< Nehemías 3 >

1 Eliasib, el sumo sacerdote, y otros sacerdotes con él, comenzaron a reconstruir la Puerta de las Ovejas. La dedicaron y colocaron sus puertas. Luego siguieron construyendo hasta la Torre de los Cien y la Torre de Hananel y la dedicaron.
Eliashibu kuhani mkuu na makuhani wenzake walikwenda kufanya kazi na kulijenga upya Lango la Kondoo. Waliliweka wakfu na kuweka milango mahali pake, wakajenga hadi kufikia Mnara wa Mia, ambao waliuweka wakfu hadi Mnara wa Hananeli.
2 Los hombres de Jericó construyeron la parte contigua a Eliasib, y Zacur, hijo de Imri, construyó la siguiente.
Watu wa Yeriko wakajenga sehemu zilizopakana nao, naye Zakuri mwana wa Imri akajenga karibu nao.
3 La Puerta del Pescado fue reconstruida por los hijos de Senaa. Colocaron sus vigas y levantaron sus puertas, junto con sus cerrojos y barras.
Lango la Samaki lilijengwa upya na wana wa Hasenaa. Waliweka boriti zake, na wakaweka milango yake na makomeo na nondo.
4 La siguiente sección fue reparada por Meremot, hijo de Urías, hijo de Cos; junto a él, estaba Mesulam, hijo de Berequías, hijo de Mesezabeel; y junto a él, Sadoc, hijo de Baana.
Meremothi mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, alikarabati sehemu iliyofuatia. Baada yake Meshulamu mwana wa Berekia, mwana wa Meshezabeli, alifanya ukarabati na aliyemfuatia ni Sadoki mwana wa Baana.
5 A continuación estaban los tecoítas, pero sus nobles se negaron a realizar trabajos manuales bajo un supervisor.
Sehemu iliyofuatia ilikarabatiwa na watu kutoka Tekoa, lakini wakuu wao walikataa kufanya kazi chini ya wasimamizi wao.
6 La Puerta Vieja fue reparada por Joiada, hijo de Paseah, y Mesulam, hijo de Besodías. Colocaron sus vigas y levantaron sus puertas, junto con sus cerrojos y barras.
Lango la Yeshana lilikarabatiwa na Yoyada mwana wa Pasea, na Meshulamu mwana wa Besodeya. Waliweka boriti zake, na wakaweka milango, makomeo na nondo.
7 Luego fueron Melatiá el gabaonita, Jadón el meronita y los hombres de Gabaón y Mizpa, que estaban bajo la jurisdicción del gobernador de la provincia al oeste del Éufrates.
Karibu nao ukarabati ulifanywa na watu kutoka Gibeoni na Mispa, yaani Melati Mgibeoni, na Yadoni Mmeronothi, sehemu hizi zikiwa chini ya mamlaka ya mtawala wa Ngʼambo ya Frati.
8 A continuación estaba Uziel, hijo de Harhaiah, uno de los orfebres; y junto a él, Hananías, hijo del perfumista. Ellos reforzaron Jerusalén hasta el Muro Ancho.
Uzieli mwana wa Harhaya, mmoja wa masonara, alikarabati sehemu iliyofuatia, naye Hanania mmoja wa watengenezaji marashi akakarabati sehemu iliyofuatia. Walitengeneza Yerusalemu mpaka kufikia Ukuta Mpana.
9 El siguiente fue Refaías, hijo de Hur, gobernante de la mitad de Jerusalén.
Refaya mwana wa Huri, mtawala wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, alikarabati sehemu iliyofuatia.
10 El siguiente fue Jedaías, hijo de Harumap, que hizo reparaciones frente a su casa. El siguiente fue Hattush, hijo de Hasabneías.
Kupakana na sehemu hii, Yedaya mwana wa Harumafu alikarabati sehemu iliyokuwa mkabala na nyumba yake, naye Hatushi mwana wa Hashabnea akakarabati sehemu iliyofuatia.
11 Malquías, hijo de Harim, y Hasub, hijo de Pahat-moab, trabajaron en otra sección, así como en la Torre de los Hornos.
Malkiya mwana wa Harimu, na Hashubu mwana wa Pahath-Moabu walikarabati sehemu nyingine pamoja na Mnara wa Matanuru.
