< Salmos 108 >

1 Una canción. Un salmo de David. ¡Oh, Dios! ¡He confiado plenamente en ti! ¡Todo mi ser canta alabanzas a tu nombre!
Wimbo. Zaburi ya Daudi. Ee Mungu, moyo wangu ni thabiti; nitaimba na kusifu kwa moyo wangu wote.
2 ¡Levántense, arpa y lira! ¡Despertaré al amanecer!
Amka, kinubi na zeze! Nitayaamsha mapambazuko.
3 Te agradeceré entre los pueblos, Señor, cantaré alabanzas a ti entre las naciones.
Nitakusifu wewe, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaimba habari zako, katikati ya jamaa za watu.
4 Porque tu gran amor llega más alto que los cielos, tu fidelidad es más grande que las nubes.
Kwa maana upendo wako ni mkuu, ni juu kuliko mbingu; uaminifu wako unazifikia anga.
5 Dios, tu grandeza sobrepasa los cielos, y tu gloria está sobre toda la tierra.
Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu, utukufu wako na uenee duniani kote.
6 ¡Rescata a los que amas! Respóndenos, y sálvanos con tu poder!
Tuokoe na utusaidie kwa mkono wako wa kuume, ili wale uwapendao wapate kuokolewa.
7 Dios ha hablado desde su Templo: “He dividido triunfantemente a Siquem y parte del Valle de Sucot.
Mungu amenena kutoka patakatifu pake: “Nitaigawa Shekemu kwa ushindi na kulipima Bonde la Sukothi.
8 Tanto Gilead como Manasés me pertenecen. Efraín es mi casco, y Judá es mi cetro.
Gileadi ni yangu, Manase ni yangu, Efraimu ni kofia yangu ya chuma, nayo Yuda ni fimbo yangu ya utawala.
9 Trataré a Moab como mi lavabo; pondré mi sandalia sobre Edom; gritaré en triunfo sobre Filistea”.
Moabu ni sinia langu la kunawia, juu ya Edomu natupa kiatu changu; nashangilia kwa kushindwa kwa Ufilisti.”
10 ¿Quién me traerá a la ciudad fortificada? ¿Quién me guiará a Edom?
Ni nani atakayenipeleka hadi mji wenye ngome? Ni nani atakayeniongoza hadi nifike Edomu?
11 ¿Nos has rechazado, Dios? ¿No dirigirás a tus ejércitos nunca más?
Ee Mungu, si ni wewe uliyetukataa sisi, na hutoki tena na majeshi yetu?
12 Bríndanos, por favor, una mano de ayuda en contra de nuestros enemigos, porque la ayuda humana no vale la pena.
Tuletee msaada dhidi ya adui, kwa maana msaada wa mwanadamu haufai kitu.
13 Nuestra fuerza está en Dios, y él destruirá a nuestros enemigos.
Kwa msaada wa Mungu tutapata ushindi, naye atawaponda adui zetu.

< Salmos 108 >