< Proverbios 29 >
1 Cualquiera que siga rechazando obstinadamente muchas advertencias, sufrirá destrucción repentina, sin ningún remedio.
Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi, ataangamia ghafula, wala hapati dawa.
2 Cuando los justos están a cargo, todos celebran; pero cuando los malvados gobiernan, todos gimen.
Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi; waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.
3 El hombre que ama la sabiduría, hace feliz a su padre; pero el que visita a las prostitutas, está desperdiciando su dinero.
Mtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.
4 El rey que gobierna con justicia hace que el país esté seguro; pero el que pide sobornos, lo destruirá.
Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.
5 Los que adulan a sus amigos ponen una trampa para hacerlos caer.
Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili, anautandaza wavu kuitega miguu yake.
6 Los malvados están atrapados por sus propios pecados; pero los que hacen el bien, cantan y celebran.
Mtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.
7 Los justos se preocupan por trartar a los pobres con justiciar; pero los malvados no piensan en ello.
Mwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini, bali mwovu hajishughulishi na hilo.
8 Los cínicos pueden inflamar toda una ciudad, pero los sabios hacen calmar el furor.
Wenye mzaha huuchochea mji, bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.
9 Cuando un sabio lleva a un tonto a la corte, habrá rabia y ridículo pero sin soluciones.
Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu, mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani.
10 Los asesinos odian a las personas con integridad, pero los que viven rectamente tratarán de ayudarlos.
Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu na hutafuta kumuua mtu mnyofu.
11 Los tontos dejan salir toda su rabia, pero los sabios la contienen.
Mpumbavu huonyesha hasira yake yote, bali mwenye hekima hujizuia.
12 El gobernante que escucha la mentira no tendrá nada, sino solo oficiales malvados.
Kama mtawala akisikiliza uongo, maafisa wake wote huwa waovu.
13 Los pobres y sus opresores tienen algo en común: el Señor les da la vida.
Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili: Bwana hutia nuru macho yao wote wawili.
14 Si un rey juzga con justicia a los pobres, tendrá un largo reinado.
Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki, kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote.
15 La disciplina y la corrección proporcionan sabiduría; pero el hijo que no recibe disciplina es una vergüenza para su madre.
Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo humwaibisha mama yake.
16 Cuando los malvados están al poder, el pecado aumenta; pero los justos verán su caída.
Wakati waovu wanapostawi, pia dhambi vivyo hivyo, lakini wenye haki wataliona anguko lao.
17 Disciplina a tus hijos, y no te causarán preocupaciones. Te harán muy feliz.
Mrudi mwanao, naye atakupa amani, atakufurahisha nafsi yako.
18 Sin la revelación de Dios el pueblo se descontrola; pero los que guardan la ley son felices.
Mahali pasipo na ufunuo, watu kujizuia, bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
19 Un siervo no puede ser disciplinado solo con palabras; aunque entienden, no siguen la instrucción.
Mtumishi hawezi kuonywa kwa maneno matupu, ajapoelewa, hataitikia.
20 ¿Has visto a un hombre que habla sin pensar? ¡Hay más esperanza para un tonto que para él!
Je, unamwona mtu azungumzaye kwa haraka? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko yeye.
21 El siervo consentido desde la infancia será incontrolable.
Kama mtu akimdekeza mtumishi wake tangu ujanani, atamletea sikitiko mwishoni.
22 La gente enojada crea problemas, los irascibles cometerán muchos pecados.
Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi, naye mtu mwenye hasira ya haraka hutenda dhambi nyingi.
23 Si eres orgulloso serás humillado; pero si eres humilde, serás honrado.
Kiburi cha mtu humshusha, bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima.
24 El compañero de un ladrón aborrece su vida; incluso bajo amenaza y maldiciones, no podrá decir la verdad.
Anayekubaliana na mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe; huapishwa lakini hathubutu kushuhudia.
25 El temor a la gente es una trampa. Pero si confías en el Señor estarás a salvo.
Kuwaogopa watu huwa ni mtego, bali yeyote amtumainiaye Bwana atakuwa salama.
26 Muchos procuran el favor de un gobernante; pero la justicia viene del Señor.
Wengi hutafuta kusikilizwa na mtawala, bali mtu hupata haki kutoka kwa Bwana.
27 Los justos aborrecen a los injustos; los malvados aborrecen a los que hacen el bien.
Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu; waovu huwachukia sana wenye haki.