< Proverbios 13 >
1 Un hijo sabio acepta la disciplina de su padre, pero el burlador no escuchará la corrección.
Mwana mwenye hekima husikia mafundisho ya baba yake, bali mwenye dhihaka hatasikiliza karipio.
2 Recibirás recompensa por usar las palabras correctas; pero las personas deshonestas procuran la violencia.
Mtu hufurahia vitu vizuri kutokana na matunda ya kinywa chake, bali hamu ya wadanganyifu ni jeuri.
3 Cuida lo que dices y salvaras tu vida; decir mucho conlleva al desastre.
Yeye anayelinda kinywa chake huyalinda maisha, bali anayefumbua sana midomo yake atajiangamiza mwenyewe.
4 Los perezosos desean muchas cosas pero no reciben nada; pero si trabajas duro serás recompensado.
Hamu ya watu wavivu ni uchu lakini hawapati kitu, bali hamu ya watu wenye bidii hutoshelezwa sana.
5 Las personas de bien odian las mentiras; pero los malvados hieden y solo aportan desgracia.
Atendaye haki huchukia uongo, bali mtu mwovu hukinzana mwenyewe, na kufanya ya kuaibisha.
6 La bondad protege a los que viven en rectitud; pero el pecado destruirá a los malvados.
Wenye haki huwalinda wale ambao ni wakamilifu katika mapito yao, bali uovu huwaangusha wale watendao dhambi.
7 Algunos aparentan ser ricos, pero n tienen nada; mientras que otros aparentan ser pobres pero son muy ricos.
Kuna mtu ambaye hujitajirisha mwenyewe, lakini hana chochote na kuna mtu ambaye hutoa kila kitu, bado ni tajiri kweli.
8 Los ricos pueden pagar recompensa para salvar sus vidas, pero los pobres ni siquiera experimentan tal tribulación.
Mtu tajiri anaweza kufidia maisha yake kwa mali zake, bali mtu masikini hatapokea kitisho cha aina hiyo.
9 La vida de las personas buenas alumbra con esplendor, pero la lampara de los malvados será apagada.
Mwanga wa mtu atendaye haki hufurahia, bali taa ya waovu itazimika.
10 El orgullo solo causa conflicto; pero los sabios aceptan el consejo.
Kiburi huzaa mafarakano, bali kwa wale wasikiao shauri jema kuna hekima.
11 La riqueza que se logra con fraude desaparece rápidamente; pero los que la logran poco a poco prosperarán.
Penye majivuno mengi utajiri hufifia, bali yeye apataye pesa kwa kufanya kazi kwa mkono wake pesa zake zitaongezeka.
12 La esperanza que se tarda puede causar malestar, pero un deseo cumplido puede darte vida nuevamente.
Tumaini linapoachwa, huvunja moyo, bali kukamilishwa kwa shauku ni mti wa uzima.
13 Si rechazas las palabras de consejo, pagaras por ello; pero si respetas el consejo que te dan, serás recompensado.
Yule ambaye anadharau fundisho bado atakuwa chini ya utawala wake, bali yeye ambaye anaheshimu amri atapewa thawabu.
14 La enseñanza del sabio es como una fuente de vida, gracias a la cual puedes evadir las trampas de la muerte.
Mafundisho ya mtu mwenye hekima ni chemchemi ya uzima, yanakuondoa kutoka kwenye mitego ya mauti.
15 La inteligencia produce gran estima, pero el camino de los infieles es duro.
Busara njema huleta fadhila, bali njia ya wadanganyifu haina mwisho.
16 Todas las personas sabias actúan con inteligencia; pero los tontos demuestran su estupidez.
Watu wenye busara hutenda kwa maarifa kwa kila uamuzi, bali mpumbavu huonyesha upuuzi wake.
17 Un mal mensajero crea problemas; pero un embajador fiel trae sanidad.
Mjumbe mbaya huangukia kwenye shida, bali balozi mwaminifu huleta upatanisho.
18 La pobreza y la desgracia can sobre aquellos que carecen de instrucción; pero los que aceptan la corrección serán honrados.
Yeye ambaye hupuuza kurudiwa atapata umasikini na aibu, bali heshima itamjia yeye ambaye hujifunza kutokana na masahihisho.
19 Es bueno ver un deseo cumplido; pero los necios odian tener que alejarse del mal para lograr su deseo.
Shauku iliyotambuliwa ni tamu kwa hamu, bali wapumbavu huchukia kuacha uovu.
20 Ser amigo de sabios te hará sabio; pero ser amigo de tontos te traerá problemas.
Tembea pamoja na watu wenye hekima nawe utakuwa na hekima, bali rafiki wa wapumbavu atateseka.
21 La tragedia persigue al pecador; pero la prosperidad recompensa al justo.
Maafa huwakimbilia wenye dhambi, bali wale watendao haki hupewa thawabu kwa mema.
22 Los justos dejan herencia para sus nietos, pero la riqueza del pecador está reservada para los que viven en justicia.
Mtu mwema huacha urithi kwa wajukuu wake, bali mali ya mwenye dhambi huwekwa akiba kwa yule atendaye haki.
23 La tierra sin arar de los pobres puede producir mucho alimento, pero es robado por causa de la injusticia.
Shamba la masikini lisilolimwa linaweza huzalisha chakula kingi, bali huchukuliwa kwa udhalimu.
24 Los que no disciplinan a sus hijos, los odian. Los que aman a sus hijos los disciplinan con cuidado.
Yeye ambaye hamrudi mwanawe humchukia, bali yule anayempenda mwanawe humjali kwa kumwadibisha.
25 Los justos comen hasta saciarse; pero el estómago de los malvados esta vacío.
Yeye atendaye haki hula hadi kutosheleza hamu yake bali tumbo la mwovu linanjaa daima.