< Proverbios 26 >

1 Honrar a un tonto es tan inoportuno como la nieve en el verano, o la lluvia durante la cosecha.
Kama theluji wakati wa kiangazi au mvua wakati wa mavuno, ndivyo asivyostahili heshima mpumbavu.
2 La maldición no caerá sobre la persona que no la merece. Será como el ave o la golondrina que revolotean.
Kama shomoro apigapigavyo mabawa yake au mbayuwayu katika kuruka kwake kasi, ndivyo ilivyo laana isiyo na sababu haimpati mtu.
3 Los caballos necesitan un látigo, los asnos necesitan un freno. ¡Del mismo modo, los tontos necesitan vara en sus lomos!
Mjeledi kwa farasi, lijamu kwa punda, nayo fimbo kwa migongo ya wapumbavu!
4 No respondas al tonto según su estupidez, o terminarás igual que ellos.
Usimjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama wewe mwenyewe utakuwa kama yeye.
5 No respondas al tonto según su estupidez, o pensaran que son sabios.
Mjibu mpumbavu sawasawa na upumbavu wake, ama atakuwa mwenye hekima machoni pake mwenyewe.
6 Confiar la entrega de un mensaje en manos de un tonto, es como cortar tus pies o beber veneno.
Kama vile ilivyo kujikata miguu au kunywa hasara, ndivyo ilivyo kutuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu.
7 Un proverbio dicho por un tonto es tan inútil como las piernas de un inválido.
Kama miguu ya kiwete inavyoningʼinia ndivyo ilivyo mithali katika kinywa cha mpumbavu.
8 Honrar a un tonto es tan inútil como tratar de atar una piedra a una honda.
Kama kufunga jiwe kwenye kombeo, ndivyo ilivyo kumpa mpumbavu heshima.
9 Un proverbio dicho por un tonto es tan ridículo como ver a un borracho entre espinos.
Kama mwiba kwenye mkono wa mlevi ndivyo ilivyo mithali kinywani mwa mpumbavu.
10 Todo el que contrata a un tonto o a un desconocido errante, es como un arquero que hiere a la gente lanzando flechas al azar.
Kama mpiga upinde ambaye hujeruhi ovyo, ndivyo alivyo yeye aajiriye mpumbavu au yeyote apitaye njiani.
11 Los tontos repiten su estupidez, así como un perro vuelve a comer su vomito.
Kama mbwa ayarudiavyo matapiko yake, ndivyo mpumbavu arudiavyo upumbavu wake.
12 ¡Has visto a un hombre sabio en su propia opinión? ¡Hay más esperanza para un tonto que para él!
Je, unamwona mtu ajionaye mwenye hekima machoni pake mwenyewe? Liko tumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
13 Los perezosos son los que dicen: “¡Hay un león en el camino, un león por las calles!”
Mvivu husema, “Yuko simba barabarani, simba mkali anazunguka mitaa!”
14 El perezoso se voltea en la cama, como la puerta se recuesta en sus bisagras.
Kama vile mlango ugeukavyo kwenye bawaba zake, ndivyo mvivu ajigeuzavyo kitandani mwake.
15 Los perezosos extienden su mano hasta el plato, pero están demasiado cansados como para llevarse la comida a la boca.
Mtu mvivu hutumbukiza mkono wake kwenye sahani, naye huchoka kuupeleka kwenye kinywa chake.
16 Los perezosos son más sabios en su propia opinión que muchos consejeros prudentes.
Mtu mvivu ni mwenye hekima machoni pake mwenyewe, kuliko watu saba wawezao kujibu kwa busara.
17 Tomar parte en la disputa de otra persona es como agarrar a un perro callejero por las orejas.
Kama yeye amkamataye mbwa kwa masikio, ndivyo alivyo mtu apitaye njiani na kujiingiza kwenye ugomvi usiomhusu.
18 Serás como un loco lanzando flechas con fuego y matando gente
Kama mtu mwendawazimu atupaye vijinga vya moto au mishale ya kufisha,
19 si mientes a tu amigo, para luego decirle que era una broma.
ndivyo alivyo mtu amdanganyaye jirani yake na kusema, “Nilikuwa nikifanya mzaha tu!”
20 Sin madera, el fuego se apaga, y sin chismosos, se acaba la discordia.
Bila kuni moto huzimika; pasipo uchongezi ugomvi humalizika.
21 Una persona conflictiva aumenta la discordia, como poner carbón en brasas, o madera en el fuego.
Kama makaa juu ya makaa yanayowaka, na kama kuni kwenye moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuchochea ugomvi.
22 Escuchar chismes es como tragar bocados de tu comida preferida. Llegan hasta lo más profundo.
Maneno ya mchongezi ni kama chakula kitamu; huingia sehemu za ndani sana za mtu.
23 La persuación con intenciones malvadas es como un esmalte brillante de plomo en una olla de barro.
Kama rangi ingʼaayo iliyopakwa kwenye vyombo vya udongo ndivyo ilivyo midomo laini pamoja na moyo mbaya.
24 La gente te adulará aunque te odien. En el fondo te mienten.
Mtu mwenye nia ya kudhuru wengine hujificha kwa maneno ya midomo yake, lakini moyoni mwake huficha udanganyifu.
25 Cuando las personas sean buenas contigo, no les creas. Su mente está llena de odio hacia ti.
Ingawa maneno yake huvutia, usimwamini, kwa maana machukizo saba hujaza moyo wake.
26 Aunque su odio esté oculto detrás de su astucia, su maldad quedará expuesta delante de todos.
Nia yake ya kudhuru wengine inaweza kufichwa na udanganyifu, lakini uovu wake utafichuliwa kwenye kusanyiko.
27 Aquellos que cavan fosos para hacer caer a otros, terminarán cayendo ellos mismos. Y los que hacen rodar piedras, quedarán aplastados por ellas.
Kama mtu akichimba shimo, atatumbukia ndani yake, kama mtu akivingirisha jiwe, litamrudia.
28 Si mientes, muestras odio por las víctimas de tus mentiras. Si halagas a las personas, causarás desastre.
Ulimi wa uongo, huwachukia wale unaowaumiza, nacho kinywa cha kujipendekeza hutenda uharibifu.

< Proverbios 26 >