< Números 33 >

1 Este es un registro de los viajes realizados por los israelitas al salir de Egipto en sus divisiones tribales lideradas por Moisés y Aarón.
Hizi ndizo safari za wana wa Israeli hapo walipotoka katika nchi ya Misri pamoja na makundi yao ya kijeshi chini ya uongozi wa Musa na Haruni.
2 Moisés registró las diferentes partes de su viaje según las instrucciones del Señor. Estos son los viajes que hicieron listados en orden desde donde comenzaron:
Musa aliandika maeneo yote tangu walipoondoka mpaka walipofika, kama alivyoamuriwa na BWANA. Hizi ndizo safari zao kama kutoka kwao kulivyokuwa kwa kila walipotoka.
3 Los israelitas dejaron Ramsés el día quince del primer mes, el día después de la Pascua. Salieron triunfantes mientras todos los egipcios observaban.
Mwezi wa kwanza walisafiri kutoka Ramesi, waliondoka siku ya kumi na tano. Asubuhi siku iliyofuata baada ya Pasaka, Wana wa Israeli waliondoka wazi wazi, mbele ya machoya Wamisri wote.
4 Los egipcios enterraban a todos sus primogénitos que el Señor había matado, porque el Señor había hecho caer sus juicios sobre sus dioses.
Hii ilitokea wakati Wamisiri walipokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza, ambao BWANA alikuwa amewaua miongoni mwao, kwa kuwa pia alikuwa ameiadhibu miungu yao.
5 Los israelitas dejaron Ramsés e instalaron un campamento en Sucot.
Wana wa Israeli walisafiri kutoka Ramesi na kuweka kambi
6 Se fueron de Sucot y acamparon en Etam, en la frontera con el desierto.
Sukothi. Walisafiri toka Sukothi na kuweka kambi Ethamu, mwisho wa nyika.
7 Se alejaron de Etam, volviendo a Pi-hahiroth, frente a Baal-zefón, y acamparon cerca de Migdol.
Wakasafiri kutoka Ethamu wakarudi mpaka Pi-Hahirothi, ambayo inaikabili Baali Zephoni, ambapo waliweka kambi kuikabili Migidoli
8 Se mudaron de Pi-hahirot y cruzó por el medio del mar hacia el desierto. Viajaron durante tres días al desierto de Etham y establecieron un campamento en Marah.
Kisha wakasafiri toka mkabala wa Pi-Hairothi na kupita katikati ya bahari kuelekea nyikani. Wakasafiri safari ya siku tatu katika nyika ya Ethamu na kuweka kambi Mara.
9 Se desplazaron desde Mara y llegaron a Elim, donde había doce manantiales de agua y setenta palmeras, y acamparon allí.
Wakasafiri kutoka Mara kufika Elimu. Pale Elimu kulikuwa na chemichemi kumi na mbili za maji na miti sabini ya mitende. hapo ndipo walipoweka kambi.
10 Se trasladaron de Elim y acamparon al lado del Mar Rojo.
Walisafiri kutoka Elimu na kuweka kambi karibu na Bahari ya Shamu.
11 Se trasladaron desde el Mar Rojo y acamparon en el Desierto del Pecado.
Walisafiri kutoka Bahari ya Shamu na kuweka kambi katika nyika ya Sini.
12 Se trasladaron del desierto de Sin y acamparon en Dofca.
Walisafiri kutoka nyika ya Sini na kuweka kambi Dofka.
13 Se mudaron de Dofca y acamparon en Alús.
Wakasafiri kutoka Dofka na kuweka kambi Alushi.
14 Se mudaron de Alús y acamparon en Refidím. No había agua allí para que la gente bebiera.
Wakasafiri kutoka Alushi na kuweka kambi Refidimu, ambapo watu walikosa maji ya kunywa.
15 Se fueron de Refidim y acamparon en el desierto del Sinaí.
Walisafiri kutoka Refidimu na kuweka kambi kwenye nyika ya Sinai.
16 Se fueron del desierto del Sinaí y acamparon en Kibroth-hataava.
Walisafiri kutoka nyika ya Sinai na kuweka kambi Kibrothi Hataava.
17 Se mudaron de Kibroth-hattaavah y acamparon en Hazerot.
Walisafiri kutoka Kibrothi Hataava na kuweka kambi Hazerothi.
