< Proverbios 8 >

1 ¿No llama la sabiduría? ¿No alza su voz el entendimiento?
Je hekima haiti? Je ufahamu hapazi sauti yake?
2 En lo alto de la colina, se pone en pie junto al camino, y sobre en las encrucijadas.
Juu ya kilima kando ya barabara, kwenye njia panda, hekima anasimama.
3 A las puertas de la ciudad, en la entrada grita:
Kando ya njia ya kuingilia mjini, karibu na milango ya mji, anaita kwa sauti.
4 “¡Los estoy llamando a todos ustedes! ¡A todos los habitantes del mundo!
Watu, ninawaita ninyi na ninapaza sauti yangu kwa wana wa wanadamu.
5 Si eres inmaduro, aprende a crecer. Si eres tonto, aprende y vuélvete inteligente.
Ninyi wajinga, jifunzeni hekima, na ninyi mnaochukia maarifa, lazima mjipatieni moyo wa ufahamu.
6 Escúchame porque tengo valiosas cosas que explicarte.
Sikiliza na mimi nitasema mambo mazuri na nifumbuapo midomo yangu nitaongea haki.
7 Yo digo lo correcto, porque digo la verdad y odio la maldad en todas sus formas.
Maana kinywa changu hunena uaminifu na midomo yangu huchukia uovu.
8 Todas mis palabras son verdaderas, y ninguna es falsa ni engañosa.
Maneno ya kinywa changu yote ni haki; hakuna kilichogeuzwa wala kupotoshwa.
9 Mis palabras son fáciles de entender para todo el que tiene entendimiento. Son rectas para el que tiene conocimiento.
Maneno yangu yote yamenyooka kwa yule mwenye kuelewa; maneno yangu ni haki kwa wale wanaotafuta maarifa.
10 Elige mi enseñanza por encima de la plata; elige el conocimiento más que el oro puro.
Chagua fundisho langu badala ya fedha na maarifa kuliko dhahabu safi.
11 Porque la sabiduría es más valiosa que los rubíes. ¡Nada de lo que puedas desear se compara a ella!
Maana mimi, hekima ni bora kuliko vito; hakuna unachokitamani kinaweza kulinganishwa na mimi.
12 “Yo, la sabiduría, vivo con las buenas decisiones. Sé como hallar el conocimiento y el discernimiento.
Mimi, hekima, naishi kwa utaratibu, na ninamiliki maarifa na busara.
13 Honrar al Señor significa aborrecer el mal. Por ello aborrezco el orgullo y la arrogancia, la conducta malvada y el decir mentiras.
Hofu ya Mungu ni kuchukia uovu- nachukia majivuno na kiburi, njia ya uovu, na kauli iliyopotoka- hivyo ninavichukia.
14 Tengo el consejo y el buen juicio. Conmigo está la inteligencia y el poder.
Ninaushauri mzuri na hekima sahihi; mimi ni busara; nguvu zipo kwangu.
15 Gracias a mi los reyes reinan, y los gobernantes emiten decretos justos.
Kwa njia yangu wafalme hutawala- pia na waungwana, na wote ambao hutawala kwa haki.
16 Gracias a mi los líderes y nobles pueden gobernar, así como todos los que gobiernan con justicia.
Kwa njia yangu wafalme hutawala na waungwana na wote wanaotawala kwa haki.
17 Amo a los que me aman, y los que me buscan de corazón me encontrarán.
Nawapenda wale wanaonipenda, na wale wanaonitafuta kwa bidii, wataniona.
18 Conmigo está la riqueza y el honor, así como la riqueza y prosperidad duraderas.
Kwangu kunautajiri na heshima, utajiri wa kudumu na haki.
19 El fruto que produzco es mejor que el oro, incluso que el oro puro, y mi cosecha es mejor que la plata más fina.
Tunda langu ni bora kuliko dhahabu, bora hata kuliko dhahabu safi.
20 Vivo con rectitud, y sigo los caminos de la justicia.
Ninazalisha kilicho bora kuliko fedha safi. Natembea katika njia ya haki,
21 Yo otorgo riqueza a los que me aman, y lleno sus almacenes de tesoros.
katika mapito ambayo huelekea kwenye haki, ili niwape urithi wale wanaonipenda na kuzijaza hazina zao.
22 “El Señor me creó desde el principio. Fui creada antes que cualquier otra cosa.
Yehova aliniumba tokea mwanzo- mwazoni mwa matendo yake ya nyakati za kale.
23 Fui formada hace mucho tiempo, desde el principio, y antes de que el mundo existiera.
Tokea enzi za kale niliwekwa katika nafasi- tokea kwanza, tokea mwanzo wa dunia.
24 Nací cuando no había profundidades en el océano, cuando no había fuentes de aguas.
Kabla ya bahari, mimi nilizaliwa- kabla ya kuwepo chemchemi zenye maji tele.
25 Nací antes de que se formaran las montañas y colinas,
Kabla ya milima na vilima kuwekwa, mimi nilizaliwa.
26 aun antes de que él hiciera la tierra y sus campos, o siquiera el polvo de la tierra.
Nilizaliwa kabla ya Yehova hajaiumba dunia wala makonde, hata mavumbi ya kwanza katika dunia.
27 Estuve allí cuando los cielos fueron puestos en su lugar, cuando él dibujó el horizonte sobre el océano,
Nilikuwepo alipoziimarisha mbingu, wakati alipochora mstari katika sura ya kilindi.
28 cuando puso las nubes arriba en el cielo, y cuando creó las fuentes de los océanos.
Nilikuwepo alipoimarisha anga la juu na wakati wa kutengeneza kina cha chemchemi.
29 Cuando estableció los límites del mar para que no se saliera más allá de su voluntad, y cuando estableció los fundamentos de la tierra.
Nilikuwepo alipotengeneza mipaka ya bahari, ili maji yasisambae kuvuka pale alipoyaamuru, na wakati anaamuru misingi ya dunia sehemu ya kukaa.
30 En ese tiempo estaba a su lado, como maestro artesano. Lo alegraba todos los días, y yo sentía siempre alegría en su presencia.
Nilikuwa kando yake, kama fundistadi mkuu, na mimi nilikuwa furaha yake siku kwa siku, nikifurahi mbele zake daima.
31 Estuve muy feliz en el mundo que creó, y celebrábamos juntos con los seres humanos.
Nilikuwa nikifurahi katika dunia yake yote na furaha yangu ilikuwa kwa wana wa wanadamu.
32 “Ahora, hijos míos, escúchenme, porque los que siguen mis caminos son felices.
Na sasa, wanangu, nisikilizeni, maana wale wazishikao njia zangu watakuwa na furaha.
33 Escuchen mis instrucciones y sean sabios. No rechacen mi instrucción
Sikilizeni fundisho langu na mpate hekima; wala msilipuuze.
34 Felices son los que me escuchan, los que están pendientes en mi puerta para verme llegar.
Anisikilizaye atakuwa na furaha- kila siku akitazama katika malango yangu, akinisubiri pembeni mwa milango ya masikani yangu.
35 Porque los que me encuentran, encuentran la vida, y son aceptados por el Señor.
Maana yeyote anionaye mimi, anapata uzima, naye atapata kibali kwa Yehova.
36 Pero los que no me encuentran se hacen daño a sí mismos, pues todos los que me aborrecen aman la muerte”.
Na yeyote asiyeniona mimi, hujiumiza mwenyewe, wote wanaonichukia hupenda mauti.

< Proverbios 8 >