< Proverbios 24 >

1 No tengas envidia de los malvados, ni desees su compañía,
Usiwaonee wivu watu waovu, usitamani ushirika nao;
2 porque ellos conspiran planes crueles y discuten entre ellos para causar tribulación.
kwa maana mioyo yao hupanga mambo ya jeuri, nayo midomo yao husema juu ya kuleta madhara.
3 Una casa se construye con sabiduría. Su fundamento seguro es la inteligencia.
Kwa hekima nyumba hujengwa, nayo kwa njia ya ufahamu huimarishwa
4 Sus habitaciones están llenas de conocimiento, con todo tipo de hermosos y valiosos objetos.
kwa njia ya maarifa vyumba vyake hujazwa vitu vya thamani na vya kupendeza.
5 Si tienes sabiduría, serás fuerte. Si tienes inteligencia, tu poder aumentará.
Mtu mwenye hekima ana uwezo mkubwa, naye mtu mwenye maarifa huongeza nguvu,
6 Porque con la guía correcta, podrás ir a la guerra, y serás victorioso si tienes muchos buenos consejeros.
kwa kufanya vita unahitaji uongozi na kwa ushindi washauri wengi.
7 La sabiduría examina las mentes de los tontos. Ellos no tienen nada que aportar en las discusiones sobre los asuntos importantes.
Hekima i juu mno kwa mpumbavu, katika kusanyiko langoni hana lolote la kusema.
8 Todo aquel que hace planes para hacer el mal, será considerado un problemático.
Yeye apangaye mabaya atajulikana kama mtu wa hila.
9 Los planes que hacen los tontos son de pecado. Todos aborrecen a los que se burlan de otros.
Mipango ya upumbavu ni dhambi, watu huchukizwa na mwenye dhihaka.
10 Si te rindes en el momento de la prueba, mostraras cuan débil eres.
Ukikata tamaa wakati wa taabu, jinsi gani nguvu zako ni kidogo!
11 Rescata a los que son expulsados para ser ejecutados. Salva a los que desfallecen de camino a su muerte.
Okoa wale wanaoongozwa kwenye kifo; wazuie wote wanaojikokota kuelekea machinjoni.
12 Si dices: “No sabíamos nada sobre esto”, ¿no crees que el Dios que juzga las motivaciones no se dará cuenta de lo que ocurre realmente? El que te mira desde arriba lo sabe todo, y le pagará a todos según sus actos.
Kama mkisema, “Lakini hatukujua lolote kuhusu hili,” je, yule apimaye mioyo halitambui hili? Je, yule awalindaye maisha yenu halijui hili? Je, hatamlipa kila mtu kulingana na aliyotenda?
13 Hijo mío, comer miel te conviene; el panal de miel tiene un dulce sabor.
Ule asali mwanangu, kwa kuwa ni nzuri; asali kutoka kwenye sega ni tamu kwa kuonja.
14 Del mismo modo, debes saber que te conviene la sabiduría; y que sin la encuentras habrá un futuro para ti que no será frustrado.
Ujue pia kwamba hekima ni tamu kwa nafsi yako, kama ukiipata, kuna matumaini kwako ya siku zijazo, nalo tumaini lako halitakatiliwa mbali.
15 No seas como el criminal que espera para entrar por sorpresa en las casas de las buenas personas. No ataques el lugar donde viven.
Usivizie kama haramia afanyavyo ili kuyashambulia makao ya mwenye haki, wala usiyavamie makazi yake,
16 Los que hacen el bien podrán caer siete veces, y aun así se levantaran; pero el desastre vendrá para derribar a los malvados.
Kwa maana ingawa mtu mwenye haki huanguka mara saba, huinuka tena, lakini waovu huangushwa chini na maafa.
17 No celebres cuando tu enemigo caiga. No te alegues cuando se tropiece,
Usitazame kwa kufurahia adui yako aangukapo; wakati ajikwaapo, usiruhusu moyo wako ushangilie.
18 porque puede que cuando el Señor lo note, se desagrade de ti y no lo castigue como lo había pensado.
Bwana asije akaona na kuchukia akaiondoa ghadhabu yake mbali naye.
19 No te enojes por causa de los malvados, ni sientas celos por los que hacen el mal,
Usikasirike kwa sababu ya watu wabaya wala usiwaonee wivu waovu,
20 porque los malvados no tienen futuro. La lámpara de los malvados se apagará.
kwa maana mtu mbaya hana tumaini la siku zijazo, nayo taa ya waovu itazimwa.
21 Hijo mío, honra al Señor y al rey, y no te juntes con los rebeldes,
Mwanangu, mche Bwana na mfalme, wala usijiunge na waasi,
22 porque el desastre vendrá sobre ellos repentinamente. ¿Quién podrá saber cómo los castigarán el Señor y el rey?
kwa maana hao wawili watatuma maangamizi ya ghafula juu yao, naye ni nani ajuaye maafa wawezayo kuleta?
23 Estos son más dichos del sabio: Mostrar preferencias cuando emites un juicio no es bueno.
Hii pia ni misemo ya wenye hekima: Kuonyesha upendeleo katika hukumu si vyema:
24 Los que le dicen al culpable: “Eres inocente”, serán malditos por el pueblo y odiados por la nación,
Yeyote amwambiaye mwenye hatia, “Wewe huna hatia,” Kabila zitamlaani na mataifa yatamkana.
25 pero los que condenan al culpable serán estimados, y recibirán rica bendición.
Bali itakuwa vyema kwa wale watakaowatia hatiani wenye hatia, nazo baraka tele zitawajilia juu yao.
26 Una respuesta honesta es como un beso en los labios.
Jawabu la uaminifu ni kama busu la midomoni.
27 Haz primero el trabajo que necesitas hacer afuera y prepárate para sembrar tus campos. Solo después de eso, comienza a construir tu casa.
Maliza kazi zako za nje, nawe uweke mashamba yako tayari, baada ya hayo, jenga nyumba yako.
28 No seas testigo contra tu prójimo sin tener una buena razón, ni digas mentiras.
Usishuhudie dhidi ya jirani yako bila sababu, au kutumia midomo yako kudanganya.
29 No digas en tu pensamiento: “Voy a hacerle lo mismo que me hizo! ¡Haré que me pague por lo que ha hecho!”
Usiseme, “Nitamtenda kama alivyonitenda mimi; nitamlipiza mtu yule kwa kile alichonitendea.”
30 Mientras caminaba, pasé por el campo del hombre perezoso, y por el viñedo de un insensato.
Nilipita karibu na shamba la mvivu, karibu na shamba la mizabibu la mtu asiye na akili,
31 Y estaba lleno de monte y espinas, el suelo estaba cubierto de hierba y la piedra angular se había caído.
miiba ilikuwa imeota kila mahali, ardhi ilikuwa imefunikwa na magugu, na ukuta wa mawe ulikuwa umebomoka.
32 Y mientras veía, pensé y aprendí una lección:
Nikatafakari moyoni mwangu lile nililoliona, nami nikajifunza somo kutokana na niliyoyaona:
33 Puedes decir: “Solo dormiré un poco más, me recostaré apenas un rato, y cruzaré mis brazos para descansar un poco más”,
Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
34 pero la pobreza te atacará como un ladrón, y la miseria como un guerrero armado.
hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.

< Proverbios 24 >