18 Se trasladaron de Hazerot y establecieron un campamento en Ritma.
Walisafiri kutoka Hazerothi na kuweka kambi Rithima.
19 Se trasladaron de Ritma y establecieron un campamento en Rimón-fares.
Walisafiri kutoka Rithima na kuweka kambi Rimoni Perezi.
20 Se trasladaron de Rimmon-fares y acamparon en Libna.
Walisafiri kutoka Rimoni Perezi na kuweka kambi Libna.
21 Se trasladaron de Libna y establecieron un campamento en Rissa.
Walisafiri kutoka Libna na kuweka kambi Risa.
22 Se trasladaron de Rissa y establecieron un campamento en Ceelata.
Walisafiri kutoka Risa na kuweka kambi Kehelatha.
23 Se trasladaron de Ceelata y acamparon en el Monte Sefer.
Walisafiri kutoka Kehelatha na kuweka kambi kwenye Mlima Sheferi.
24 Se trasladaron del Monte Sefer y acamparon en Harada.
Walisafiri kutoka Mlima Sheferi na kuweka kambi Harada.
25 Se trasladaron de Harada y acamparon en Macelot.
Walisafiri kutoka Harada na kuweka kambi Makelothi.
26 Se trasladaron de Macelot y acamparon en Tahat.
Walisafiri kutoka Makelothi na kuweka kambi Tahathi.
27 Se fueron de Tahat y acamparon en Tara.
Walisafiri kutoka Ttahalathi na kuweka kambi Tera.
28 Se mudaron de Tara y acamparon en Mitca.
Walisafiri kutokaTera na kuweka kambi Mithika.
29 Se mudaron de Mitca y acamparon en Hasmona.
Walisafiri kutoka Mithika na kuweka kambi Hashimona.
30 Se fueron de Hasmona y acamparon en Moserot.
Walisafiri kutoka Hashimona na kuweka kambi Moserothi.
31 Se mudaron de Moserot y acamparon en Bene-jaacán.
Walisafiri kutoka Moserothi na kuweka kambi Bene Jaakani.
32 Se mudaron de Bene-jaacán y acamparon en Hor-haggidgad.
Walisafiri kutoka Bene Jaakani na kuweka kambi Hori Hagidigadi.
33 Se trasladaron de Hor-haggidgad y acamparon en Jotbata.
Walisafiri kutoka Hori Hagidigadi na kuweka kambi Jotibatha.
34 Se mudaron de Jotbata y establecieron un campamento en Abrona.
Walisafiri kutoka Jotibatha na kuweka kambi Abrona.
35 Se mudaron de Abrona y acamparon en Ezión-geber.
Walisafiri kutoka Abrona na kuweka kambi Ezioni Geberi.
36 Se trasladaron de Ezion-geber y acamparon en Cades, en el desierto de Zin.
Walisafiri toka Ezioini Geberi na kuweka kambi katika nyika ya Sini kule Kadeshi.
37 Se trasladaron de Cades y acamparon en el monte Hor, en la orilla de Edom.
Walisafiri kutoka Kadeshi na kuweka kambi Mlima Hori, Pembezoni mwa nchi ya Edomu.
38 El sacerdote Aarón subió al monte Hor como el Señor le había ordenado, y murió allí el primer día del quinto mes, en el cuadragésimo año después de que los israelitas hubieran salido de Egipto.
Hapo ndipo Haruni kuhani alipoenda kwenye Mlima Hori kwa amri ya BWANA na kufa kule mwaka wa arobaini bada ya Wisraeli kutoka katika nchi ya Misri, katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano.
39 Aarón tenía 123 años cuando murió en el Monte Hor.
Haruni alikuwa na umri wa mika 123 alipokufa pale juu ya Mlima Hori.
40 (El rey cananeo de Arad, que vivía en el Néguev en el país de Canaán, se enteró de que los israelitas estaban en camino).
Wakanaani, mfalme wa Aradi, ambao waliishi kusini mwa nyika katika nchi ya Kanaani, walisikia juu ya ujio wa wana wa Israeli.
41 Los israelitas se trasladaron del Monte Hor y establecieron un campamento en Zalmona.
Walisafiri kutika Mlima Hori n a kuweka kambi Zalimona.
