< Salmos 26 >

1 Un Salmo de David. Confirma que soy inocente, Señor, porque he actuado con integridad, y he confiado en el Señor sin falta.
Zaburi ya Daudi. Ee Bwana, nithibitishe katika haki, maana nimeishi maisha yasiyo na lawama; nimemtumainia Bwana bila kusitasita.
2 Examíname, Señor, pruébame; investiga mi corazón y mi mente.
Ee Bwana, unijaribu, unipime, uuchunguze moyo wangu na mawazo yangu;
3 Porque yo siempre recuerdo tu amor fiel, y sigo tu verdad.
kwa maana upendo wako uko mbele yangu daima, nami natembea siku zote katika kweli yako.
4 No me junto con mentirosos, ni me asocio con hipócritas.
Siketi pamoja na watu wadanganyifu, wala siandamani na wanafiki,
5 Me rehúso a estar junto a aquellos que hacen el mal, y no me veré envuelto con los malvados.
ninachukia kusanyiko la watenda mabaya na ninakataa kuketi pamoja na waovu.
6 Lavo mis manos para mostrar mi inocencia. Vengo a adorar a tu altar, Señor,
Ninanawa mikono yangu kwa kuwa sina hatia, naikaribia madhabahu yako, Ee Bwana,
7 cantando mis agradecimientos, contando todas las cosas maravillosas cosas que has hecho.
nikitangaza sifa yako kwa sauti kubwa, huku nikisimulia matendo yako ya ajabu.
8 Señor, amo tu casa, el lugar donde vives en tu gloria.
Ee Bwana, naipenda nyumba yako mahali unakoishi, mahali ambapo utukufu wako hukaa.
9 Por favor, no me lances lejos con los pecadores. No me incluyas con aquellos que cometieron asesinatos,
Usiiondoe nafsi yangu pamoja na watenda dhambi, wala uhai wangu pamoja na wamwagao damu,
10 y cuyas manos cargan sus planes malvados y sobornos.
ambao mikononi mwao kuna mipango miovu, ambao mikono yao ya kuume imejaa rushwa.
11 Porque yo no hago eso, yo actúo con integridad. ¡Sálvame, y ten gracia conmigo!
Bali mimi ninaishi maisha yasiyo na lawama; nikomboe na unihurumie.
12 Estoy a favor de lo que es correcto, y alabaré al Señor cuando nos reunamos a adorarle.
Miguu yangu imesimama katika uwanja tambarare; katika kusanyiko kuu nitamsifu Bwana.

< Salmos 26 >