< Salmos 6 >

1 Para el director del coro. Para acompañamiento de instrumentos de cuerda según el Seminit. Un salmo de David. Señor, por favor, no me condenes por causa de tu enojo hacia mi; por favor, no me castigues con tu ira.
Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Mtindo wa sheminithi. Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, usinikemee katika hasira yako, wala usiniadhibu katika ghadhabu yako.
2 Ten misericordia de mi, Señor, porque estoy débil; sáname, Señor, porque estoy enfermo hasta los huesos.
Unirehemu Bwana, kwa maana nimedhoofika; Ee Bwana, uniponye, kwa maana mifupa yangu ina maumivu makali.
3 Tiemblo de miedo. ¿Hasta cuándo Señor, harás algo?
Nafsi yangu ina uchungu mwingi. Mpaka lini, Ee Bwana, mpaka lini?
4 Vuélvete hacia mi, Señor, ¡y rescátame! ¡Sálvame por tu gran amor!
Geuka Ee Bwana, unikomboe, uniokoe kwa sababu ya fadhili zako.
5 Porque nadie recuerda cuando ya está muerto. ¿Quién podrá alabarte desde el sepulcro? (Sheol h7585)
Hakuna mtu anayekukumbuka akiwa amekufa. Ni nani awezaye kukusifu akiwa kuzimu? (Sheol h7585)
6 Mis gemidos me han consumido. Cada noche mi cama se inunda con mi llanto, y mi sillón rebosa con mis lágrimas.
Nimechakaa kwa kulia kwa huzuni; usiku kucha nafurikisha kitanda changu kwa machozi; nimelowesha viti vyangu vya fahari kwa machozi.
7 De tanto llorar no puedo casi ni ver. Mis ojos se debilitan por la agonía que me causan mis enemigos.
Macho yangu yamedhoofika kwa kuhuzunika, yamedhoofika kwa sababu ya adui zangu wote.
8 Déjenme en paz, pueblo que hace el mal. Porque el Señor ha escuchado mi llanto.
Kaeni mbali nami, ninyi nyote mtendao mabaya, kwa maana Bwana amesikia kulia kwangu.
9 El Señor ha escuchado mi ruego de ayuda, y él responde mi oración.
Bwana amesikia kilio changu kwa huruma, Bwana amekubali sala yangu.
10 Todos los que me odian serán vencidos y aterrorizados con gran vergüenza, y huirán con gran humillación.
Adui zangu wote wataaibika na kufadhaika, watarudi nyuma kwa aibu ya ghafula.

< Salmos 6 >