< Proverbios 17 >

1 Mejor es comer un trozo seco de comida en paz, que un banquete en una casa llena de conflictos.
Afadhali kula ukoko mkavu ukiwa na amani na utulivu kuliko kukaa kwenye nyumba ya karamu kukiwa na magomvi.
2 Un siervo que actúa con sabiduría se hará cargo del hijo que ha caído en desgracia, y compartirá la herencia de la familia con los hermanos.
Mtumishi mwenye hekima atatawala juu ya mwana aaibishaye, naye atashirikiana katika urithi kama mmoja wa hao ndugu.
3 El crisol sirve para probar la plata, y un horno para probar el oro; pero el Señor prueba las mentes.
Kalibu ni kwa ajili ya fedha na tanuru ni kwa ajili ya dhahabu, bali Bwana huujaribu moyo.
4 Las personas malvadas escuchan las palabras dañinas; y los mentirosos escuchan las palabras de maldad.
Mtu mwovu husikiliza midomo mibaya; mwongo husikiliza kwa makini ulimi wa madhara.
5 Todo aquél que oprime al pobre, insulta a su Hacedor; y el que disfruta viendo el sufrimiento de otros será castigado.
Yeye anaye mdhihaki maskini huonyesha dharau kwa Muumba wake; yeyote afurahiaye maafa hataepuka kuadhibiwa.
6 Los ancianos se alegran de sus nietos, y los hijos sienten orgullo de sus padres.
Wana wa wana ni taji la wazee, nao wazazi ni fahari ya watoto wao.
7 Las palabras sofisticadas no lucen en la boca de los tontos; mucho menos las mentiras deben estar en labios de un gobernante.
Midomo yenye uwezo wa ushawishi haimfai mpumbavu: je, ni mibaya kiasi gani zaidi midomo ya uongo kwa mtawala!
8 Los que practican el soborno creen que tienen una piedra mágica, y creen que tendrán éxito dondequiera que vayan.
Kipawa ni kama kito cha thamani machoni pake yeye aliye nacho; kokote kigeukiapo, hufanikiwa.
9 Si perdonas un mal, cosecharás una amistad; pero si sigues hablando de la ofensa, perderás a tu amigo.
Yeye anayesamehe kosa hudumisha upendo, bali yeyote arudiaye jambo hutenganisha marafiki wa karibu.
10 Duele más un solo reproche al que es inteligente, que cien golpes a un tonto.
Karipio humwingia sana mtu mwenye kutambua kuliko mapigo mia kwa mpumbavu.
11 Los malvados solo piensan en rebelarse, por eso un mensajero cruel será enviado para atacarlos.
Mtu mbaya hupenda kuasi tu; mjumbe asiye na huruma atatumwa dhidi yake.
12 Mejor es encontrarte con una madre oso a quien le han robado sus hijos, que con una persona estúpida.
Ni afadhali ukutane na dubu aliyenyangʼanywa watoto wake, kuliko mpumbavu katika upumbavu wake.
13 Si pagas con mal el bien, el mal nunca saldrá de tu casa.
Ikiwa mtu atalipa baya kwa jema, kamwe ubaya hautaondoka katika nyumba yake.
14 El comienzo de una discordia es como la primera grieta en una presa de agua, así que abandónala antes de que la discusión estalle.
Kuanzisha ugomvi ni kama kutoboa bwawa la maji; kwa hiyo acha jambo hilo kabla mabishano hayajaanza.
15 El Señor odia cuando los malvados son absueltos y los inocentes son condenados.
Yeye asemaye kuwa asiye na haki ana haki, naye asemaye kuwa mwenye haki hana haki: Bwana huwachukia sana wote wawili.
16 ¿Tiene sentido que los tontos traten de comprar sabiduría cuando ni siquiera quieren aprender?
Fedha ina faida gani mikononi mwa mpumbavu, wakati yeye hana haja ya kupata hekima?
17 Un verdadero amigo estará siempre allí para amarte, y la familia te ayudará en momentos de tribulación.
Rafiki hupenda wakati wote naye ndugu amezaliwa kwa ajili ya wakati wa shida.
18 No es sabio comprometerse y ser fiador de la deuda del prójimo.
Mtu mjinga hupana mkono ili kuweka rehani, naye huweka dhamana kwa jirani yake.
19 A los que aman el pecado les gusta el pleito. Los que construyen muros altos invitan a la destrucción.
Yeye apendaye ugomvi apenda dhambi; naye ainuaye sana lango lake hutafuta uharibifu.
20 Las personas con mentes perversas no tendrán éxito; Los mentirosos se meterán en problemas.
Mtu mwenye moyo mpotovu hawezi kufanikiwa; naye ambaye ulimi wake ni mdanganyifu huanguka kwenye taabu.
21 Un hijo tonto acarrea tristeza para tu padre; el padre de un hijo que actúa con necedad no vivirá con alegría.
Kuwa na mwana mpumbavu huleta huzuni; hakuna furaha kwa baba wa mpumbavu.
22 Un corazón alegre es buena medicina; pero el desánimo te enfermará.
Moyo wenye furaha ni dawa nzuri, bali roho iliyopondeka hukausha mifupa.
23 Los malvados toman botines ocultos para tergiversar el curso de la justicia.
Mtu mwovu hukubali rushwa kwa siri ili kupotosha njia ya haki.
24 Los prudentes están atentos a la sabiduría, pero los ojos de los tontos siempre están divagando.
Mtu wa ufahamu huitazama hekima, lakini macho ya mpumbavu huhangaika hadi kwenye miisho ya dunia.
25 Un hijo tonto acarrea vergüenza a su padre, y tristeza a la madre que lo parió.
Mwana mpumbavu huleta huzuni kwa baba yake na uchungu kwa yeye aliyemzaa.
26 No es correcto imponer una multa a una persona inocente ni flagelar a los líderes buenos por su honestidad.
Si vizuri kumwadhibu mtu asiye na hatia, au kuwapiga sana maafisa kwa ajili ya uadilifu wao.
27 Si eres sabio, cuidarás tus palabras; y si eres prudente, cuidarás tu temperamento.
Mtu mwenye maarifa hutumia maneno kwa kujizuia, naye mtu mwenye ufahamu ana moyo wa utulivu.
28 Hasta los tontos son considerados sabios cuando callan; y al no decir nada, aparentan inteligencia.
Hata mtu mpumbavu hudhaniwa kuwa na hekima kama akinyamaza, na mwenye ufahamu kama akiuzuia ulimi wake.

< Proverbios 17 >