< Salmos 110 >

1 Un salmo de David. El Señor dijo a mi Señor, “Siéntate a mi derecha, hasta que haga de tus enemigos un estrado para ti”.
Zaburi ya Daudi. Bwana amwambia Bwana wangu: “Keti mkono wangu wa kuume, mpaka nitakapowafanya adui zako kuwa mahali pa kuweka miguu yako.”
2 El Señor extenderá tu poderío desde Sión; y gobernarás sobre tus enemigos.
Bwana ataeneza fimbo yako ya utawala yenye nguvu kutoka Sayuni; utatawala katikati ya adui zako.
3 Tu pueblo te seguirá en el día en que tu poder sea revelado en las montañas santas, renovado en fuerza cada mañana como el rocío al amanecer.
Askari wako watajitolea kwa hiari katika siku yako ya vita. Ukiwa umevikwa fahari takatifu, kutoka tumbo la mapambazuko utapokea umande wa ujana wako.
4 El Señor ha hecho un pacto que no romperá: “Eres un sacerdote para siempre, siguiendo la orden de Melquisedec”.
Bwana ameapa, naye hatabadilisha mawazo yake: “Wewe ni kuhani milele, kwa mfano wa Melkizedeki.”
5 El Señor permanece a tu lado para apoyarte; derribará a reyes en su ira.
Bwana yuko mkono wako wa kuume, atawaponda wafalme siku ya ghadhabu yake.
6 Ejecutará juicios en las naciones, llenando sus tierras con cadáveres. Derrotará a los que gobiernan toda la tierra.
Atawahukumu mataifa, akilundika mizoga na kuwaponda watawala wa dunia nzima.
7 Él beberá de arroyos ante el camino. Por lo tanto, será victorioso.
Atakunywa maji katika kijito kando ya njia, kwa hiyo atainua kichwa chake juu.

< Salmos 110 >