< Nehemías 12 >

1 Esta es la lista de los sacerdotes y levitas que volvieron con Zorobabel, hijo de Sealtiel, y Jesúa, el sumo sacerdote: Seraías, Jeremías, Esdras,
Hawa wafuatao walikuwa makuhani na Walawi ambao walirudi na Zerubabeli mwana wa Shealtieli pamoja na Yeshua: Seraya, Yeremia, Ezra,
2 Amarías, Maluc, Hatús,
Amaria, Maluki, Hatushi,
3 Secanías, Rehum, Meremot,
Shekania, Rehumu, Meremothi,
4 Iddo, Gineto, Abías,
Ido, Ginethoni, Abiya,
5 Miamín, Maadías, Bilga,
Miyamini, Moadia, Bilga,
6 Semaías, Joiarib, Jedaías,
Shemaya, Yoyaribu, Yedaya,
7 Salú, Amoc, Hilcías y Jedaías. Estos eran los líderes de los sacerdotes y sus parientes en el tiempo de Jesúa.
Salu, Amoki, Hilkia na Yedaya. Hawa walikuwa viongozi wa makuhani na wenzao wakati wa Yeshua.
8 Los levitas eran Jesúa, Binúi, Cadmiel, Serebías, Judá y Matanías, quien con sus compañeros levitas estaba a cargo de los cantos de alabanza.
Walawi walikuwa Yeshua, Binui, Kadmieli, Sherebia, Yuda, na pia Matania, ambaye pamoja na wenzake, alikuwa kiongozi wa nyimbo za shukrani.
9 Otros dos levitas, Bacbuquías y Uni, estaban frente a ellos en el servicio.
Bakbukia na Uni, wenzao, walisimama mkabala nao wakati wa ibada.
10 El sumo sacerdote Jesúa era el padre de Joiacim, que era el padre de Eliasib, que era el padre de Joiada,
Yeshua alikuwa baba wa Yoyakimu, Yoyakimu alikuwa baba wa Eliashibu, Eliashibu alikuwa baba wa Yoyada,
11 que era el padre de Jonatán, que era el padre de Jadúa.
Yoyada alikuwa baba wa Yonathani, na Yonathani alikuwa baba wa Yadua.
12 En tiempos de Joiacim, estos eran los jefes de familia de los sacerdotes de la familia de Seraías, Meraías; de la de Jeremías, Ananías;
Katika siku za Yoyakimu, kulikuwa na wakuu wa jamaa za kikuhani: wa jamaa ya Seraya, Meraya; wa jamaa ya Yeremia, Hanania;
13 de la de Esdras, Mesulam; de la de Amarías, Johanán;
wa jamaa ya Ezra, Meshulamu; wa jamaa ya Amaria, Yehohanani;
14 de la de Maluci, Jonatán; de la de Sebanías, José;
wa jamaa ya Maluki, Yonathani; wa jamaa ya Shebania, Yosefu;
15 de la de Harim, Adna; de la de Meraiot, Helcai;
wa jamaa ya Harimu, Adna; wa jamaa ya Meremothi, Helkai;
16 de la de Iddo, Zacarías; de la de Gineto, Mesulam
wa jamaa ya Ido, Zekaria; wa jamaa ya Ginethoni, Meshulamu;
17 de Abías, Zicri; de Miiamín y de Maadías, Piltai;
wa jamaa ya Abiya, Zikri; wa jamaa ya Miniamini na ya Maazia, Piltai;
18 de Bilga, Samúa; de Semaías, Jonatán;
wa jamaa ya Bilgai, Shamua; wa jamaa ya Shemaya, Yehonathani;
19 de Joiarib, Matenai; de Jedaías, Uzi;
wa jamaa ya Yoyaribu, Matenai; wa jamaa ya Yedaya, Uzi;
20 de Salai, Calai; de Amoc, Eber;
wa jamaa ya Salu, Kalai; wa jamaa ya Amoki, Eberi;
21 de Hicíash, Hasabías; de Jedaías, Natanael.
wa jamaa ya Hilkia, Hashabia; wa jamaa ya Yedaya, Nethaneli.
22 Los jefes de familia de los levitas en la época de Eliasib, Joiada, Johanán y Jaddua, además de los de los sacerdotes, fueron registrados durante el reinado de Darío el Persa.
Wakuu wa jamaa za Walawi katika siku za Eliashibu, Yoyada, Yohanani na Yadua, pia wale jamaa za makuhani, waliandikishwa wakati wa utawala wa Dario, Mwajemi.
23 En cuanto a la genealogía de los hijos de Leví, los jefes de familia hasta la época de Johanán, hijo de Eliasib, fueron inscritos en el Libro de los Registros.
Wakuu wa jamaa miongoni mwa wazao wa Lawi hadi wakati wa Yohanani mwana wa Eliashibu waliandikishwa katika kitabu cha kumbukumbu.
