< Levítico 14 >

1 El Señor le dijo a Moisés,
Bwana akamwambia Mose,
2 “Estas son las normas relativas a los que han tenido una enfermedad de la piel cuando se declaran limpios habiendo sido llevados al sacerdote.
“Haya ndiyo masharti yamhusuyo mtu mgonjwa wakati wa kufanyiwa ibada ya utakaso wakati aletwapo kwa kuhani:
3 El sacerdote debe salir del campamento e inspeccionar a la persona. Si la enfermedad de la piel se ha curado,
Kuhani atakwenda kumchunguza nje ya kambi. Kama mtu huyo atakuwa amepona ugonjwa wake wa ngozi wa kuambukiza,
4 el sacerdote hará que le traigan dos pájaros ceremoniales limpios, también algo de madera de cedro, hilo carmesí e hisopo, en nombre de la persona que se va a limpiar.
kuhani ataagiza vitu vifuatavyo viletwe kwa ajili ya mtu atakayetakaswa: ndege wawili safi walio hai, mti wa mwerezi, kitani nyekundu, na hisopo.
5 “El sacerdote ordenará que se mate a uno de los pájaros sobre una vasija de arcilla llena de agua fresca.
Kisha kuhani ataagiza kwamba mmoja wa ndege wale achinjwe kwenye chungu chenye maji safi.
6 Tomarás el pájaro vivo junto con la madera de cedro, el hilo carmesí y el hisopo, y los mojará en la sangre del pájaro que fue matado sobre el agua fresca.
Kisha kuhani atamchukua ndege aliye hai na kumtumbukiza pamoja na mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo ndani ya damu ya yule ndege aliyechinjiwa kwenye maji safi.
7 Usará la sangre para rociar siete veces a la persona que está siendo limpiada de la enfermedad de la piel. Luego el sacerdote los declarará limpios y dejará que el pájaro vivo se vaya volando.
Atamnyunyizia yule mwenye ugonjwa wa kuambukiza maji hayo mara saba, na kumtangaza kuwa safi. Kisha atamwachia yule ndege aliye hai aende zake kwenye mashamba.
8 “El que se limpia debe lavar su ropa, afeitarse todo el pelo y lavarse con agua; entonces se limpiará ceremonialmente. Después de eso pueden entrar en el campamento, pero deben permanecer fuera de su tienda durante siete días.
“Huyo mtu atakayetakaswa ni lazima afue nguo zake, anyoe nywele zake zote, na aoge kwa maji; ndipo atakapokuwa safi kwa desturi ya ibada. Baada ya hili anaweza kuingia kambini, lakini ni lazima akae nje ya hema lake kwa siku saba.
9 El séptimo día se afeitarán todo el pelo: la cabeza, la barba, las cejas y el resto del cabello. Deben lavar su ropa y lavarse con agua, y estarán limpios.
Siku ya saba ni lazima anyoe nywele zake zote; yaani anyoe nywele za kichwa, ndevu zake, kope zake na nywele nyingine zote. Ni lazima afue nguo zake, na aoge kwa maji, naye atakuwa safi.
10 “El octavo día traerán dos corderos machos y una hembra, todos de un año de edad y sin defectos; una ofrenda de grano que consiste en tres décimos de una efa de la mejor harina mezclada con aceite de oliva, y un ‘tronco’ de aceite de oliva.
“Siku ya nane, ni lazima alete kondoo dume wawili na kondoo jike mmoja, wote wa mwaka mmoja na wasio na dosari, pamoja na sehemu tatu za kumi za efa za unga laini uliochanganywa na mafuta, kwa ajili ya sadaka ya nafaka, na logi moja ya mafuta.
11 El sacerdote que dirige la ceremonia presentará al Señor la persona a ser limpiada, junto con estas ofrendas, a la entrada del Tabernáculo de Reunión.
Kuhani atakayemtangaza kuwa safi atahitaji kumkabidhi mgonjwa aliyepona pamoja na sadaka zake zote mbele za Bwana katika ingilio la Hema la Kukutania.
12 El sacerdote tomará uno de los corderos machos y lo presentará como ofrenda por la culpa, junto con el tronco de aceite de oliva; y lo agitará ante el Señor como ofrenda mecida.
“Kisha kuhani atamchukua mmoja wa wale kondoo dume na kumtoa kuwa sadaka ya hatia, pamoja na ile logi moja ya mafuta; ataviinua mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
13 “Luego degollará el cordero cerca del santuario donde se degüella la ofrenda por el pecado y el holocausto. La ofrenda por el pecado y la ofrenda por la culpa pertenecen al sacerdote; es muy sagrada.
