< Proverbios 25 >

1 Aquí hay más proverbios de Salomón, recopilados por los escribas de Ezequías, rey de Judá.
Hizi ni mithali zaidi za Solomoni, zilizonakiliwa na watu wa Hezekia mfalme wa Yuda:
2 La grandeza de Dios está en las cosas ocultas, mientras que la grandeza de los reyes está en revelar lo desconocido.
Ni Utukufu wa Mungu kuficha jambo, bali ni utukufu wa wafalme kuchunguza jambo.
3 Así como la altura de los cielos y la profundidad de la tierra, el pensamiento de un rey no se puede conocer.
Kama mbingu zilivyo juu na nchi ilivyo chini, ndivyo ambavyo mioyo ya wafalme haichunguziki.
4 Quita la escoria de la plata y el platero tendrá plata pura para hacer su trabajo.
Ondoa takataka kwenye madini ya fedha, nako ndani yake kutatokea chombo cha mfua fedha.
5 Quita al malvado de la presencia del rey, y el rey gobernará confiado y con justicia.
Ondoa waovu mbele ya mfalme, nacho kiti chake cha enzi kitaimarishwa kwa njia ya haki.
6 No trates de parecer grande delante del rey, y no finjas para estar entre la gente importante.
Usijikweze mwenyewe mbele ya mfalme, wala usidai nafasi miongoni mwa watu wakuu;
7 Porque es mejor que te digan: “Ven aquí arriba”, que ser humillado delante de un noble. Aunque hayas visto algo con tus propios ojos,
ni afadhali yeye akuambie, “Njoo huku juu,” kuliko yeye kukuaibisha mbele ya mkuu. Kile ulichokiona kwa macho yako
8 no corras a tomar acciones legales, porque ¿qué harás al final cuando tu vecino demuestre que estás equivocado y te humille?
usiharakishe kukipeleka mahakamani, maana utafanya nini mwishoni kama jirani yako atakuaibisha?
9 Debate el caso primero con tu vecino, y no traiciones el secreto que otra persona te ha confiado,
Kama ukifanya shauri na jirani yako, usisaliti siri ya mtu mwingine,
10 de lo contrario el que escuche te avergonzará y no podrás recuperarte de tu mala reputación.
ama yeye aisikiaye aweza kukuaibisha na kamwe sifa yako mbaya haitaondoka.
11 El consejo impartido en el momento correcto es como manzanas de oro con baño de plata.
Neno lisemwalo kwa wakati ufaao ni kama matunda ya mtofaa ya dhahabu yaliyowekwa kwenye vijalizo vya fedha.
12 La crítica constructiva de los sabios a quien escucha el consejo, es como un anillo de oro y un collar de oro fino.
Kama vile kipuli cha dhahabu au pambo la dhahabu safi, ndivyo lilivyo karipio la mtu mwenye hekima kwa sikio lisikilizalo.
13 El mensajero fiel es un fresco para su maestro, como la nieve fresca en un día caluroso de siega.
Kama vile ubaridi wa theluji wakati wa mavuno ndivyo alivyo mjumbe mwaminifu kwa wale wamtumao, huburudisha roho za bwana zake.
14 Quien se jacta de un regalo que nunca entrega, es como las nubes y el viento sin lluvia.
Kama vile mawingu na upepo pasipo mvua ndivyo alivyo mtu ajisifuye kwa zawadi ambazo hatoi.
15 Si eres paciente, podrás persuadir a tu superior, y las palabras suaves pueden derribar la oposición.
Kwa njia ya uvumilivu mtawala aweza kushawishiwa, nao ulimi laini waweza kuvunja mfupa.
16 Si hallas dinero, come lo necesario; porque si comes demasiado, te enfermarás.
Ukipata asali, kula kiasi tu cha kukutosha, ukila zaidi, utatapika.
17 No visites la casa de tu vecino con mucha frecuencia, o se cansarán y te aborrecerán.
Ingiza mguu wako nyumbani kwa jirani yako mara chache, ukizidisha, atakukinai na atakuchukia.
18 Mentir en la corte contra un amigo es como atacarlo con una maza, con una espada o con una lanza.
Kama vile rungu au upanga au mshale mkali ndivyo alivyo mtu atoaye ushuhuda wa uongo dhidi ya jirani yake.
19 Confiar en las personas poco fiables en momentos de dificultad es como comer con un diente partido, o caminar con un pie herido.
Kama vile jino bovu au mguu uliolemaa, ndivyo ilivyo kumtegemea mtu asiye mwaminifu wakati wa shida.
20 Cantar canciones alegres a quien tiene el corazón quebrantado, es como quitarte el abrigo en un día de frio, o poner vinagre en una herida abierta.
Kama vile avuaye mavazi siku ya baridi, au kama siki iliyomwagwa juu ya magadi, ndivyo alivyo yeye amuimbiaye nyimbo mtu mwenye moyo mzito.
21 Si tu enemigo tiene hambre, dale de comer; si tiene sed, dale de beber.
Kama adui yako ana njaa, mpe chakula ale; kama ana kiu, mpe maji anywe.
22 Esto hará que se avergüence como si tuviera carbones encendidos sobre su cabeza, y el Señor te recompensara.
Kwa kufanya hivyo, unaweka makaa ya moto yanayowaka kichwani pake, naye Bwana atakupa thawabu.
23 Así como el viento del norte trae la lluvia, las personas calumniadoras hacen enojar.
Kama vile upepo wa kaskazini uletavyo mvua, ndivyo ulimi usingiziao uletavyo uso wa hasira.
24 Mejor es vivir en un rincón de la azotea, que compartir toda la casa con una mujer conflictiva.
Ni afadhali kuishi pembeni mwa paa la nyumba, kuliko kuishi nyumba moja na mke mgomvi.
25 Las buenas noticias que vienen de un país lejano son como agua fresca para un viajero cansado.
Kama vile maji baridi kwa nafsi iliyochoka ndivyo zilivyo habari njema kutoka nchi ya mbali.
26 Los justos que ceden ante los malvados son como una fuente llena de barro, o un pozo contaminado.
Kama vile chemchemi iliyotibuliwa matope au kisima kilichotiwa taka ndivyo alivyo mtu mwenye haki akishiriki na waovu.
27 No es bueno comer mucha miel, tampoco desear mucha alabanza.
Si vyema kula asali nyingi sana, wala si heshima kujitafutia heshima yako mwenyewe.
28 Una persona sin dominio propio es como una ciudad expuesta, cuyos muros están agrietados.
Kama vile mji ambao kuta zake zimebomoka ndivyo alivyo mtu ambaye hawezi kujitawala mwenyewe.

< Proverbios 25 >