< Salmos 2 >

1 ¿Por qué traman rebelión las naciones? Los pueblos conspiran, pero sin ningún sentido.
Kwa nini mataifa wanashauriana kufanya mabaya, na kabila za watu kula njama bure?
2 Los reyes del mundo se preparan para el ataque, y los gobernantes se reúnen para conspirar contra el Señor y su ungido, diciendo:
Wafalme wa dunia wanajipanga na watawala wanajikusanya pamoja dhidi ya Bwana na dhidi ya Mpakwa Mafuta wake.
3 “Rompamos las cadenas y desechemos las cuerdas que nos atan”
Wanasema, “Tuvunje minyororo yao na kuvitupilia mbali vifungo vyao.”
4 Pero el que se sienta en el trono hasta se ríe. El Señor se ríe de ellos.
Yeye atawalaye mbinguni hucheka, Bwana huwadharau.
5 Con un trueno los espantará en medio de su furia, diciendo:
Kisha huwakemea katika hasira yake na kuwaogopesha katika ghadhabu yake, akisema,
6 “Yo soy quien puso a mi rey en Sión, mi monte sagrado”.
“Nimemtawaza Mfalme wangu juu ya Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
7 “Yo proclamaré el decreto del Señor”, dice el rey. “Él me dijo: ‘Tú eres mi hijo. Hoy me he convertido en tu padre.
Nitatangaza amri ya Bwana: Yeye aliniambia, “Wewe ni Mwanangu, leo mimi nimekuzaa.
8 Si me lo pides, te daré las naciones como posesión. Toda la tierra será tuya.
Niombe, nami nitayafanya mataifa kuwa urithi wako, miisho ya dunia kuwa milki yako.
9 Los quebrantarás con vara de hierro, y como vasija de barro los desmenuzarás’”.
Utawatawala kwa fimbo ya chuma na kuwavunjavunja kama chombo cha mfinyanzi.”
10 Entonces, ustedes los reyes, ¡Actúen con sabiduría! ¡Estén advertidos, gobernantes de la tierra!
Kwa hiyo, ninyi wafalme, kuweni na hekima; mwonyeke, enyi watawala wa dunia.
11 ¡Sirvan al Señor con reverencia, y alégrense con temblor!
Mtumikieni Bwana kwa hofu na mshangilie kwa kutetemeka.
12 Sométanse a su hijo para que no se enoje y mueran repentinamente. Su ira se inflama de repente, pero felices son los que acuden a él buscando protección.
Mbusu Mwana, asije akakasirika nawe ukaangamizwa katika njia yako, kwa maana hasira yake inaweza kuwaka ghafula. Heri wote wanaomkimbilia.

< Salmos 2 >