Atamchinja huyo kondoo katika mahali patakatifu ambapo sadaka ya dhambi na ile ya kuteketezwa huchinjiwa. Kama ilivyo sadaka ya dhambi, sadaka ya hatia ni ya kuhani; nayo ni takatifu sana.
14 El sacerdote pondrá parte de la sangre de la ofrenda por la culpa en el lóbulo de la oreja derecha, en el pulgar derecho y en el dedo gordo del pie derecho de la persona que se está limpiando.
Kuhani atachukua sehemu ya damu ya sadaka ya hatia na kuitia kwenye ncha ya sikio la kuume la yule atakayetakaswa, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
15 El sacerdote echará un poco del tronco de aceite de oliva en su palma izquierda,
Kuhani atachukua sehemu ya ile logi ya mafuta, ayamimine kwenye kiganja cha mkono wake mwenyewe wa kushoto,
16 mojará su dedo índice derecho en él, y con su dedo rociará un poco de aceite de oliva siete veces ante el Señor.
na achovye kidole chake cha shahada cha mkono wake wa kuume kwenye mafuta yaliyoko kwenye kiganja chake, na kwa kidole hicho anyunyize mafuta hayo mara saba mbele za Bwana.
17 El sacerdote usará entonces parte del resto del aceite de oliva que queda en su palma sobre la persona que se está limpiando, y lo pondrá sobre la sangre de la ofrenda de culpa. Esto estará en el lóbulo de su oreja derecha, en su pulgar derecho y en el dedo gordo de su pie derecho, sobre la sangre de la ofrenda de culpa.
Kuhani atampaka yule anayetakaswa sehemu ya mafuta yaliyobaki kiganjani kwenye ncha ya sikio lake la kuume, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume, mahali palepale alipompaka damu ya sadaka ya kuondoa hatia.
18 Lo que quede del aceite de oliva en su palma, el sacerdote lo pondrá sobre la cabeza de la persona que se está limpiando y luego lo hará justo ante el Señor.
Kuhani atayapaka mafuta yaliyobaki kwenye kiganja chake juu ya kichwa cha yule anayetakaswa, na kufanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana.
19 El sacerdote sacrificará la ofrenda por el pecado para hacer a la persona correcta, de modo que ahora esté limpia de su impureza. Después de eso, el sacerdote matará el holocausto
“Kisha kuhani atatoa dhabihu ya sadaka ya dhambi na kufanya upatanisho kwa ajili ya yule atakayetakaswa kutoka unajisi wake. Baada ya hayo, kuhani atachinja sadaka ya kuteketezwa
20 y lo ofrecerá en el altar, junto con la ofrenda de grano, para enderezarlos, y estarán limpios.
na kuitoa juu ya madhabahu, pamoja na sadaka ya nafaka ili kumfanyia upatanisho, naye atakuwa safi.
21 “Pero los que son pobres y no pueden pagar estas ofrendas deben traer un cordero macho como ofrenda de culpa para ser agitado para hacerlos rectos, junto con una décima parte de la mejor harina mezclada con aceite de oliva para una ofrenda de grano, un tronco de aceite de oliva,
“Hata hivyo, kama ni maskini na hawezi kupata vitu hivi, lazima achukue mwana-kondoo mmoja kama sadaka ya hatia ipate kuinuliwa ili kumfanyia upatanisho, pamoja na sehemu ya kumi ya efa ya unga laini uliochanganywa na logi moja ya mafuta kwa ajili ya sadaka ya nafaka,
22 y dos tórtolas o dos pichones de paloma, lo que puedan pagar. Una se usará como ofrenda por el pecado y la otra como holocausto.
na hua wawili au makinda mawili ya njiwa, kile atakachoweza kupata, mmoja kwa sadaka ya dhambi, na mwingine kwa sadaka ya kuteketezwa.
23 “Al octavo día deben llevarlos al sacerdote a la entrada del Tabernáculo de Reunión ante el Señor para que los limpie.
“Katika siku ya nane, lazima avilete vitu hivyo kwa kuhani, kwa ajili ya kutakaswa kwake kwenye ingilio la Hema la Kukutania mbele za Bwana.
24 El sacerdote tomará el cordero para la ofrenda por la culpa, junto con el tronco de aceite de oliva, y los agitará como ofrenda mecida ante el Señor.
Kuhani atamchukua mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya hatia, pamoja na ile logi ya mafuta ya kuinuliwa mbele za Bwana kuwa sadaka ya kuinuliwa.
25 Después de matar el cordero para la ofrenda por la culpa, el sacerdote tomará un poco de la sangre de la ofrenda por la culpa y la pondrá en el lóbulo de la oreja derecha del que se está limpiando, en el pulgar derecho y en el dedo gordo del pie derecho.