24 Los jefes de los levitas eran Hasabías, Serebías y Jesúa, hijo de Cadmiel, junto con sus compañeros levitas, que estaban de pie frente a ellos, cada sección dando alabanzas y agradecimientos y respondiendo unos a otros, según lo dispuesto por David, el hombre de Dios.
Viongozi wa Walawi walikuwa: Hashabia, Sherebia, Yeshua mwana wa Kadmieli na wenzao, waliosimama mkabala nao kusifu na kushukuru, sehemu moja ikipokezana na nyingine kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu.
25 Se les unieron Matanías, Bacbucías y Abdías. Mesulam, Talmón y Acub eran guardianes de los almacenes de las puertas.
Mabawabu waliokuwa wakilinda kwenye malango ya ghala ni: Matania, Bakbukia, Obadia, Meshulamu, Talmoni na Akubu.
26 Sirvieron en tiempos de Joiaquim, hijo de Jesúa, hijo de Josadac, y en tiempos del gobernador Nehemías y del sacerdote y escriba Esdras.
Walihudumu siku za Yoyakimu mwana wa Yeshua, mwana wa Yosadaki, na katika siku za mtawala Nehemia, na za Ezra kuhani na mwandishi.
27 Para dedicar el muro de Jerusalén, se llamó a los levitas de todos los lugares donde vivían para que vinieran a Jerusalén y celebraran con alegría la dedicación con cantos de alabanza y agradecimiento, acompañados de címbalos, arpas y liras.
Wakati wa kuwekwa wakfu ukuta wa Yerusalemu, Walawi walitafutwa kule walikokuwa wakiishi, nao wakaletwa Yerusalemu kuadhimisha kwa shangwe huko kuweka wakfu kwa nyimbo za shukrani na kwa uimbaji wakitumia matoazi, vinubi na zeze.
28 También trajeron a los cantores de los alrededores de Jerusalén y de las aldeas de los netofatitas,
Pia waimbaji walikusanywa pamoja kutoka maeneo yaliyozunguka Yerusalemu, kutoka vijiji vya Wanetofathi,
29 así como de Bet-gilgal y de la zona de Geba y Azmavet, pues los cantores se habían construido aldeas alrededor de Jerusalén.
kutoka Beth-Gilgali, na kutoka eneo la Geba na Azmawethi, kwa kuwa waimbaji walikuwa wamejijengea vijiji kuzunguka Yerusalemu.
30 Una vez que los sacerdotes y los levitas se purificaron, purificaron el pueblo, las puertas y la muralla.
Wakati makuhani na Walawi walipokuwa wamekwisha kujitakasa kwa kufuatana na desturi, waliwatakasa watu, malango na ukuta.
31 Hice que los jefes de Judá subieran a la muralla y dispuse dos grandes coros para dar gracias. Un grupo se dirigió a la derecha de la muralla, hasta la Puerta del Desecho.
Niliwaagiza viongozi wa Yuda wapande juu ya ukuta. Pia niliagiza makundi mawili makubwa ya waimbaji waimbe nyimbo za kumshukuru Mungu. Kundi moja lilipanda juu ya ukuta upande wa kuume, kuelekea Lango la Samadi.
32 Los siguieron Oseas y la mitad de los dirigentes de Judá,
Hoshaya na nusu ya viongozi wa Yuda wakawafuata,
33 con Azarías, Esdras, Mesulam,
pamoja na Azaria, Ezra, Meshulamu,
34 Judá, Benjamín, Semaías y Jeremías,
Yuda, Benyamini, Shemaya, Yeremia,
35 así como algunos de los sacerdotes con trompetas, y Zacarías, hijo de Jonatán, hijo de Semaías hijo de Matanías, hijo de Micaías, hijo de Zaccur, hijo de Asaf,
pamoja na baadhi ya makuhani wenye tarumbeta, na pia walikuwa na Zekaria mwana wa Yonathani, mwana wa Shemaya, mwana wa Matania, mwana wa Mikaya, mwana wa Zakuri, mwana wa Asafu,
36 y sus compañeros sacerdotes, Semaías, Azarel, Milalai, Gilalai, Maai, Netanel, Judá y Hanani, junto con los instrumentos musicales, tal como lo exigió David, el hombre de Dios. El escriba Esdras los dirigía.
pamoja na wenzake, Shemaya, Azareli, Milalai, Gilalai, Maai, Nethaneli, Yuda na Hanani, wakiwa na vyombo vya uimbaji, kama ilivyoagizwa na Daudi mtu wa Mungu. Mwandishi Ezra aliongoza maandamano.
37 En la Puerta de la Fuente se dirigieron hacia arriba por la escalera de la ciudad de David, donde la muralla sube, por encima de la casa de David, y hacia la Puerta del Agua, al este.