42 Se trasladaron de Zalmona y acamparon en Punón.
Walisafiri kutoka Zalimona na kuweka kambi Punoni.
43 Se trasladaron de Punón y acamparon en Obot.
Walisafiri kutoka Punoni na kuweka kambi Obothi.
44 Se trasladaron de Oboth y acamparon en Iye-abarim, en la frontera de Moab.
Walisafiri kutoka Obothi na kuweka kambi Abarimu, katika mpaka wa Moabu.
45 Se mudaron de Iye-abarim y acamparon en Dibon-gad.
Walisafiri kutoka Abarimu na kuweka kambi Diboni Gadi.
46 Se mudaron de Dibon-gad y acamparon en Almon-diblataim.
Walisafiri kutoka Diboni Gadi na kuweka kambi Alimoni Diblathaimu.
47 Se mudaron de Almon-diblataim y acamparon en las montañas de Abarim, frente a Nebo.
Walisafiri kutoka Alimoni Diblathaimu na kuweka kambi kwenye milima ya Abarimu mkabala na Nebo.
48 Se trasladaron de las montañas de Abarim y acamparon en las llanuras de Moab, junto al Jordán, frente a Jericó.
Walisafiri kutoka mlima wa Abarimuna kuweka kambi kwenye nyanda za Moabu karibu na Yorodani huko Yeriko.
49 Allí, en las llanuras de Moab, acamparon al lado del Jordán, desde Beth-jesimot hasta Abel-sitim.
Waliweka kambi karibu na Yorodani, kutoka Bethi Jeshimothi mpaka Abeli Shitimu katika nyanda za Moabu.
50 Aquí fue donde, en la llanura de Moab junto al Jordán, frente a Jericó, el Señor le dijo a Moisés,
Hapo BWANA alinenana Musa katika nyanda za Moabu karibu na Yorodani kule Yeriko akasema,
51 “Dile a los israelitas: Tan pronto crucen el Jordán y entren en el país de Canaán,
“Nena na wana wa Israeli uwaambie. 'Mtakapovuka mto Yorodani kuingia Kanaani,
52 deben expulsar a todos los que viven en la tierra, destruir todas sus imágenes talladas e ídolos de metal, y derribar todos sus templos paganos.
ndipo mtakapowafukuza wenyeji wote mbele yenu. Mtaziharibu sanamu zote za kuchongwa. Mtaziharibu sanamu zao za kusubu na kuharibu mahali pao pote palipoinuka.
53 Debes tomar el país y establecerte allí, porque te he dado la tierra y te pertenece.
Mtachukua hiyo ardhi iwe mali yenu na muishi ndani yake, kwa sababu nimewapeni hiyo nchi iwe mali yenu.
54 Debes dividir la tierra y asignarla por sorteo a las diferentes familias tribales. Dale una porción más grande a una familia más grande, y una porción más pequeña a una familia más pequeña. La asignación de cada uno se decide por sorteo, y todos ustedes recibirán una asignación dependiendo de su tribu.
Mtairithi hiyo nchi kwa kupiga kura, kwa kufuata kila ukoo. Kwa zile koo kubwa kubwa mtawapa sehemu kubwa ya ardhi, na kwa zile koo ndogo ndogo mtawapa sehemu ndogo ya ardhi. Kura itakapoanguka kwenye kila ukoo, hiyo ardhi itakuwa mali yake. Mtairithi ardhi kufuata ukoo wa kabilla la jamaa zenu.
55 “Pero si no expulsan a todos los que viven en la tierra, las personas que dejen permanecer serán como arena en sus ojos y espinas en sus costados. Les causarán problemas cuando se establezcan en el país.
Lakini kama hamtawafukuza wenyeji wa nchi hiyo watoke mbele yenu, ndipo wale watu mtakaowaruhusu wakae nanyi watakapokuwa kama sindano machoni mwenu na miiba katika mbavu zenu. Watayafanya maisha yenu yawe magumu katika nchi mnayoishi.
56 Eventualmente, el castigo que planeé para ellos se los infligiré a ustedes”.
Ndipo itakapotokea kuwa kile ambacho Mimi ninakusudia kufanya kwa wale watu, Nitawafanyia pia ninyi'”

< Números 33 >