< Salmos 107 >

1 ¡Agradezcan al Señor, porque él es bueno! ¡Su misericordioso amor perdura para siempre!
Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
2 Que todos a los que salvó salgan a gritarle al mundo; aquellos a quienes rescató del poder del enemigo.
Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
3 Los ha reunido desde tierras lejanas, desde el este y el oeste, y del norte y el sur.
wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
4 Ellos vagaron por el árido desierto, sin encontrar una sola ciudad en la que vivir.
Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
5 Hambrientos y sedientos, se desanimaron.
Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
6 Entonces clamaron al Señor para que los ayudara, y los salvó de su sufrimiento.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
7 Los guió por un camino directo a la ciudad donde podrían vivir.
Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
8 Alaben al Señor por su gran amor, y por todas las cosas hermosas que hace por la gente.
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
9 Porque brinda agua al sediento, y alimenta a los hambrientos.
kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
10 Algunos se sientan en completas tinieblas, prisioneros de la miseria y atados con cadenas de hierro,
Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
11 Porque se han revelado contra lo que Dios ha dicho; han rechazado la dirección del Altísimo.
kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
12 Entonces Dios humillará su orgullo con los problemas de la vida; tropezarán y no habrá nadie cerca que los ayude a no caer.
Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
13 Y llamarán al Señor en medio de sus problemas, y los salvará de su sufrimiento.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
14 Los traerá de vuelta desde las tinieblas, romperá en pedazos sus cadenas.
Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
15 Alaben al Señor por su gran amor, y por todas las cosas hermosas que hace por la gente.
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
16 Porque Él rompe las puertas de bronce, y corta las barras de hierro.
kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
17 Ellos fueron necios al rebelarse; y sufrieron por sus pecados.
Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
18 No quisieron comer; y estuvieron a las puertas de la muerte.
Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
19 Entonces llamaron al Señor para que los ayudara, y Él los salvó de su sufrimiento.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
20 Dio la orden y fueron sanados; los salvó de la tumba.
Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
21 Alaben al Señor por su gran amor, y por todas las cosas hermosas que hace por la gente.
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
22 Preséntense ante él con ofrendas de gratitud y canten de alegría sobre lo que ha hecho.
Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
23 Los que zarpan en barcos, y cruzan océanos para ganar la vida,
Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
24 ellos han visto el increíble poder de Dios en marcha, y las maravillas que hizo en aguas profundas.
Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
25 Él solo tiene que hablar para causar vientos tormentosos y levantar grandes olas,
Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
26 Lanzando a los barcos al aire y luego arrastrándolos una vez más al suelo. Los navegantes estaban tan aterrorizados que su coraje se desvaneció.
Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
27 Se tambalearon, cayendo de lado a lado como ebrios, todas sus habilidades de marineros les fueron inútiles.
Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
28 Entonces llamaron al Señor para que los ayudara, y Él los salvó de su sufrimiento.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
29 Calmó la tempestad, y las olas se aquietaron.
Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
30 Los navegantes estaban tan felices de que las aguas se hubieran calmado, y el Señor los llevó hasta el puerto que querían.
Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
31 Alaben al Señor por su gran amor, y por todas las cosas hermosas que ha hecho por su pueblo.
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
32 Digan cuán maravilloso es en frente de toda la congregación y de los ancianos.
Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
33 Él seca ríos y convierte tierras en desiertos; las cascadas de agua dejan de fluir y la tierra se vuelve seca y polvorienta.
Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
34 Los terrenos fructíferos se convierten tierras arenosas y baldías a causa de la maldad de los que allí vivían.
nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
35 Pero Él también se vuelve y hace lagunas de agua en mitad del desierto, y hace fluir cascadas en tierras secas.
Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
36 Trae a la gente hambrienta a un lugar donde pueden reconstruir sus ciudades.
aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
37 Ellos siembran sus campos y plantan viñas, produciendo buena cosecha.
Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
38 Él cuida de su pueblo, y este aumenta su tamaño drásticamente, también el número de sus ganados!
Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
39 Cuando son pocos, reducidos por el dolor, la miseria y la opresión.
Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
40 Derrama su desprecio hacia sus líderes, haciéndolos vagar, perdidos en el desierto.
Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
41 Pero Él saca al pobre de sus problemas, y hace a sus familias tan grandes como los rebaños.
Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
42 Los que viven en rectitud mirarán lo que está pasando y se alegrarán, pero los malvados serán silenciados.
Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
43 Aquellos que son sabios prestarán atención a esto, y meditarán en el gran amor de Dios.
Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.

< Salmos 107 >