< Jueces 12 >

1 Entonces los efraimitas fueron convocados y cruzaron el Jordán hasta Zafón. Le dijeron a Jefté: “¿Por qué fuiste a luchar contra los amonitas sin convocarnos para que fuéramos contigo? Vamos a quemar tu casa contigo dentro”.
Watu wa Efraimu wakaita majeshi yao, wakavuka kwenda Zafoni, wakamwambia Yefta, “Kwa nini mmekwenda kupigana na Waamoni bila kutuita ili twende pamoja nawe? Basi tutaichoma moto nyumba yako, pamoja nawe ukiwa ndani yake.”
2 “Yo era un hombre responsable de una gran lucha”, respondió Jefté. “Yo y mi pueblo estábamos luchando contra los amonitas. Cuando te pedí ayuda, no vinieron a salvarme de ellos.
Yefta akajibu, “Mimi na watu wangu tulikuwa na ugomvi mkubwa na Waamoni, hata ingawa niliwaita hamkuniokoa katika mkono wao.
3 Cuando me di cuenta de que no iban a ayudarme, me hice cargo de mi propia vida y fui a luchar contra los amonitas, y el Señor me hizo victorioso sobre ellos. Entonces, ¿por qué han venido hoy a atacarme?”.
Nilipoona kuwa hamkunipa msaada nikauhatarisha uhai wangu na nikavuka kupigana na Waamoni. Naye Bwana akanipatia ushindi dhidi yao. Sasa kwa nini mnanijia leo ili kupigana nami?”
4 Jefté convocó a todos los hombres de Galaad y luchó contra los efraimitas. Los hombres de Galaad los mataron porque los efraimitas se burlaban de ellos, diciendo: “Ustedes los galaaditas no son más que fugitivos que viven entre Efraín y Manasés”.
Ndipo Yefta akakusanya watu wa Gileadi pamoja na kupigana na Efraimu. Wagileadi wakawashinda Efraimu, kwa kuwa Waefraimu walisema, “Ninyi Wagileadi ni watoro mliotoroka toka Efraimu na Manase.”
5 Los galaaditas tomaron el control de los vados sobre el río Jordán que conducían al territorio de Efraín, y cuando un efraimita que escapaba de la batalla venía y pedía: “Déjenme cruzar”, los galaaditas le preguntaban: “¿Eres efraimita?”; si respondían “No”,
Wagileadi wakaviteka vivuko vya Yordani dhidi ya hao Waefraimu, kisha ilikuwa yeyote yule aliyenusurika katika Efraimu aliposema, “Niache nivuke,” hao watu wa Gileadi walimuuliza, “Je wewe ni Mwefraimu?” Kama alijibu “Hapana,”
6 le decían: “Di Shibboleth”. Y los que eran de Efraín, dirían“Sibboleth” porque ellos no podían pronunciarlo bien, y así los agarrarían y los matarían allí en los vados del Jordán. Un total de 42.000 fueron asesinados en esa ocasión.
walimwambia, “Sawa, sema ‘Shibolethi.’” Iwapo alitamka, “Sibolethi,” kwa sababu hakuweza kutamka hilo neno sawasawa, walimkamata na kumuua hapo kwenye vivuko vya Yordani. Waefraimu 42,000 waliuawa wakati huo.
7 Jefté dirigió a Israel como juez durante seis años. Luego murió y fue enterrado en una de las ciudades de Galaad.
Yefta akawa mwamuzi wa Waisraeli kwa muda wa miaka sita. Basi Yefta akafa, akazikwa katika mmojawapo wa miji ya Gileadi.
8 Después de Jefté, Ibzán de Belén dirigió a Israel como juez.
Baada yake, Ibzani wa Bethlehemu akawa mwamuzi wa Israeli.
9 Tuvo treinta hijos y treinta hijas. Casó a sus hijas con hombres de otras tribus, y trajo a treinta esposas de otras tribus para que se casaran con sus hijos. Ibzán dirigió a Israel como juez durante siete años.
Alikuwa na wana thelathini na binti thelathini. Akawaoza binti zake kwa watu wengine nje ya ukoo wake, na kuwatwalia wanawe wanawake thelathini toka nje ya ukoo wake. Ibzani akawa mwamuzi wa Israeli kwa muda wa miaka saba.
10 Luego Ibzán murió y fue enterrado en Belén.
Ibzani akafa, akazikwa huko Bethlehemu.
11 Después de él, Elón de Zabulón dirigió a Israel como juez durante diez años.
Baada yake Eloni, Mzabuloni, akawa mwamuzi wa Israeli, naye akawaamua kwa muda wa miaka kumi.
12 Luego murió y fue enterrado en Ajalón, en el territorio de Zabulón.
Kisha Eloni akafa, akazikwa katika Aiyaloni, katika nchi ya Zabuloni.
13 Después de él, Abdón, hijo de Hilel, de Piratón, dirigió a Israel como juez.
Baada yake, Abdoni mwana wa Hileli, Mpirathoni, akawa mwamuzi wa Israeli.
14 Tuvo cuarenta hijos y treinta nietos, que montaban setenta asnos. Dirigió a Israel como juez durante ocho años.
Naye akazaa wana arobaini na wana wa wanawe thelathini waliopanda punda sabini. Akawa mwamuzi wa Israeli kwa muda wa miaka minane.
15 Luego murió y fue enterrado en Piratón, en el territorio de Efraín, en la región montañosa de los amalecitas.
Ndipo Abdoni mwana wa Hileli, Mpirathoni, akafa, naye akazikwa huko Pirathoni katika Efraimu, katika nchi ya vilima ya Waamaleki.

< Jueces 12 >