< Números 33 >

1 Este es un registro de los viajes realizados por los israelitas al salir de Egipto en sus divisiones tribales lideradas por Moisés y Aarón.
Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
2 Moisés registró las diferentes partes de su viaje según las instrucciones del Señor. Estos son los viajes que hicieron listados en orden desde donde comenzaron:
Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
3 Los israelitas dejaron Ramsés el día quince del primer mes, el día después de la Pascua. Salieron triunfantes mientras todos los egipcios observaban.
Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
4 Los egipcios enterraban a todos sus primogénitos que el Señor había matado, porque el Señor había hecho caer sus juicios sobre sus dioses.
waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
5 Los israelitas dejaron Ramsés e instalaron un campamento en Sucot.
Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
6 Se fueron de Sucot y acamparon en Etam, en la frontera con el desierto.
Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
7 Se alejaron de Etam, volviendo a Pi-hahiroth, frente a Baal-zefón, y acamparon cerca de Migdol.
Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
8 Se mudaron de Pi-hahirot y cruzó por el medio del mar hacia el desierto. Viajaron durante tres días al desierto de Etham y establecieron un campamento en Marah.
Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
9 Se desplazaron desde Mara y llegaron a Elim, donde había doce manantiales de agua y setenta palmeras, y acamparon allí.
Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
10 Se trasladaron de Elim y acamparon al lado del Mar Rojo.
Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
11 Se trasladaron desde el Mar Rojo y acamparon en el Desierto del Pecado.
Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
12 Se trasladaron del desierto de Sin y acamparon en Dofca.
Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
13 Se mudaron de Dofca y acamparon en Alús.
Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
14 Se mudaron de Alús y acamparon en Refidím. No había agua allí para que la gente bebiera.
Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
15 Se fueron de Refidim y acamparon en el desierto del Sinaí.
Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
16 Se fueron del desierto del Sinaí y acamparon en Kibroth-hataava.
Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
17 Se mudaron de Kibroth-hattaavah y acamparon en Hazerot.
Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
18 Se trasladaron de Hazerot y establecieron un campamento en Ritma.
Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
19 Se trasladaron de Ritma y establecieron un campamento en Rimón-fares.
Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
20 Se trasladaron de Rimmon-fares y acamparon en Libna.
Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
21 Se trasladaron de Libna y establecieron un campamento en Rissa.
Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
22 Se trasladaron de Rissa y establecieron un campamento en Ceelata.
Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
23 Se trasladaron de Ceelata y acamparon en el Monte Sefer.
Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
24 Se trasladaron del Monte Sefer y acamparon en Harada.
Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
25 Se trasladaron de Harada y acamparon en Macelot.
Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
26 Se trasladaron de Macelot y acamparon en Tahat.
Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
27 Se fueron de Tahat y acamparon en Tara.
Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
28 Se mudaron de Tara y acamparon en Mitca.
Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
29 Se mudaron de Mitca y acamparon en Hasmona.
Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
30 Se fueron de Hasmona y acamparon en Moserot.
Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
31 Se mudaron de Moserot y acamparon en Bene-jaacán.
Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
32 Se mudaron de Bene-jaacán y acamparon en Hor-haggidgad.
Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
33 Se trasladaron de Hor-haggidgad y acamparon en Jotbata.
Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
34 Se mudaron de Jotbata y establecieron un campamento en Abrona.
Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
35 Se mudaron de Abrona y acamparon en Ezión-geber.
Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
36 Se trasladaron de Ezion-geber y acamparon en Cades, en el desierto de Zin.
Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
37 Se trasladaron de Cades y acamparon en el monte Hor, en la orilla de Edom.
Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
38 El sacerdote Aarón subió al monte Hor como el Señor le había ordenado, y murió allí el primer día del quinto mes, en el cuadragésimo año después de que los israelitas hubieran salido de Egipto.
Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
39 Aarón tenía 123 años cuando murió en el Monte Hor.
Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
40 (El rey cananeo de Arad, que vivía en el Néguev en el país de Canaán, se enteró de que los israelitas estaban en camino).
Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
41 Los israelitas se trasladaron del Monte Hor y establecieron un campamento en Zalmona.
Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
42 Se trasladaron de Zalmona y acamparon en Punón.
Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
43 Se trasladaron de Punón y acamparon en Obot.
Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
44 Se trasladaron de Oboth y acamparon en Iye-abarim, en la frontera de Moab.
Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
45 Se mudaron de Iye-abarim y acamparon en Dibon-gad.
Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
46 Se mudaron de Dibon-gad y acamparon en Almon-diblataim.
Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
47 Se mudaron de Almon-diblataim y acamparon en las montañas de Abarim, frente a Nebo.
Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
48 Se trasladaron de las montañas de Abarim y acamparon en las llanuras de Moab, junto al Jordán, frente a Jericó.
Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
49 Allí, en las llanuras de Moab, acamparon al lado del Jordán, desde Beth-jesimot hasta Abel-sitim.
Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
50 Aquí fue donde, en la llanura de Moab junto al Jordán, frente a Jericó, el Señor le dijo a Moisés,
Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
51 “Dile a los israelitas: Tan pronto crucen el Jordán y entren en el país de Canaán,
“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
52 deben expulsar a todos los que viven en la tierra, destruir todas sus imágenes talladas e ídolos de metal, y derribar todos sus templos paganos.
wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
53 Debes tomar el país y establecerte allí, porque te he dado la tierra y te pertenece.
Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
54 Debes dividir la tierra y asignarla por sorteo a las diferentes familias tribales. Dale una porción más grande a una familia más grande, y una porción más pequeña a una familia más pequeña. La asignación de cada uno se decide por sorteo, y todos ustedes recibirán una asignación dependiendo de su tribu.
Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
55 “Pero si no expulsan a todos los que viven en la tierra, las personas que dejen permanecer serán como arena en sus ojos y espinas en sus costados. Les causarán problemas cuando se establezcan en el país.
“‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
56 Eventualmente, el castigo que planeé para ellos se los infligiré a ustedes”.
Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”

< Números 33 >