< Proverbios 9 >
1 La sabiduría ha construido su casa, ha preparado sus siete pilares.
Hekima amejenga nyumba yake; amechonga nguzo zake saba.
2 Ella ha sacrificado a sus animales para obtener su carne; ha mezclado su vino y ha alistado la mesa.
Ameandaa nyama na kuchanganya divai yake; pia ameandaa meza yake.
3 Ha enviado a sus siervas con invitaciones. Llama desde los lugares altos de la ciudad, diciendo:
Amewatuma watumishi wake wa kike, naye huita kutoka mahali pa juu sana pa mji.
4 “¡Todos los que necesiten aprender, vengan a mi!” A los insensatos les dice:
Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa!
5 “Vengan, coman mi carne y beban del vino que he mezclado.
Njooni, mle chakula changu na mnywe divai niliyoichanganya.
6 Dejen de vivir con necedad, y sigan el camino de la sensatez”.
Acheni njia zenu za ujinga nanyi mtaishi; tembeeni katika njia ya ufahamu.
7 Si corriges al burlador, recibirás insultos; si corriges al malvado por lo que hace, recibirás abuso.
“Yeyote anayemkosoa mwenye mzaha hukaribisha matukano; yeyote anayekemea mtu mwovu hupatwa na matusi.
8 Por lo tanto, no discutas con los burladores, pues solo te odiarán; discute con el sabio y te amará.
Usimkemee mwenye mzaha la sivyo atakuchukia; mkemee mwenye hekima naye atakupenda.
9 Educa al sabio y se volverá más sabio. Enseña a los que viven en rectitud y aumentarán su conocimiento.
Mfundishe mtu mwenye hekima naye atakuwa na hekima zaidi; mfundishe mtu mwadilifu naye atazidi kufundishika.
10 El principio de la sabiduría es honrar a Dios. Y el conocimiento del Santo trae inteligencia.
“Kumcha Bwana ndicho chanzo cha hekima, na kumjua Aliye Mtakatifu ni ufahamu.
11 Mediante la sabiduría vivirás muchos años más. Añadirás años a tu vida.
Kwa maana kwa msaada wangu siku zako zitakuwa nyingi, na miaka itaongezwa katika maisha yako.
12 Si eres sabio, tú obtendrás los beneficios de la sabiduría, pero si eres un burlador, solo tú sufrirás las consecuencias.
Kama wewe una hekima, hekima yako itakupa tuzo; kama wewe ni mtu wa mzaha, wewe mwenyewe ndiwe utateseka.”
13 La estupidez es como una mujer escandalosa e ignorante.
Mwanamke aitwaye Mpumbavu ana kelele; hana adabu na hana maarifa.
14 Esa que se sienta en la puerta de su casa, se sienta en los lugares altos de la ciudad,
Huketi kwenye mlango wa nyumba yake, juu ya kiti katika mahali pa juu sana pa mji,
15 llamando a los que pasan, involucrándose en asuntos ajenos, y diciendo:
akiita wale wapitao karibu, waendao moja kwa moja kwenye njia yao.
16 “¡Los que necesiten aprender, vengan a mi!” A los necios les dice:
Anawaambia wale wasio na akili, “Wote ambao ni wajinga na waje hapa ndani!”
17 “El agua robada es dulce, y la comida que se come en secreto sabe mejor!”
“Maji yaliyoibiwa ni matamu; chakula kinacholiwa sirini ni kitamu!”
18 Pero ellos no saben que los Muertos están con ella, que aquellos a quienes ella ha invitado antes están en lo profundo de una tumba. (Sheol )
Lakini hawajui hata kidogo kuwa wafu wako humo, kwamba wageni wake huyo mwanamke wako katika vilindi vya kuzimu. (Sheol )