< Proverbios 12 >
1 Si amas el conocimiento, amarás la disciplina. ¡Todo el que aborrece la corrección es un necio!
Yeyote apendaye kuadibishwa hupenda maarifa, bali yeye achukiaye kuonywa ni mpumbavu.
2 El Señor bendice a los que hacen el bien, pero condena a los que conspiran para hacer el mal.
Mtu mwema hupata kibali kutoka kwa Bwana, bali Bwana humhukumu mwenye hila.
3 La maldad no brinda seguridad, pero los que viven en justicia tienen sus raíces profundas y no serán removidos.
Mtu hathibitiki kutokana na uovu, bali mwenye haki hataondolewa.
4 Una buena esposa es corona para su esposo, pero la mujer que trae vergüenza es como descomposición en sus huesos.
Mke mwenye tabia nzuri ni taji ya mumewe, bali aaibishaye ni kama uozo katika mifupa ya mumewe.
5 Las personas que hacen el bien, hacen planes justos, pero el consejo de los malvados es engañoso.
Mipango ya mtu mwadilifu ni ya haki, bali ushauri wa mwovu ni udanganyifu.
6 Las palabras de los malvados son como una emboscada con violencia, pero las palabras de las personas honestas los salvarán.
Maneno ya waovu huotea kumwaga damu, bali maneno ya waadilifu huwaokoa.
7 Los malvados son destriudos y olvidados. Pero la familia de los que hacen el bien permanece firme.
Watu waovu huondolewa na kutoweka, bali nyumba ya mwenye haki husimama imara.
8 Las personas son estimadas cuando hablan con sensatez, pero los que tienen mentes perversas son aborrecidos.
Mtu husifiwa kulingana na hekima yake, bali watu wenye akili zilizopotoka hudharauliwa.
9 Mejor es ser humilde y trabajar para ti mismo, que ser un hombre jactancioso y no tener nada para comer.
Heri mtu wa hali ya chini mwenye mtumishi, kuliko kujifanya mtu wa hali ya juu nawe huna chakula.
10 Los justos cuidan de sus animales, pero el cuidado de los malvados es crueldad.
Mtu mwenye haki hujali mahitaji ya mnyama wake, bali matendo ya huruma ya mwovu ni ukatili.
11 Si cultivas la tierra, tendrás abundancia de dinero, pero si vas detrás de cosas inútiles, eres un tonto.
Yeye alimaye shamba lake atakuwa na chakula tele, bali yeye afuataye mambo ya upuzi hana akili.
12 Las personas malvadas buscan el grano robado, pero las personas justas lo producen ellas mismas.
Waovu hutamani mateka ya watu wabaya, bali shina la mwenye haki hustawi.
13 Los malvados quedan atrapados por sus propias palabras pecaminosas, pero las personas que hacen el bien se libran de los problemas.
Mtu mwovu hunaswa kwa mazungumzo yake ya dhambi, bali mwenye haki huepuka taabu.
14 Tus palabras te traerán recompensa, y tu trabajo regresará a bendecirte.
Kutokana na tunda la midomo yake mtu hujazwa na mambo mema, hakika kama ilivyo kazi ya mikono yake humtunza.
15 Los necios creen que van por el camino correcto, pero si eres sabio escucharás el consejo.
Njia ya mpumbavu huonekana sawa machoni pake mwenyewe, bali mtu mwenye hekima husikiliza ushauri.
16 Los necios se enojan con facilidad; pero si eres prudente, ignorarás los insultos.
Mpumbavu huonyesha kuudhika kwake mara moja, bali mtu wa busara hupuuza matukano.
17 Quien dice la verdad es honesto, pero un testigo falso dirá mentiras.
Shahidi wa kweli hutoa ushuhuda wa kuaminika, bali shahidi wa uongo husema uongo.
18 Las palabras apresuradas pueden ser tan cortantes como un cuchillo, pero las palabras de los sabios traen sanidad.
Maneno ya kipumbavu huchoma kama upanga, bali ulimi wa mwenye hekima huleta uponyaji.
19 Las palabras de verdad duran para siempre, pero las mentiras se olvidan pronto.
Midomo isemayo kweli hudumu milele, bali ulimi wa uongo hudumu kwa muda mfupi tu.
20 En la mente de los que maquinan maldad solo hay engaño; pero los que piensan en hacer el bien viven con alegría.
Upo udanganyifu katika mioyo ya wale ambao hupanga mabaya, bali kuna furaha kwa wale wanaoleta amani.
21 A los que hacen el bien no les pasara ningún mal, pero los malvados están llenos de problemas.
Hakuna dhara linalompata mwenye haki, bali waovu wana taabu nyingi.
22 El Señor aborrece a los mentirosos, pero se alegra con los fieles.
Bwana anachukia sana midomo idanganyayo, bali hufurahia watu ambao ni wa kweli.
23 Si eres prudente, no presumes de tu conocimiento; pero los tontos anuncian su estupidez.
Mtu mwenye busara hujihifadhia maarifa yeye mwenyewe, bali moyo wa wapumbavu hububujika upumbavu.
24 El trabajo duro aporta liderazgo, pero la pereza trae esclavitud.
Mikono yenye bidii itatawala, bali uvivu huishia katika kazi za utumwa.
25 Si vives con ansiedad, te sentirás sobrecargado; pero una palabra de aliento te reconfortará.
Moyo wa wasiwasi humlemea mtu, bali neno la huruma humfurahisha.
26 Las personas que hacen el bien cuidan de sus amigos, pero la forma en que viven los malvados lleva a sus amigos a la perdición.
Mtu mwenye haki ni mwangalifu katika urafiki, bali njia ya waovu huwapotosha.
27 Los perezosos no atrapan su presa, pero si trabajas duro te volverás rico.
Mtu mvivu haoki mawindo yake, bali mtu mwenye bidii ana mali za thamani.
28 El camino de los justos lleva a la vida, nunca te conducirá a la muerte.
Katika njia ya haki kuna uzima; katika mapito hayo kuna maisha ya milele.