< Números 1 >

1 El Señor le habló a Moisés en el Tabernáculo de Reunión mientras estaban en el desierto del Sinaí. Esto fue el primer día del segundo mes, dos años después de que los israelitas salieran de Egipto. Le dijo:
Bwana alisema na Mose katika Jangwa la Sinai, katika Hema la Kukutania, siku ya kwanza ya mwezi wa pili, katika mwaka wa pili baada ya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Akamwambia,
2 “Censen a todos los israelitas según su tribu y su familia. Cuenten a cada hombre y mantengan un registro del nombre de cada uno.
“Hesabu watu wa jumuiya yote ya Waisraeli kwa kufuata koo zao na jamaa zao, ukiorodhesha kila mwanaume kwa jina lake, mmoja mmoja.
3 Tú y Aarón deberán registrar a todos los mayores de veinte años que sean aptos para prestar el servicio militar según sus divisiones en el ejército israelita.
Wewe na Aroni mtawahesabu kwa migawanyo yao wanaume wote katika Israeli wenye miaka ishirini na kuendelea ambao wanaweza kutumika katika jeshi.
4 Para ayudarlos habrá estar con ustedes un representante de cada tribu, que es el jefe de cada familia:
Mwanaume mmoja kutoka kila kabila, kila aliye kiongozi wa jamaa yake, atawasaidia.
5 “Estos son los nombres de los hombres que trabajarán con ustedes: De la tribu de Rubén, Elisur, hijo de Sedeur;
Haya ndiyo majina ya wanaume watakaowasaidia: “kutoka Reubeni, ni Elisuri mwana wa Shedeuri;
6 de la tribu de Simeón, Selumiel, hijo de Zurisadai;
kutoka Simeoni, ni Shelumieli mwana wa Surishadai;
7 de la tribu de Judá, Naasón, hijo de Aminadab;
kutoka Yuda, ni Nashoni mwana wa Aminadabu;
8 de la tribu de Isacar, Nataanel, hijo de Zuar;
kutoka Isakari, ni Nethaneli mwana wa Suari;
9 de la tribu de Zabulón, Eliab, hijo de Helón;
kutoka Zabuloni, ni Eliabu mwana wa Heloni;
10 de los hijos de José: de la tribu de Efraín, Elisama, hijo de Amihud; y de la tribu de Manasés, Gamaliel, hijo de Pedasur;
kutoka wana wa Yosefu: kutoka Efraimu, ni Elishama mwana wa Amihudi; kutoka Manase, ni Gamalieli mwana wa Pedasuri;
11 de la tribu de Benjamín, Abidán, hijo de Gedeoni;
kutoka Benyamini, ni Abidani mwana wa Gideoni;
12 de la tribu de Dan, Ajiezer, hijo de Amisadai;
kutoka Dani, ni Ahiezeri mwana wa Amishadai;
13 de la tribu de Aser, Pagiel, hijo de Ocrán;
kutoka Asheri, ni Pagieli mwana wa Okrani;
14 de la tribu de Gad, Eliasaf, hijo de Deuel;
kutoka Gadi, ni Eliasafu mwana wa Deueli;
15 y de la tribu de Neftalí, Ahira, hijo de Enán”.
kutoka Naftali, ni Ahira mwana wa Enani.”
16 Estos fueron los hombres elegidos de la comunidad israelita. Eran los jefes de las tribus de sus padres; los jefes de las familias de Israel.
Hawa walikuwa wanaume walioteuliwa kutoka jumuiya, viongozi wa makabila ya baba zao. Walikuwa wakuu wa koo za Israeli.
17 Moisés y Aarón convocaron a estos hombres que habían sido seleccionados por nombre.
Mose na Aroni wakawachukua wanaume hao waliokuwa wamepewa majina yao,
18 Hicieron que todos los israelitas se reunieran el primer día del segundo mes, y registraron la genealogía del pueblo según su tribu y familia, y contaron los nombres de todos los que tenían veinte años o más,
wakaita jumuiya yote pamoja katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Watu wakaonyesha nasaba zao kwa koo zao na jamaa zao, nao wanaume waliokuwa na miaka ishirini au zaidi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja,
19 como el Señor le había dicho a Moisés que hiciera. Moisés llevó a cabo este censo en el desierto del Sinaí.
kama Bwana alivyomwagiza Mose. Hivyo aliwahesabu katika Jangwa la Sinai:
20 Los descendientes de Rubén, (que era el hijo primogénito de Israel), hombres de veinte años o más, fueron registrados por nombre según los registros genealógicos de su tribu y familias. Y todos los hombres registrados que estaban aptos para servir en el ejército
Kutoka wazao wa Reubeni, mzaliwa wa kwanza wa kiume wa Israeli: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
21 n la tribu de Rubén sumaron 46.500.
