimbo. Katika Yuda, Mungu anajulikana, jina lake ni kuu katika Israeli.
2 Él vive en Jerusalén y habita en Sión.
Hema lake liko Salemu, makao yake katika Sayuni.
3 Allí quebró las fechas encendidas, los escudos, la espada y las armas de guerra. (Selah)
Huko alivunja mishale imetametayo, ngao na panga, silaha za vita.
4 Tu luz es gloriosa y eres más majestuoso que las montañas eternas.
Wewe unangʼaa kwa mwanga, mwenye fahari zaidi ya milima yenye utajiri wa wanyama pori.
5 Nuestros enemigos más valientes han sido saqueados. Ya duermen el sueño de la muerte. Incluso los más fuertes entre ellos no pudieron levantar una mano contra nosotros.
Mashujaa hulala wametekwa nyara, hulala usingizi wao wa mwisho; hakuna hata mmoja wa watu wa vita anayeweza kuinua mikono yake.
6 A tu voz, Dios de Jacob, tanto el caballo como el jinete caen muertos.
Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, farasi na gari la vita vilikaa kimya.
7 Todos te temen. ¿Quién podría mantenerse en pie ante tu ira?
Wewe peke yako ndiye wa kuogopwa. Ni nani awezaye kusimama mbele yako unapokasirika?
8 Anunciaste juicio desde el cielo. Todos en la tierra se espantaron y quedaron inmóviles
Kutoka mbinguni ulitamka hukumu, nayo nchi ikaogopa, ikawa kimya:
9 cuando te levantaste para pronunciar juicio y salvar a los oprimidos de la tierra. (Selah)
wakati wewe, Ee Mungu, ulipoinuka kuhukumu, kuwaokoa wote walioonewa katika nchi.
10 Incluso la ira humana contra ti te hace brillar, porque la usas como corona.
Hakika ghadhabu yako dhidi ya wanadamu inakuletea sifa, na masalia ya ghadhabu yako unajifunga mshipi.
11 Haz promesas a Dios y asegúrate de cumplirlas. Todos rinden tributo al Temible.
Wekeni nadhiri kwa Bwana Mungu wenu na kuzitimiza; nchi zote za jirani na walete zawadi kwa Yule astahiliye kuogopwa.
12 Porque él humilla a los líderes orgullosos. Y aterroriza a los reyes de la tierra.
Huvunja roho za watawala; anaogopwa na wafalme wa dunia.

< Salmos 76 >