< Proverbios 11 >

1 El Señor odia los pesos falsos, pero el peso acertado le complace.
Bwana huchukia sana mizani za udanganyifu, bali vipimo sahihi ni furaha yake.
2 El orgullo trae desgracia, pero la humildad trae sabiduría.
Kiburi kinapokuja, ndipo huja aibu, bali unyenyekevu huja na hekima.
3 La honestidad es la guía de los que hacen el bien, pero el engaño destruye a los mentirosos.
Uadilifu wa wenye haki huwaongoza, bali wasio waaminifu huharibiwa na hila yao.
4 La riqueza no te ayudará en el día del juicio, pero la bondad te salvará de la muerte.
Utajiri haufaidi kitu katika siku ya ghadhabu, bali haki huokoa kutoka mautini.
5 La bondad del inocente lo mantendrá en el buen camino, pero los malvados tropezarán y caerán por su propia maldad.
Haki ya wasio na lawama, huwatengenezea njia iliyonyooka, bali waovu huangushwa kwa uovu wao wenyewe.
6 La bondad de los que viven en rectitud los salvará, pero los deshonestos quedarán atrapados por sus propios deseos.
Haki ya wanyofu huwaokoa, bali wasio waaminifu hunaswa na tamaa mbaya.
7 Cuando una persona malvada muere, sus esperanzas mueren con ella; la esperanza de los rebeldes se desvanecerá.
Wakati mtu mwovu anapokufa, matumaini yake hutoweka; yote aliyoyatazamia kutokana na nguvu zake huwa si kitu.
8 Los rectos son librados de las dificultades, pero los malvados estarán en dificultades.
Mtu mwenye haki huokolewa kutoka taabu, naye mtu mwovu huingia humo badala yake.
9 Los rebeldes contra Dios discuten su voluntad y destruyen a su prójimo; pero los justos son salvados por la sabiduría.
Kwa kinywa chake mtu asiyemwamini Mungu humwangamiza jirani yake, bali kwa maarifa mwenye haki huokolewa.
10 Toda la ciudad celebra cuando los buenos tienen éxito; así mismo gritan de alegría cuando mueren los malvados.
Wakati mwenye haki anapofanikiwa, mji hufurahi; mwovu atowekapo, kuna kelele za furaha.
11 Los que viven con ética son una bendición para la ciudad, pero las palabras de los malvados la destruyen.
Kutokana na baraka ya mtu mnyofu mji hukwezwa, bali kwa kinywa cha mwovu mji huharibiwa.
12 Los que denigran a su prójimo no tienen inteligencia; pero los sensatos guardan silencio.
Mtu asiye na akili humdharau jirani yake, bali mtu mwenye ufahamu huuzuia ulimi wake.
13 Una persona chismosa anda de aquí para allá divulgando secretos; pero una persona fiel guarda el secreto que le han confiado.
Masengenyo husaliti tumaini, bali mtu mwaminifu hutunza siri.
14 Sin una buena guía, la nación cae; pero la nación se salva por los muchos consejos sabios.
Pasipo ushauri wa hekima taifa huanguka, bali washauri wengi hufanya ushindi uwe wa hakika.
15 Si eres fiador de un extranjero, te meterás en problemas. Estarás más seguro si evitas tales promesas.
Yeye amdhaminiye mgeni hakika atateseka, bali yeyote akataaye kuunga mkono dhamana ni salama.
16 Una mujer refinada se aferra a su honra, así como los hombres implacables se aferran a su riqueza.
Mwanamke mwenye moyo wa huruma hupata heshima, bali wanaume wakorofi hupata mali tu.
17 Si eres bondadoso, obtendrás recompensa; pero si eres cruel, te harás daño a ti mismo.
Mwenye huruma hujinufaisha mwenyewe, bali mkatili hujiletea taabu mwenyewe.
18 El salario que reciben los malvados es engañoso, pero los que siembran bondad, cosecharán una buena recompensa.
Mtu mwovu hupata ujira wa udanganyifu, bali yeye apandaye haki huvuna tuzo ya uhakika.
19 Haz el bien y vivirás. Busca el mal y morirás.
Mtu mwenye haki kweli kweli hupata uzima, bali yeye afuatiliaye ubaya huendea kifo chake.
20 El Señor odia las mentes perversas, pero se complace con los que viven una vida de obediencia.
Bwana huwachukia sana watu wenye moyo wa upotovu, bali hupendezwa na wale ambao njia zao hazina lawama.
21 De algo puedes estar seguro: los malvados no se quedaran sin castigo, pero los justos serán salvos.
Uwe na hakika na hili: Waovu hawataepuka kuadhibiwa, bali wenye haki watakuwa huru.
22 Una mujer hermosa con carencia de buen juicio es como una argolla de oro en el hocico de un cerdo.
Kama pete ya dhahabu katika pua ya nguruwe ndivyo alivyo mwanamke mzuri ambaye hana busara.
23 A las buenas personas les espera lo mejor, pero la esperanza de los malvados terminara en muerte.
Shauku ya mwenye haki huishia tu kwenye mema, bali tumaini la mwovu huishia tu kwenye ghadhabu.
24 Si das con generosidad, recibirás más; pero si eres mezquino terminaras en la pobreza.
Kuna mtu atoaye kwa ukarimu, hata hivyo hupata zaidi, mwingine huzuia, lakini huwa maskini.
25 Si eres generoso te volverás rico; dale a los demás un vaso de agua y recibirás uno también.
Mtu mkarimu atastawi; yeye awaburudishaye wengine ataburudishwa mwenyewe.
26 La gente maldice a los que acumulan el trigo, pero bendicen a quienes lo venden.
Watu humlaani mtu awanyimae watu nafaka, bali baraka itamkalia kichwani kama taji yeye aliye radhi kuiuza.
27 Si procuras hacer el bien, serás estimado; pero si buscas el mal, lo encontraras!
Yeye atafutaye mema hupata ukarimu, bali ubaya huja kwake yeye autafutaye.
28 Si pones tu confianza en tus riquezas, caerás; pero si haces el bien, florecerás como hojas verdes.
Yeyote ategemeaye utajiri wake ataanguka, bali mwenye haki atastawi kama jani bichi.
29 Si eres causa de problemas en tu familia, apenas heredaras aire. Los necios terminan siendo siervos de los que piensan con sabiduría.
Yeye aletaye taabu kwa jamaa yake atarithi tu upepo, naye mpumbavu atakuwa mtumishi wa wenye hekima.
30 El fruto de los justos es un árbol de vida. La persona sabia salva a las demás personas.
Tunda la mwenye haki ni mti wa uzima, naye mwenye hekima huvuta roho za watu.
31 Si los justos reciben recompensa aquí en la tierra, ¡cuanto más los malvados!
Kama wenye haki watapokea ujira wao duniani, si zaidi sana yule asiyemcha Mungu na mwenye dhambi?

< Proverbios 11 >