Kwenye Lango la Chemchemi waliendelea moja kwa moja mpaka kwenye ngazi za Mji wa Daudi, kwenye mwinuko wa ukuta, na kupitia juu ya nyumba ya Daudi mpaka kwenye Lango la Maji upande wa mashariki.
38 El otro grupo del coro fue en dirección contraria. Los seguí, junto con la mitad del pueblo, por la muralla, pasando por la Torre de los Hornos, hasta la Muralla Ancha,
Kundi la pili la waimbaji lilielekea upande wa kushoto. Niliwafuata juu ya ukuta, pamoja na nusu ya watu kupitia Mnara wa Tanuru mpaka kwenye Ukuta Mpana,
39 por la Puerta de Efraín, la Puerta de Jesana, la Puerta del Pescado, la Torre de Hananel y la Torre de los Cien, hasta la Puerta de las Ovejas, deteniéndose en la Puerta de la Guardia.
juu ya Lango la Efraimu, Lango la Yeshana, Lango la Samaki, Mnara wa Hananeli, na Mnara wa Mia, mpaka kwenye Lango la Kondoo. Walipofika kwenye Lango la Ulinzi wakasimama.
40 Los dos coros de acción de gracias ocuparon entonces su lugar en el Templo de Dios. Yo seguí con el grupo de líderes que me acompañaba,
Kisha yale makundi mawili ya waimbaji yaliyoshukuru yakachukua nafasi zao katika nyumba ya Mungu. Nami pia nikafanya hivyo, pamoja na nusu ya maafisa,
41 junto con los sacerdotes que tocaban sus trompetas: Eliaquim, Maasías, Miniamin, Micaías, Elioenai, Zacarías y Ananías.
na makuhani wafuatao: Eliakimu, Maaseya, Miniamini, Mikaya, Elioenai, Zekaria na Hanania wakiwa na tarumbeta zao,
42 Luego vinieron los cantores Maasías, Semaías, Eleazar, Uzzi, Johanán, Malquías, Elam y Ezer, y los coros cantaron, dirigidos por Izrahías.
na pia Maaseya, Shemaya, Eleazari, Uzi, Yehohanani, Malkiya, Elamu na Ezeri. Makundi haya yaliimba chini ya uongozi wa Yezrahia.
43 Ese día se ofrecieron muchos sacrificios, celebrando que Dios les había traído tanta felicidad, una felicidad tremenda. Las mujeres y los niños también celebraron, y los sonidos de alegría en Jerusalén se podían escuchar a lo lejos.
Siku hiyo watu walitoa dhabihu nyingi, wakishangilia kwa sababu Mungu aliwapa furaha kuu. Wanawake na watoto walishangilia pia. Sauti ya kushangilia huko Yerusalemu iliweza kusikika mbali sana.
44 Ese mismo día se pusieron hombres a cargo de los almacenes que contenían las ofrendas, la primera parte de las cosechas y los diezmos. Lo que la Ley asignaba a los sacerdotes y a los levitas se llevaba a estos almacenes desde los campos de los alrededores de las ciudades, porque todo el pueblo de Judá se alegraba por el servicio de los sacerdotes y de los levitas.
Wakati huo watu walichaguliwa kuwa wasimamizi wa vyumba vya ghala kwa ajili ya matoleo, malimbuko na zaka. Kutoka kwenye yale mashamba yaliyozunguka miji walipaswa walete kwenye ghala mafungu kama sheria ilivyoamuru kwa ajili ya makuhani na Walawi, kwa kuwa Yuda alifurahishwa na huduma ya makuhani na Walawi.
45 Ellos eran responsables del culto a su Dios y del servicio de purificación, junto con los cantores y los porteros, siguiendo las instrucciones de David y de su hijo Salomón.
Walifanya ibada ya Mungu wao na ibada ya utakaso, nao waimbaji na walinzi wa lango wakafanya hivyo pia, kufuatana na amri za Daudi na Solomoni mwanawe.
46 Porque hace mucho tiempo, en tiempos de David y de Asaf, se habían designado directores para los cantores y para los cantos de alabanza y de agradecimiento a Dios.
Muda mrefu uliopita, katika siku za Daudi na Asafu, walikuwepo viongozi wa waimbaji na wa nyimbo za sifa na za kumshukuru Mungu.
47 Así que en el tiempo de Zorobabel y de Nehemías, todos en Israel proveían las dietas para los cantores y los porteros. También se aseguraban de proveer para los otros levitas, y los levitas daban una parte de esto a los descendientes de Aarón.
Kwa hiyo katika siku za Zerubabeli na za Nehemia, Israeli wote walitoa mafungu kila siku kwa ajili ya waimbaji na mabawabu. Pia walitenga fungu kwa ajili ya Walawi wengine, nao Walawi walitenga fungu kwa ajili ya wazao wa Aroni.

< Nehemías 12 >