< Salmos 34 >
1 Un salmo de David sobre la vez que aparentó estar loco frente a Abimelec, quien lo echó de su presencia. Siempre alabaré al Señor; mi boca continuamente lo alabará.
Zaburi ya Daudi, alipojifanya mwendawazimu mbele ya Abimeleki, ambaye alimfukuza, naye akaondoka. Nitamtukuza Bwana nyakati zote, sifa zake zitakuwa midomoni mwangu siku zote.
2 Estoy orgulloso del Señor desde lo profundo de mi corazón; aquellos que son humildes oirán y serán felices.
Nafsi yangu itajisifu katika Bwana, walioonewa watasikia na wafurahi.
3 Glorifiquen al Señor conmigo; honremos juntos su nombre.
Mtukuzeni Bwana pamoja nami, naam, na tulitukuze jina lake pamoja.
4 Clamé al Señor por ayuda, y él me respondió. Me liberó de todos mis miedos.
Nilimtafuta Bwana naye akanijibu, akaniokoa kwenye hofu zangu zote.
5 Las caras de aquellos que lo miran brillaran de alegría. Nunca serán abatidos con vergüenza.
Wale wamtazamao hutiwa nuru, nyuso zao hazifunikwi na aibu kamwe.
6 Este pobre hombre lloró, y el Señor me oyó, y me salvó de todos mis problemas.
Maskini huyu alimwita Bwana, naye akamsikia, akamwokoa katika taabu zake zote.
7 El ángel del Señor permanece vigilante sobre los que le honran, manteniéndolos a salvo.
Malaika wa Bwana hufanya kituo akiwazunguka wale wamchao, naye huwaokoa.
8 ¡Prueba, y verás que el Señor es bueno! ¡Cuán felices son los que creen su protección!
Onjeni mwone kwamba Bwana ni mwema, heri mtu yule anayemkimbilia.
9 Muestra tu reverencia al Señor, tú que eres su pueblo santo, porque a los que lo respetan no les faltará nada.
Mcheni Bwana enyi watakatifu wake, kwa maana wale wamchao hawapungukiwi na chochote.
10 Los leones pueden crecer débiles y hambrientos, pero los que confían en el Señor tienen todo lo que es bueno.
Wana simba wenye nguvu hutindikiwa na kuona njaa, bali wale wamtafutao Bwana hawatakosa kitu chochote kilicho chema.
11 ¡Niños, escúchenme! Les enseñaré como respetar al Señor.
Njooni, watoto wangu, mnisikilize, nitawafundisha kumcha Bwana.
12 ¿Quién de ustedes quiere vivir una vida larga y feliz?
Yeyote kati yenu anayependa uzima na kutamani kuziona siku nyingi njema,
13 Entonces no dejen que sus lenguas hablen maldad, o que sus labios digan mentiras.
basi auzuie ulimi wake na mabaya, na midomo yake kutokana na kusema uongo.
14 Rechacen lo malo, hagan lo bueno. Busquen la paz, y trabajen para hacerla realidad.
Aache uovu, atende mema, aitafute amani na kuifuatilia.
15 El Señor cuida a los que hacen lo correcto, y escucha cuando claman por ayuda.
Macho ya Bwana huwaelekea wenye haki, na masikio yake yako makini kusikiliza kilio chao.
16 El Señor es enemigo de los que hacen el mal. Él borrará hasta la memoria de ellos de la tierra.
Uso wa Bwana uko kinyume na watendao maovu, ili kufuta kumbukumbu lao duniani.
17 Pero cuando su pueblo llama pidiendo ayuda, él los escucha y los rescata de sus problemas.
Wenye haki hulia, naye Bwana huwasikia, huwaokoa katika taabu zao zote.
18 El Señor está cerca de los que tienen el corazón roto. Él salva a aquellos cuyo espíritu está quebrantado.
Bwana yu karibu na waliovunjika moyo, na huwaokoa waliopondeka roho.
19 Aquellos que hacen lo correcto tienen muchos problemas, pero el Señor los resuelve todos.
Mwenye haki ana mateso mengi, lakini Bwana humwokoa nayo yote,
20 Él los mantiene a salvo, ni uno de sus huesos se romperá.
huhifadhi mifupa yake yote, hata mmoja hautavunjika.
21 La maldad mata a los malvados. Aquellos que odian a la gente buena sufrirán por sus malos actos.
Ubaya utamuua mtu mwovu, nao adui za mwenye haki watahukumiwa.
22 El Señor protege la vida de sus siervos. Aquellos que confían en su protección no sufrirán por sus acciones equivocadas.
Bwana huwakomboa watumishi wake, yeyote anayemkimbilia yeye hatahukumiwa kamwe.