Atamchinja huyo mwana-kondoo kwa ajili ya sadaka ya hatia. Pia ataichukua sehemu ya damu yake na kuipaka kwenye ncha ya sikio la kuume la yule anayetakaswa, na aipake pia kwenye kidole gumba cha mkono wa kuume wa huyo mtu, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
26 “Entonces el sacerdote verterá un poco de aceite de oliva en su palma izquierda
Kuhani atamiminia sehemu ya mafuta kwenye kiganja chake cha mkono wa kushoto,
27 y con su dedo índice derecho, rociará un poco de aceite de su palma izquierda siete veces ante el Señor.
na kwa kidole chake cha shahada cha mkono wa kuume, atamnyunyizia yule anayetakaswa yale mafuta yaliyo kwenye kiganja chake mara saba mbele za Bwana.
28 El sacerdote pondrá también un poco de aceite de oliva en su palma, en el lóbulo de la oreja derecha de la persona que se está limpiando, en el pulgar derecho y en el dedo gordo del pie derecho, en los mismos lugares que la sangre de la ofrenda de culpa.
Atampaka mafuta yaliyobaki kwenye kiganja chake katika sehemu zote, kama alivyompaka damu ya sadaka ya hatia: yaani, kwenye ncha ya sikio la kuume la yule anayetakaswa, kwenye kidole gumba cha mkono wake wa kuume, na kidole kikubwa cha mguu wake wa kuume.
29 Lo que quede del aceite de oliva en su palma, el sacerdote lo pondrá en la cabeza de la persona que se está limpiando y luego lo pondrá delante del Señor.
Kuhani atayapaka mafuta yaliyobaki katika kiganja chake kwenye kichwa cha yule anayetakaswa, na kufanya upatanisho kwa ajili yake mbele za Bwana.
30 Luego deberán sacrificar una de las tórtolas o palomas jóvenes, según sus posibilidades,
Kisha atatoa dhabihu wale hua ama yale makinda ya njiwa ambayo mtu ataweza kuwapata,
31 una como ofrenda por el pecado y la otra como holocausto, junto con la ofrenda de grano. Así es como el sacerdote hará a la persona correcta y limpia ante el Señor.
mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi, na mwingine kuwa sadaka ya kuteketezwa, pamoja na sadaka ya nafaka. Kwa njia hii kuhani atafanya upatanisho mbele za Bwana kwa ajili ya yule anayetakaswa.”
32 Estas son las normas para aquellos que tienen una enfermedad de la piel y no pueden permitirse las ofrendas habituales para hacer a la gente limpia”.
Haya ndiyo masharti kwa mtu yeyote mwenye ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, na ambaye hana uwezo wa kutoa sadaka za kawaida kwa ajili ya kutakaswa kwake.
33 Entonces el Señor les dijo a Moisés y a Aarón:
Bwana akawaambia Mose na Aroni,
34 “Cuando lleguen a Canaán, la tierra que yo les doy, si pongo un poco de moho en una casa y la contamino,
“Mtakapoingia katika nchi ya Kanaani ambayo ninawapa kuwa milki yenu, nami nikaweka upele ueneao kwenye nyumba katika nchi ile,
35 el dueño de la casa debe venir y decirle al sacerdote: ‘Parece que mi casa tiene moho’.
ni lazima mwenye nyumba hiyo akamwambie kuhani, ‘Nimeona kitu fulani kinachofanana na upele kwenye nyumba yangu.’
36 El sacerdote debe ordenar que se vacíe la casa antes de entrar a inspeccionar el moho, para que nada en la casa sea declarado impuro. Una vez hecho esto, el sacerdote debe entrar e inspeccionar la casa.
Kuhani ataagiza vitu vyote vitolewe ndani ya nyumba, kabla hajaenda kuchunguza kama ina ugonjwa huo, ili kitu chochote ndani ya nyumba kisitangazwe kuwa najisi. Baada ya hili, kuhani ataingia ndani na kuikagua hiyo nyumba.
37 Examinará la casa y verá si el moho de las paredes está hecho de hendiduras verdes o rojas que van bajo la superficie,
Atachunguza upele huo katika kuta za nyumba hiyo, nazo kama zina rangi ya kijani kibichi au wekundu, na kuna mibonyeo ndani ya ukuta,
38 el sacerdote saldrá a la puerta y sellará la casa durante siete días.
kuhani atatoka na kufunga mlango wa nyumba hiyo kwa siku saba.
39 Al séptimo día el sacerdote volverá e inspeccionará la casa de nuevo. Si el moho se ha extendido en las paredes,
Siku ya saba, kuhani atarudi kuikagua nyumba. Kama upele umeenea juu ya kuta,
40 ordenará que las piedras afectadas se retiren y se eliminen en un área impura fuera de la ciudad.
ataagiza kwamba mawe yote yaliyoambukizwa yaondolewe na kutupwa katika eneo lililo najisi nje ya mji.
