< Salmos 73 >

1 Un Salmo de Asaf. Dios es ciertamente bueno con Israel. Con los que tienen pureza en sus mentes.
Zaburi ya Asafu. Hakika Mungu ni mwema kwa Israeli, kwa wale ambao mioyo yao ni safi.
2 Pero yo caí, y mis pies comenzaron a resbalar,
Bali kwangu mimi, miguu yangu ilikuwa karibu kuteleza; nilikuwa karibu mguu wangu kuachia uliposimama.
3 porque tuve celos de pretenciosos, y vi que le iba muy bien a los malvados.
Kwa maana niliwaonea wivu wenye kujivuna nilipoona kufanikiwa kwa waovu.
4 Parecen nunca enfermarse; lucen fuertes y saludables.
Wao hawana taabu, miili yao ina afya na nguvu.
5 Ellos no tienen problemas como los demás, y no son afectados por los desastres como el resto del mundo.
Hawapati shida zinazowataabisha watu wengine, wala hawapati mapigo kama wanadamu wengine.
6 Su collar es su orgullo, y se visten con violencia.
Kwa hiyo kiburi ni mkufu wao, wamejivika jeuri.
7 Sus ojos sobresalen por su gordura, y sus mentes están llenas de vanidad y egoísmo.
Uovu hutoka katika mioyo yao iliyokufa ganzi, majivuno maovu kutoka mioyoni mwao hauna kikomo.
8 Ellos se burlan de las personas y hablan con maldad. Con arrogancia y crueldad lanzan amenazas.
Hudhihaki na kusema kwa ukorofi, katika majivuno yao wanatishia kutesa.
9 En su hablar irrespetan al cielo, y difaman a los habitantes de la tierra.
Vinywa vyao huweka madai hata kwa mbingu, nazo ndimi zao humiliki duniani.
10 Por ello la gente los busca y creen todo lo que ellos dicen.
Kwa hiyo watu wao huwageukia na kunywa maji tele.
11 “Dios no se dará cuenta”, dicen. “¡El Altísimo no sabe nada de lo que está pasando!”
Wanasema, “Mungu awezaje kujua? Je, Yeye Aliye Juu Sana anayo maarifa?”
12 ¡Miren a los malvados! ¡No tienen nada de qué preocuparse en el mundo y siempre están ganando dinero!
Hivi ndivyo walivyo waovu: siku zote hawajali, wanaongezeka katika utajiri.
13 Ha sido inútil mantener mi mente pura y mis manos limpias.
Hakika nimeuweka moyo wangu safi bure, ni bure nimenawa mikono yangu nisiwe na hatia.
14 Soy maldito con sufrimientos todo el día; cada mañana sufro castigo.
Mchana kutwa nimetaabika, nimeadhibiwa kila asubuhi.
15 Si le hubiese hablado así a otros habría traicionado a tu pueblo, Señor.
Kama ningesema, “Nitasema hivi,” ningelikuwa nimewasaliti watoto wako.
16 Así que reflexioné y traté de entenderlo, pero parecía muy difícil para mi,
Nilipojaribu kuelewa haya yote, yalikuwa magumu kwangu kuelewa.
17 hasta que fui al Templo de Dios. Entonces entendí el fin de los malvados.
Mpaka nilipoingia patakatifu pa Mungu, ndipo nilipotambua mwisho wao.
18 Porque tu los mandas por un camino resbaladizo. Los envías a la destrucción.
Hakika unawaweka mahali pa utelezi, unawaangusha chini kwa uharibifu.
19 ¡Cuán rápido son destruidos! Su fin es espantoso.
Tazama jinsi wanavyoangamizwa ghafula, wanatoweshwa kabisa na vitisho!
20 Como al despertar después de un sueño, Señor, te olvidarás de ellos.
Kama ndoto mtu aamkapo, hivyo wakati uinukapo, Ee Bwana, utawatowesha kama ndoto.
21 En ese tiempo mis pensamientos se volvieron amargos. Me sentí atravesado con cuchillos.
Wakati moyo wangu ulipohuzunishwa, na roho yangu ilipotiwa uchungu,
22 Era necio e ignorante. Como una bestia salvaje delante de ti.
nilikuwa mpumbavu na mjinga, nilikuwa mnyama mkatili mbele yako.
23 Sin embargo, siempre estoy contigo, y tú sostienes mi mano.
Hata hivyo niko pamoja nawe siku zote, umenishika mkono wangu wa kuume.
24 Tú me dices qué hacer, y al final me recibirás en tu gloria.
Unaniongoza kwa shauri lako, hatimaye utaniingiza katika utukufu.
25 ¿A quién más he de ver en el cielo si no a ti? Y en la tierra no anhelo nada sino a ti.
Nani niliye naye mbinguni ila wewe? Dunia haina chochote ninachokitamani ila wewe.
26 Mi cuerpo y mi mente podrás fallar, pero Dios es el fundamento de mi vida. Él es mío para siempre!
Mwili na moyo wangu vyaweza kushindwa, bali Mungu ni nguvu ya moyo wangu na fungu langu milele.
27 Los que están lejos de Dios morirán. Tú destruirás a los que te son infieles.
Wale walio mbali nawe wataangamia, unawaangamiza wote wasio waaminifu kwako.
28 ¡Pero yo amo estar cerca de Dios! He elegido al Señor Dios como mi protector, y contaré todo lo que has hecho.
Lakini kwangu mimi, ni vyema kuwa karibu na Mungu. Nimemfanya Bwana Mwenyezi kimbilio langu; nami nitayasimulia matendo yako yote.

< Salmos 73 >