< Proverbios 3 >

1 Hijo mío, no olvides mis instrucciones. Recuerda siempre mis mandamientos.
Mwanangu, usisahau mafundisho yangu, bali zitunze amri zangu moyoni mwako,
2 Así vivirás muchos años, y tu vida será plena.
kwa kuwa zitakuongezea miaka mingi ya maisha yako na kukuletea mafanikio.
3 Aférrate a la bondad y a la verdad. Átalas a tu cuello y escríbelas en tu mente.
Usiache kamwe upendo na uaminifu vitengane nawe; vifunge shingoni mwako, viandike katika ubao wa moyo wako.
4 Así tendrás buena reputación y serás apreciado por Dios y la gente.
Ndipo utapata kibali na jina zuri mbele za Mungu na mwanadamu.
5 Pon tu confianza totalmente en el Señor, y no te fíes de lo que crees saber.
Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote wala usizitegemee akili zako mwenyewe;
6 Recuérdalo en todo lo que hagas, y él te mostrará el camino correcto.
katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyoosha mapito yako.
7 No te creas sabio, respeta a Dios y evita el mal.
Usiwe mwenye hekima machoni pako mwenyewe; mche Bwana ukajiepushe na uovu.
8 Entonces serás sanado y fortalecido.
Hii itakuletea afya mwilini mwako, na mafuta kwenye mifupa yako.
9 Honra al Señor con tu riqueza y con los primeros frutos de tus cosechas.
Mheshimu Bwana kwa mali zako na kwa malimbuko ya mazao yako yote;
10 Entonces tus graneros serán llenos de fruto, y tus estanques rebosarán de vino nuevo.
ndipo ghala zako zitakapojaa hadi kufurika, viriba vyako vitafurika kwa mvinyo mpya.
11 Hijo mío, no rechaces la disciplina del Señor ni te enojes cuando te corrija,
Mwanangu, usiidharau adhabu ya Bwana na usichukie kukaripiwa naye,
12 porque el Señor corrige a los que ama, así como un padre corrige al hijo que más le agrada.
kwa sababu Bwana huwaadibisha wale awapendao, kama vile baba afanyavyo kwa mwana apendezwaye naye.
13 Felices son los que encuentran la sabiduría y obtienen entendimiento,
Heri mtu yule aonaye hekima, mtu yule apataye ufahamu,
14 porque la sabiduría vale más que la plata, y ofrece mejor recompensa que el oro.
kwa maana hekima ana faida kuliko fedha na mapato yake ni bora kuliko ya dhahabu safi.
15 ¡La sabiduría vale más que muchos rubíes y no se compara con ninguna cosa que puedas imaginar!
Hekima ana thamani kuliko marijani; hakuna chochote unachokitamani kinachoweza kulinganishwa naye.
16 Por un lado ella te brinda larga vida, y por el otro riquezas y honra.
Maisha marefu yako katika mkono wake wa kuume; katika mkono wake wa kushoto kuna utajiri na heshima.
17 Te dará verdadera felicidad, y te guiará a una prosperidad llena de paz.
Njia zake zinapendeza, mapito yake yote ni amani.
18 La sabiduría es un árbol de vida para todo el que se aferra a ella, y bendice a todos los que la aceptan.
Yeye ni mti wa uzima kwa wale wanaomkumbatia; wale wamshikao watabarikiwa.
19 Fue gracias a la sabiduría el Señor creó la tierra, y gracias al conocimiento puso los cielos en su lugar.
Kwa hekima Bwana aliiweka misingi ya dunia, kwa ufahamu aliziweka mbingu mahali pake;
20 Fue gracias a su conocimiento que las aguas de las profundidades fueron liberadas, y las nubes enviadas como rocío.
kwa maarifa yake vilindi viligawanywa, nayo mawingu yanadondosha umande.
21 Hijo mío, aférrate al buen juicio y a las decisiones sabias; no los pierdas de vista,
Mwanangu, hifadhi maamuzi mema na busara, usiache vitoke machoni pako;
22 porque serán vida para ti, y como un adorno en tu cuello.
ndipo vitakapokuwa uzima nafsini mwako na pambo la neema shingoni mwako.
23 Caminarás con confianza y no tropezarás.
Kisha utaenda katika njia yako salama, wala mguu wako hautajikwaa;
24 Cuando descanses, no tendrás temor, y cuando te acuestes tu sueño será placentero.
ulalapo, hautaogopa; ulalapo usingizi wako utakuwa mtamu.
25 No tendrás temor del pánico repentino, ni de los desastres que azotan al malvado,
Usiogope maafa ya ghafula au maangamizi yanayowapata waovu,
26 porque el Señor será tu confianza, y evitará que caigas en trampa alguna.
kwa kuwa Bwana atakuwa tumaini lako na kuepusha mguu wako kunaswa katika mtego.
27 No le niegues el bien a quien lo merece cuando tengas el poder en tus manos.
Usizuie wema kwa wale wanaostahili ikiwa katika uwezo wako kutenda.
28 No le digas a tu prójimo: “Vete. Ven mañana, y yo te daré”, si ya tienes los recursos para darle.
Usimwambie jirani yako, “Njoo baadaye, nitakupa kesho”: wakati wewe unacho kitu kile karibu nawe.
29 No hagas planes para perjudicar a tu prójimo que vive junto a ti, y que confía en ti.
Usifanye hila ya kumdhuru jirani yako, ambaye anaishi karibu na wewe akikuamini.
30 No discutas con nadie sin razón, si no han hecho nada para hacerte daño alguno.
Usimshtaki mtu bila sababu, wakati hajakutenda dhara lolote.
31 ¡No sientas celos de los violentos, ni sigas su ejemplo!
Usimwonee wivu mtu mwenye jeuri wala kuchagua njia yake iwayo yote,
32 Porque el Señor aborrece a los mentirosos, pero es amigo de los que hacen lo que es bueno.
kwa kuwa Bwana humchukia mtu mpotovu, lakini siri yake iko kwa mwenye haki.
33 Las casas de los malvados están malditas por el Señor, pero él bendice los hogares de los que viven en rectitud.
Laana ya Bwana i juu ya nyumba ya mwovu, lakini yeye huibariki nyumba ya mwenye haki.
34 Él se burla de los que se burlan, pero es bondadoso con los humildes.
Huwadhihaki wale wanaodhihaki, lakini huwapa neema wale wanyenyekevu.
35 Los sabios recibirán honra, pero los necios permanecerán en desgracia.
Wenye hekima hurithi heshima, bali huwaaibisha wapumbavu.

< Proverbios 3 >