< Proverbios 16 >

1 Los seres humanos hacen planes en sus mentes, pero la decisión final le pertenece al Señor.
Mipango ya moyo ni ya mtu, bali Yehova hutoa jawabu kutoka kwenye ulimi wake.
2 Las personas creen que todo lo que hacen está bien, pero el Señor mira sus intenciones.
Njia zote za mtu ni safi kwenye macho yake mwenyewe, bali Yehova huipima mioyo.
3 Encomienda todas tus obras al Señor, y tus planes serán exitosos.
Kabidhi kwa Yehova kazi zako zote na mipango yako itafanikiwa.
4 El Señor tiene un propósito con todo lo que hace, incluso al malvado para el día de tribulación.
Yehova alifanya kila kitu kwa kusudi lake, hata waovu kwa ajili ya siku ya taabu.
5 El Señor aborrece al arrogante. De algo puedes estar seguro: los malvados no se quedarán sin castigo.
Yehova anamchukia kila mtu mwenye moyo wa majivuno, ingawa wanasimama imara, hawakosi kupata adhabu.
6 Hay perdón de pecados por medio del amor fiel y la lealtad; honrando al Señor serás librado del mal.
Kwa agano la uaminifu na udhamini uovu husafishwa na kwa kumcha Yehova watu hujitenga na ubaya.
7 Cuando el camino del ser humano agrada al Señor, hasta a sus enemigos hace estar en paz con él.
Njia za mtu zinapompendeza Yehova, huwafanya hata adui zake huyo mtu wawe na amani naye.
8 Mejor es tener poco y ser honesto, que tener mucho practicando la deshonestidad.
Bora kitu kidogo pamoja na haki, kuliko mapato makubwa pamoja na udhalimu.
9 Puedes hacer planes en tu mente sobre qué hacer, pero el Señor será tu guía.
Katika moyo wake mtu hunuia njia yake, bali Yehova huziongoza hatua zake.
10 El rey se inspira antes de hablar, y sus decisiones son fieles.
Mshauri yupo katika midimo ya mfalme, katika hukumu kinywa chake hakisemi kwa udanganyifu.
11 Para el Señor es importante que el peso y la balanza muestren el peso correcto. Él mismo ha determinado todos los pesos en la bolsa.
Vipimo vya kweli hutoka kwa Yehova; uzito wote kwenye gunia ni kazi yake.
12 Que el rey actúe con maldad es terrible, pues su trono le ha sido dado por hacer lo recto.
Wafalme wanapofanya mambo maovu, hicho ni kitu cha kudharauliwa, kwa maana utawala huimarishwa kwa kutenda haki.
13 Aquellos que hablan con la verdad agradan a los reyes. Ellos aman a quienes hablan con rectitud.
Mfalme hufurahia midomo ambayo husema haki na anampenda mwenye kusema waziwazi.
14 Un rey enojado puede enviarte a la muerte. Si eres sabio, procurarás apaciguar su ira.
Hasira ya mfalme ni mjumbe wa mauti lakini mtu mwenye busara atajaribu kutuliza hasira yake.
15 Si el rey sonríe, vivirás. Su bendición es como las nubes que traen lluvia en primavera.
Katika nuru ya uso wa mfalme ni uzima na fadhila yake ni kama wingu linaloleta mvua ya masika.
16 Más valioso es obtener sabiduría que oro. Mejor elige el conocimiento antes que la plata.
Ni bora kiasi gani kupata hekima kuliko dhahabu. Kuchagua kupata ufahamu ni zaidi kuliko fedha.
17 El camino de los rectos te llevará lejos del mal. Si estás atento a dónde vas, salvarás tu vida.
Njia kuu ya watu waadilifu hujitenga na ubaya; mwenye kuyahifadhi maisha yake huilinda njia yake.
18 El orgullo lleva a la destrucción. Y un espíritu arrogante conduce a la caída.
Kiburi hutangulia kabla ya uharibifu na moyo wa kujivuna kabla ya maangamizi.
19 Mejor es tener un espíritu humilde y convivir con los pobres, que compartir el botín con los soberbios.
Ni bora kunyenyekea miongoni mwa watu masikini kuliko kugawana ngawira pamoja watu wenye kiburi.
20 Si estás atento a la instrucción sabia te irá bien; vivirás feliz si confías en el Señor.
Mwenye kutafakari yaliyofundishwa hupata kilicho chema na wenye kumtumaini Yehova watafurahi.
21 Si piensas con sabiduría serás considerado como prudente; si hablas con gracia serás persuasivo.
Mwenye hekima moyoni anaitwa ufuhamu na utamu wa hotuba huongeza uwezo wa kufundisha.
22 Si tienes inteligencia, será como una Fuente de vida para ti; pero los tontos son castigados por su estupidez.
Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwake ambaye nayo, bali adhabu ya wapumbavu ni upumbavu wao.
23 Una mente sabia se asegura de hablar con prudencia; las palabras dichas son persuasivas.
Moyo wa mtu mwenye hekima hutoa busara katika kinywa chake na huongeza ushawishi katika midomo yake.
24 Las palabras bondadosas son como un panal de miel, su sabor es dulce y aportan salud al cuerpo.
Maneno yenye kufaa ni sega la asali -matamu kwenye nafsi na huponya mifupa.
25 Hay camino que parece ser bueno, pero al final es camino de muerte.
Kuna njia ambayo huonekana sawa kwa mtu, bali mwisho wake ni njia ya mauti.
26 Un buen apetito ayuda al trabajador. El hambre los impulsa a trabajar.
Hamu ya kibarua humfanyia kazi; njaa yake humsihi kuendelea.
27 Las personas vacías conspiran para hacer el mal y sus palabras arden como fuego.
Mtu duni huchimba madhara na usemi wake ni kama moto unaounguza.
28 Las personas rencillosas causan conflictos, y el chisme nace entre los amigos más cercanos.
Mtu mkaidi huchochea mafarakano na umbeya huwafarakanisha marafiki.
29 Las personas malvadas adulan a sus amigos, y los conducen por el camino que no les conviene.
Mtu wa vurugu humdanganya jirani yake na kumwongoza kwenye mapito ambayo si mema.
30 Las personas que guiñan su ojo están conspirando el mal; aprietan sus labios y provocan el mal.
Yule anayekonyeza kwa jicho anapanga njama za mambo ya ukaidi; wenye kuandama midomo yao watapitisha mabaya.
31 El cabello con canas es como una corona de gloria; solo se obtiene al vivir en rectitud.
Mvi ni taji ya utukufu; hupatikana kwa kuishi katika njia ya haki.
32 Mejor es ser lento para enojarse, que ser poderoso; mejor es tener dominio propio que conquistar una ciudad.
Ni bora kukawia kuwa na hasira kuliko kuwa shujaa na mwenye kutawala roho yake ni imara zaidi kuliko yule anayeuteka mji.
33 Lanzan la suerte sobre el regazo, pero el Señor es quien toma las decisiones.
Kura hurushwa kwenye mkunjo, bali maamuzi hutoka kwa Yehova.

< Proverbios 16 >