< Salmos 63 >

1 Un salmo de David, cuando estaba en el desierto de Judá. Dios, tú eres mi Dios y te busco de todo corazón. Mi ser entero te anhela y tiene sed de ti, en medio de esta tierra seca, árida y carente de aguas.
Zaburi ya Daudi. Wakati alipokuwa katika Jangwa la Yuda. Ee Mungu, wewe ni Mungu wangu, nakutafuta kwa moyo wote; nafsi yangu inakuonea kiu, mwili wangu unakuonea wewe shauku, katika nchi kame na iliyochoka mahali ambapo hapana maji.
2 Te veo en el Templo. Contemplo tu poder y tu gloria.
Nimekuona katika mahali patakatifu na kuuona uwezo wako na utukufu wako.
3 Tu fidelidad y amor son mejores que la vida misma. Por ello te alabaré.
Kwa sababu upendo wako ni bora kuliko uhai, midomo yangu itakuadhimisha.
4 Te agradeceré tanto como viva. Elevo mis manos hacia ti y celebro tu maravilloso carácter.
Nitakusifu siku zote za maisha yangu, na kwa jina lako nitainua mikono yangu.
5 Tú me satisfaces más que el mejor de los alimentos. Te alabaré con canciones alegres.
Nafsi yangu itatoshelezwa kama kwa wingi wa vyakula; kwa midomo iimbayo kinywa changu kitakusifu wewe.
6 Paso la noche entera pensando en ti desde que me acuesto, meditando sobre ti.
Kitandani mwangu ninakukumbuka wewe, ninawaza juu yako makesha yote ya usiku.
7 Porque eres quien me ayuda, canto feliz bajo tus alas.
Kwa sababu wewe ndiwe msaada wangu, chini ya uvuli wa mbawa zako naimba.
8 Me aferro a ti y tus fuertes brazos me levantan.
Nafsi yangu inaambatana nawe, mkono wako wa kuume hunishika.
9 Los que tratan de destruirme irán a la tumba.
Wale wanaotafuta uhai wangu wataharibiwa, watakwenda chini kwenye vilindi vya dunia.
10 Morirán a punta de espada y serán alimento para los chacales.
Watatolewa wafe kwa upanga, nao watakuwa chakula cha mbweha.
11 Pero el rey vivirá feliz por todo lo que Dios ha hecho. Todos los que siguen a Dios le alabarán, pero los que mienten serán silenciados.
Bali mfalme atafurahi katika Mungu, wale wote waapao kwa jina la Mungu watamsifu, bali vinywa vya waongo vitanyamazishwa.

< Salmos 63 >