12 A continuación fue Salum, hijo de Halohes, gobernante de un medio distrito de Jerusalén, ayudado por sus hijas.
Shalumu mwana wa Haloheshi, mtawala wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, alikarabati sehemu iliyofuatia akisaidiwa na binti zake.
13 La Puerta del Valle fue reparada por Hanún y la gente que vivía en Zanoa. La reconstruyeron, colocaron sus puertas, junto con sus cerrojos y barras, y repararon mil codos de la muralla hasta la Puerta del Desecho.
Lango la Bondeni lilikarabatiwa na Hanuni na wakazi wa Zanoa. Walilijenga upya, na kuweka milango yake na makomeo na nondo mahali pake. Pia walikarabati ukuta wenye urefu wa mita 450 hadi Lango la Samadi.
14 Malquías, hijo de Recab, jefe del distrito de Bet-haquerem, reparó la Puerta de la Basura, la reconstruyó y colocó sus puertas, junto con sus cerrojos y barras.
Lango la Samadi lilikarabatiwa na Malkiya mwana wa Rekabu, mtawala wa wilaya ya Beth-Hakeremu. Alilijenga upya, na kuweka milango yake, na makomeo na nondo.
15 La Puerta de la Fuente fue reparada por Salún, hijo de Col-hoze, jefe del distrito de Mizpa. La reconstruyó, le puso un techo y levantó sus puertas, junto con sus cerrojos y barras. Reconstruyó el muro del estanque de Selá, junto al jardín del rey, hasta las escaleras que bajan de la ciudad de David.
Lango la Chemchemi lilikarabatiwa na Shalumu mwana wa Kolhoze, mtawala wa wilaya ya Mispa. Alilijenga upya, akaliezeka na kuweka milango yake, na makomeo na nondo mahali pake. Pia alikarabati ukuta wa Bwawa la Siloamu karibu na Bustani ya Mfalme, hadi kwenye ngazi zinazoshuka kutoka Mji wa Daudi.
16 Después de él, Nehemías, hijo de Azbuk, gobernante de un semidistrito de Bet-Zur, reparó hasta un punto frente al cementerio de David, hasta el estanque artificial y la Casa de los Guerreros Poderosos.
Baada yake, Nehemia mwana wa Azbuki, mtawala wa nusu ya wilaya ya Beth-Suri, alikarabati kufikia mkabala na makaburi ya Daudi, mpaka kwenye bwawa lililotengenezwa, na kufikia Nyumba ya Mashujaa.
17 A continuación estaban los levitas bajo el mando de Rehum hijo de Bani, y a continuación estaba Hasabías, gobernante de la mitad de la región de Keila, que hizo las reparaciones en nombre de su distrito.
Baada yake, ukarabati ulifanywa na Walawi chini ya uongozi wa Rehumu mwana wa Bani. Aliyefuatia ni Hashabia, mtawala wa nusu ya wilaya ya Keila, aliyekarabati sehemu ya wilaya yake.
18 Junto a ellos estaban sus vecinos bajo Binui, hijo de Henadad, gobernante de la otra mitad de la región de Keila.
Baada yake, ukarabati ulifanywa na ndugu zao chini ya usimamizi wa Binui mwana wa Henadadi, mtawala wa nusu hiyo ingine ya wilaya ya Keila.
19 El siguiente fue Ezer, hijo de Jesúa, gobernante de Mizpa, quien reparó otra sección frente a la Colina de la Armería, donde la muralla gira.
Baada yao, Ezeri mwana wa Yeshua, mtawala wa Mispa, alikarabati sehemu nyingine, kuanzia ile sehemu inayotazamana na mwinuko wa kuelekea kwenye ghala la kuhifadhia silaha, mpaka kwenye pembe ya ukuta.
20 El siguiente fue Baruc, hijo de Zabai, que trabajó duro reparando otra sección, desde donde la muralla gira hasta la entrada de la casa del sumo sacerdote Eliasib.
Baada yake, Baruku mwana wa Zakai alikarabati kwa bidii sehemu nyingine kuanzia ile pembe, mpaka kwenye lango la nyumba ya Eliashibu kuhani mkuu.
21 A continuación, Meremot, hijo de Urías, ton de Cos, que reparó otro tramo, desde la entrada de la casa del sumo sacerdote Eliasib hasta el final.