Idadi kutoka kabila la Reubeni ilikuwa watu 46,500.
22 Los descendientes de Simeón, hombres de veinte años o más, fueron registrados por nombre según los registros genealógicos de su tribu y sus familias. Todos hombres registrados que estaban aptos para servir en el ejército,
Kutoka wazao wa Simeoni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi walihesabiwa na kuorodheshwa kwa majina, mmoja mmoja, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
23 de la tribu de Simeón, sumaron 59.300.
Idadi kutoka kabila la Simeoni walikuwa watu 59,300.
24 Los descendientes de Gad, hombres de veinte años o más, fueron registrados por nombre según los registros genealógicos de su tribu y sus familias. Todos los hombres registrados que estaban aptos para servir en el ejército,
Kutoka wazao wa Gadi: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
25 de la tribu de Gad, sumaron 45.650.
Idadi kutoka kabila la Gadi walikuwa watu 45,650.
26 Los descendientes de Judá, hombres de veinte años o más, fueron registrados por nombre según los registros genealógicos de su tribu y sus familias. Todos los hombres inscritos, que estaban aptos para servir en el ejército,
Kutoka wazao wa Yuda: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
27 de la tribu de Judá, sumaron 74.600.
Idadi kutoka kabila la Yuda walikuwa watu 74,600.
28 Los descendientes de Isacar, hombres de veinte años o más, fueron registrados por nombre según los registros genealógicos de su tribu y sus familias. Todos los hombres inscritos que eran aptos para servir en el ejército,
Kutoka wazao wa Isakari: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
29 de la tribu de Isacar, sumaron 54.400.
Idadi kutoka kabila la Isakari walikuwa watu 54,400.
30 Los descendientes de Zabulón, hombres de veinte años o más, fueron registrados por nombre según los registros genealógicos de su tribu y sus familias. Todos los hombres inscritos que estaban aptos para servir en el ejército,
Kutoka wazao wa Zabuloni: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
31 de la tribu de Zabulón, sumaron 57.400.
Idadi kutoka kabila la Zabuloni walikuwa watu 57,400.
32 Los descendientes de José: los descendientes de Efraín, hombres de veinte años o más, fueron registrados por nombre según los registros genealógicos de su tribu y sus familias. Todos los hombres registrados que estaban aptos para servir en el ejército
Kutoka wana wa Yosefu: Kutoka wazao wa Efraimu: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
33 de la tribu de Efraín, sumaron 40.500.
Idadi kutoka kabila la Efraimu walikuwa watu 40,500.
34 Y los descendientes de Manasés, hombres de veinte años o más, fueron registrados por nombre según los registros genealógicos de su tribu y sus familias. Todos los hombres registrados que estaban aptos para servir en el ejército
Kutoka wazao wa Manase: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
35 de la tribu de Manasés, sumaron 32.200.
Idadi kutoka kabila la Manase walikuwa watu 32,200.
36 Los descendientes de Benjamín, hombres de veinte años o más, fueron registrados por nombre según los registros genealógicos de su tribu y sus familias. Todos los hombres registrados que estaban aptos para servir en el ejército,
Kutoka wazao wa Benyamini: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
37 de la tribu de Benjamín, totalizaban 35.400.
Idadi kutoka kabila la Benyamini walikuwa watu 35,400.
38 Los descendientes de Dan, hombres de veinte años o más, fueron registrados por nombre según los registros genealógicos de su tribu y sus familias. Todos los hombres registrados que estaban aptos para servir en el ejército,
Kutoka wazao wa Dani: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
39 de la tribu de Dan, sumaron 62.700.