41 Luego ordenará que todo el yeso del interior de la casa sea raspado y arrojado en una zona impura fuera de la ciudad.
Kuta zote za ndani ya nyumba hiyo ni lazima zikwanguliwe, na kifusi chake kitupwe mahali najisi nje ya mji.
42 Se deben usar diferentes piedras para reemplazar las que se han quitado, y se necesitará un nuevo yeso para volver a enlucir la casa.
Kisha watachukua mawe mengine na kujenga palipobomolewa kwa udongo mpya wa mfinyanzi, na kuipiga nyumba hiyo lipu mpya.
43 Si el moho vuelve y afecta de nuevo a la casa, incluso después de haber quitado las piedras y de haber raspado y vuelto a enlucir la casa,
“Ikiwa upele huo utatokea tena ndani ya ile nyumba baada ya mawe kuondolewa na nyumba kukwanguliwa na kuwekwa lipu mpya,
44 el sacerdote debe venir a inspeccionarla. Si ve que el moho se ha extendido en la casa, es un moho dañino; la casa está sucia.
kuhani atakwenda kuikagua, na kama upele umeenea ndani ya nyumba, basi ni upele uharibuo; nyumba hiyo ni najisi.
45 Debe ser demolida, y todas sus piedras, maderas y yeso deben ser tomadas y arrojadas en un área impura fuera de la ciudad.
Ni lazima ibomolewe: mawe yake, mbao na lipu yake, vyote vikatupwe nje ya mji mahali palipo najisi.
46 Cualquiera que entre en la casa durante cualquier tiempo que esté sellada será impuro hasta la noche.
“Yeyote atakayeingia katika nyumba hiyo ikiwa imefungwa, atakuwa najisi mpaka jioni.
47 Quien duerma o coma en la casa debe lavar su ropa.
Yeyote atakayelala au kula ndani ya nyumba hiyo ni lazima afue nguo zake.
48 “Sin embargo, si cuando el sacerdote venga a inspeccionarla y encuentra que el moho no ha reaparecido después de que la casa haya sido tapizada, declarará la casa limpia porque el moho ha desaparecido.
“Lakini ikiwa kuhani atakuja kuikagua na kukuta kuwa upele haujaenea tena baada ya nyumba kupigwa lipu, ataitangaza nyumba ile kuwa safi, kwa sababu upele umekwisha.
49 Traerá dos pájaros, madera de cedro, hilo carmesí e hisopo para limpiar la casa.
Ili kuitakasa nyumba hiyo, mwenye nyumba ataleta ndege wawili, mti wa mwerezi, kitani nyekundu na hisopo.
50 Matará a uno de los pájaros sobre una vasija de arcilla llena de agua fresca.
Atamchinja mmoja wa wale ndege kwenye chungu chenye maji safi.
51 Sumergirá el pájaro vivo, la madera de cedro, el hilo carmesí y el hisopo en la sangre del pájaro muerto y en el agua fresca, y rociará la casa siete veces.
Kisha atachukua mti wa mwerezi, hisopo, kitani nyekundu na ndege aliye hai, na kuvitumbukiza ndani ya damu ya ndege aliyechinjwa pamoja na maji safi, na kuinyunyizia nyumba ile mara saba.
52 Limpiará la casa con la sangre del pájaro, el agua fresca, el pájaro vivo, la madera de cedro, el hisopo y el hilo carmesí.
Ataitakasa nyumba kwa damu ya yule ndege, maji safi, ndege aliye hai, mti wa mwerezi, hisopo na kitani nyekundu.
53 Luego dejará que el pájaro vivo se vaya volando fuera de la ciudad. Así es como hará la casa bien, y estará limpia.
Kisha atamwachia yule ndege aliye hai huru mashambani nje ya mji. Kwa njia hii atafanya upatanisho kwa ajili ya nyumba ile, nayo itakuwa safi.”
54 “Estas son las regulaciones para cualquier enfermedad infecciosa de la piel, para una infección de costra,
Haya ndiyo masharti kuhusu aina yoyote ya ugonjwa wa ngozi wa kuambukiza, mwasho wowote,
55 para el moho en la ropa y en una casa,
upele ndani ya nguo au ndani ya nyumba,
56 así como para una hinchazón, sarpullido o mancha.
kwa uvimbe, vipele au kipaku kingʼaacho,
57 Se utilizan para decidir si algo está limpio o sucio. Estas son las normas relativas a las enfermedades de la piel y el moho”.
kupambanua wakati kitu fulani ni safi au najisi. Haya ndiyo masharti kuhusu magonjwa ya ngozi ya kuambukiza na upele.

< Levítico 14 >