Kupakana naye, Meremothi mwana wa Uria, mwana wa Hakosi, alikarabati sehemu nyingine, kuanzia penye lango la nyumba ya Eliashibu mpaka mwisho wake.
22 A continuación, los sacerdotes de los alrededores hicieron las reparaciones.
Baada yake, ukarabati ulifanywa na makuhani waliotoka eneo lililouzunguka mji.
23 Después de ellos estaban Benjamín y Jasub, que hicieron reparaciones frente a su casa, y junto a ellos, Azarías, hijo de Maasías, hijo de Ananías, hizo reparaciones junto a su casa.
Baada yao Benyamini na Hashubu walikarabati mbele ya nyumba zao, na baada yao Azaria mwana wa Maaseya, mwana wa Anania alifanya ukarabati kando ya nyumba yake.
24 El siguiente fue Binui, hijo de Henadad, que reparó otra parte, desde la casa de Azarías hasta donde gira el muro y la esquina.
Baada yake, Binui mwana wa Henadadi alikarabati sehemu nyingine, kuanzia kwenye nyumba ya Azaria mpaka kwenye pembe ya ukuta.
25 Palal, hijo de Uzai, trabajó frente a donde gira el muro y la torre que se extiende desde el palacio superior, cerca del patio de la guardia. Luego estaban Pedaías, hijo de Paros
Naye Palali, mwana wa Uzai alijenga sehemu iliyokuwa mkabala na pembe ya ukuta, mpaka kwenye mnara wa juu ambao unajitokeza kuanzia kwenye jumba la kifalme, kando ya ua wa walinzi. Baada yake, Pedaya mwana wa Paroshi,
26 y los servidores del Templo que vivían en la colina de Ofel, quienes hacían reparaciones frente a la Puerta del Agua hacia el este y la torre que se extiende.
na watumishi wa Hekalu walioishi juu ya kilima cha Ofeli walikarabati hadi kufikia mkabala na Lango la Maji, kuelekea mashariki na ule mnara uliojitokeza.
27 A continuación estaban los tecoítas que repararon en otra sección frente a la gran torre que se extiende hasta la muralla de Ofel.
Baada yao, watu wa Tekoa walikarabati sehemu nyingine, kuanzia mnara mkubwa utokezao hadi ukuta wa Ofeli.
28 Encima de la Puerta de los Caballos, cada uno de los sacerdotes hizo reparaciones frente a su propia casa.
Makuhani walifanya ukarabati juu ya Lango la Farasi, kila mmoja mbele ya nyumba yake.
29 El siguiente era Sadoc, hijo de Imer, que trabajaba frente a su casa, y el siguiente era Semaías, hijo de Secanías, el guardia de la Puerta Oriental.
Baada yao, Sadoki mwana wa Imeri alifanya ukarabati mkabala na nyumba yake. Baada yake, Shemaya mwana wa Shekania, mlinzi wa Lango la Mashariki, alifanya ukarabati.
30 A continuación estaban Hananías, hijo de Selemías, y Hanún, sexto hijo de Zalaf, que se encargaba de la reparación. El siguiente fue Mesulam, hijo de Berequías, que hizo reparaciones frente a donde él vivía.
Baada yake, Hanania mwana wa Shelemia, na Hanuni mwana wa sita wa Salafu walikarabati sehemu nyingine. Baada yao, Meshulamu mwana wa Berekia alikarabati sehemu iliyokuwa mkabala na nyumba zake za kuishi.
31 El siguiente fue Malquías, uno de los orfebres, que hizo reparaciones hasta la casa de los sirvientes del Templo y de los mercaderes, frente a la Puerta de Inspección, y hasta la sala que está sobre la esquina.
Baada yake Malkiya, mmoja wa masonara, alifanya ukarabati mpaka kwenye nyumba za watumishi wa Hekalu na wafanyabiashara, mkabala na Lango la Ukaguzi, hadi kufikia chumba kilicho juu ya pembe.
32 Los orfebres y los mercaderes hicieron reparaciones entre la sala que está sobre la esquina y la Puerta de las Ovejas.
Masonara na wafanyabiashara walifanya ukarabati kutoka chumba kilichoko juu ya pembe hadi Lango la Kondoo.

< Nehemías 3 >