Idadi kutoka kabila la Dani walikuwa watu 62,700.
40 Los descendientes de Aser, hombres de veinte años o más, fueron registrados por nombre según los registros genealógicos de su tribu y sus familias. Todos los hombres inscritos que estaban aptos para servir en el ejército,
Kutoka wazao wa Asheri: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
41 de la tribu de Aser, sumaron 41.500.
Idadi kutoka kabila la Asheri walikuwa watu 41,500.
42 Los descendientes de Neftalí, hombres de veinte años o más, fueron registrados por nombre según los registros genealógicos de su tribu y sus familias. Todos los hombres inscritos que estaban aptos para servir en el ejército,
Kutoka wazao wa Naftali: Wanaume wote waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi waliorodheshwa kwa majina, kufuatana na kumbukumbu za koo zao na jamaa zao.
43 de la tribu de Neftalí, sumaron 53.400.
Idadi kutoka kabila la Naftali walikuwa watu 53,400.
44 Estos fueron los totales de los hombres contados y registrados por Moisés y Aarón, con la ayuda de los doce líderes de Israel, que representaban cada uno a su familia.
Hawa walikuwa wanaume waliohesabiwa na Mose, Aroni na viongozi kumi na wawili wa Israeli, kila mmoja akiwakilisha jamaa yake.
45 De esta manera, todos los hombres israelitas de veinte años o más que pudieron servir en el ejército de Israel fueron registrados según sus familias.
Wanaume wote Waisraeli waliokuwa na miaka ishirini au zaidi ambao waliweza kutumika katika jeshi la Israeli walihesabiwa kufuatana na jamaa zao.
46 La suma total de los registrados fue de 603.550.
Jumla ya hesabu yao ilikuwa watu 603,550.
47 Sin embargo, los levitas no estaban registrados con los demás según su tribu y sus familias.
Hata hivyo, jamaa ya kabila la Lawi hawakuhesabiwa pamoja na wengine.
48 Esto se debió a que el Señor le había dicho a Moisés:
Bwana alikuwa amemwambia Mose:
49 “No registres la tribu de Leví, ni los cuentes en el censo con los otros israelitas.
“Kamwe usihesabu kabila la Lawi wala kuwaweka pamoja katika hesabu ya Waisraeli wengine.
50 Pon a los levitas a cargo del Tabernáculo y del Testimonio, así como de todo su mobiliario y de todo lo que hay en él. Ellos serán los responsables de llevar el Tabernáculo y todos sus artículos. Deben cuidarlo, y hacer su campamento alrededor de él.
Badala yake, waweke Walawi kuwa viongozi wa Maskani ya Ushuhuda, juu ya samani zake na kila kitu kilichomo ndani yake. Wao watabeba Maskani na samani zake zote; wataitunza na kupiga kambi kuizunguka.
51 Cuando llegue el momento de trasladar el Tabernáculo, los levitas lo bajarán, y cuando llegue el momento de acampar, los levitas lo levantarán. Cualquier forastero que se acerque al Tabernáculo debe ser condenado a muerte.
Wakati wowote Maskani inapohamishwa, Walawi wataifungua, na wakati wowote maskani inapotakiwa kusimamishwa, Walawi watafanya kazi hiyo. Mtu yeyote mwingine ambaye atasogea karibu nayo atauawa.
52 Los israelitas acamparán por tribus, cada uno estará en su propio campamento, bajo su propia bandera.
Waisraeli watapiga mahema yao kwa makundi makundi, kila mwanaume katika kambi yake mwenyewe chini ya bendera yake.
53 Pero los levitas deben levantar su campamento alrededor del Tabernáculo del Testimonio para evitar que alguien me haga enojar con los israelitas. Los levitas son responsables de cuidar el Tabernáculo del Testimonio”.
Hata hivyo, Walawi watapiga mahema yao kuzunguka Maskani ya Ushuhuda ili ghadhabu isiipate jumuiya ya Waisraeli. Walawi watawajibika kwa utunzaji wa Maskani ya Ushuhuda.”
54 Los israelitas hicieron todo lo que el Señor les ordenó a través de Moisés.
Waisraeli walifanya yote haya sawasawa kama Bwana alivyomwamuru Mose.

< Números 1 >