< Salmos 120 >

1 Un cántico para los peregrinos que van a Jerusalén. Clamé al Señor en medio de todas mis tribulaciones, y Él me contestó.
Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
2 ¡Señor, por favor sálvame de los mentirosos y de los engañadores!
Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
3 ¿Qué hará el Señor con ustedes, mentirosos? ¿Cómo los castigará?
Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
4 Con la espada afilada de un guerrero y carbones encendidos de un enebro.
Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
5 ¡Ay de mí! Que soy extranjero en Meséc, que he acampado entre las tiendas de Cedar.
Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
6 He vivido por mucho tiempo entre los pueblos que odian la paz.
Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
7 Quiero paz, pero cuando hablo de paz, ellos quieren guerra.
Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.

< Salmos 120 >