< Josué 12 >
1 Estos son los reyes que los israelitas derrotaron cuando tomaron posesión de su tierra al este del Jordán, desde el valle de Arnón en el sur hasta el monte Hermón en el norte, incluyendo toda la tierra del lado oriental del Jordán.
Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Waisraeli waliwashinda na kuitwaa nchi yao upande wa mashariki mwa Yordani, kuanzia Bonde la Arnoni mpaka Mlima Hermoni, pamoja na eneo lote la upande wa mashariki ya Araba:
2 Sehón, rey de los amorreos, que vivía en Hesbón, gobernaba desde Aroer, en el borde del valle de Arnón, todo el camino desde la mitad del valle hasta el río Jaboc, la frontera con los amonitas (e incluía la mitad de Galaad).
Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye alitawala huko Heshboni. Alitawala kuanzia Aroeri kwenye ukingo wa Bonde la Arnoni, kuanzia katikati ya bonde, hadi kwenye Mto Yaboki, ambao ni mpaka wa Waamoni. Hii ilijumlisha nusu ya Gileadi.
3 Su territorio también incluía el valle del Jordán hasta el mar de Cineret y la tierra al este, y todo el camino hasta el Mar Salado, al este hacia Beth-jeshimoth y al sur hasta las laderas de Pisga.
Pia alitawala Araba ya mashariki kuanzia Bahari ya Kinerethi hadi Bahari ya Araba (yaani Bahari ya Chumvi), hadi Beth-Yeshimothi, kisha kuelekea kusini chini ya materemko ya Pisga.
4 El rey Og de Basán, uno de los últimos de los refaítas, que vivía en Astarot y Edrei,
Nayo nchi ya Ogu mfalme wa Bashani, aliyekuwa mmoja wa mabaki ya Warefai, aliyetawala Ashtarothi na Edrei.
5 gobernaba en el norte, desde el monte Hermón hasta Sacalé, y todo Basán al este, y al oeste hasta las fronteras de los guesuritas y los maacatitas, junto con la mitad de Galaad hasta la frontera de Sehón, rey de Hesbón.
Naye alitawala katika Mlima Hermoni, Saleka, Bashani yote hadi mpaka wa watu wa Geshuri, na watu wa Maaka na nusu ya Gileadi, hadi kwenye mpaka wa Sihoni mfalme wa Heshboni.
6 Moisés, el siervo del Señor, y los israelitas los habían derrotado, y Moisés había asignado la tierra a las tribus de Rubén, Gad y la media tribu de Manasés.
Mose, mtumishi wa Bwana, na Waisraeli wakawashinda. Naye Mose mtumishi wa Bwana akawapa Wareubeni, Wagadi na nusu ya kabila la Manase nchi ya hao wafalme ili iwe milki yao.
7 Estos son los reyes de la tierra que Josué y los israelitas derrotaron al oeste del Jordán, desde Baal Gad, en el valle del Líbano, hasta el monte Halak que conduce a Seír. Josué la entregó a las tribus de Israel para que la poseyeran tal y como les fue asignada.
Hawa ndio wafalme wa nchi ambao Yoshua na Waisraeli waliwashinda upande wa magharibi mwa Yordani, kuanzia Baal-Gadi katika Bonde la Lebanoni hadi kufikia Mlima Halaki, unaoinuka ukielekea Seiri. (Yoshua alitoa nchi zao kwa makabila ya Israeli iwe urithi wao sawasawa na mgawanyiko wa makabila yao:
8 La tierra incluía la región montañosa, las estribaciones, el valle del Jordán, las laderas y el desierto del Néguev: la tierra de los hititas, los amorreos, los cananeos, los ferezeos, los heveos y los jebuseos.
nchi ya vilima, shefela, upande wa magharibi, Araba, materemko ya milima, jangwa, na Negebu; nchi za Wahiti, Waamori, Wakanaani, Waperizi, Wahivi na Wayebusi):
9 El rey de Jericó. El rey de Hai, cerca de Betel.
mfalme wa Yeriko mmoja mfalme wa Ai (karibu na Betheli) mmoja
10 El rey de Jerusalén. El rey de Hebrón.
mfalme wa Yerusalemu mmoja mfalme wa Hebroni mmoja
11 El rey de Jarmut. El rey de Laquis.
mfalme wa Yarmuthi mmoja mfalme wa Lakishi mmoja
12 El rey de Eglón. El rey de Gezer.
mfalme wa Egloni mmoja mfalme wa Gezeri mmoja
13 El rey de Debir. El rey de Geder.
mfalme wa Debiri mmoja mfalme wa Gederi mmoja
14 El rey de Horma. El rey de Arad.
mfalme wa Horma mmoja mfalme wa Aradi mmoja
15 El rey de Libna. El rey de Adulam.
mfalme wa Libna mmoja mfalme wa Adulamu mmoja
16 El rey de Maceda. El rey de Betel.
mfalme wa Makeda mmoja mfalme wa Betheli mmoja
17 El rey de Tappúajh. El rey de Hefer.
mfalme wa Tapua mmoja mfalme wa Heferi mmoja
18 El rey de Afec. El rey de Lasharon.
mfalme wa Afeki mmoja mfalme wa Lasharoni mmoja
19 El rey de Madón. El rey de Hazor.
mfalme wa Madoni mmoja mfalme wa Hazori mmoja
20 El rey de Simrón-merón. El rey de Acsaf.
mfalme wa Shimron-Meroni mmoja mfalme wa Akishafu mmoja
21 El rey de Taanac. El rey de Meguido.
mfalme wa Taanaki mmoja mfalme wa Megido mmoja
22 El rey de Cedes. El rey de Jocneam en el Carmelo.
mfalme wa Kedeshi mmoja mfalme wa Yokneamu katika Karmeli mmoja
23 El rey de Doren Nafat-dor. El rey de Goim en Gilgal.
mfalme wa Dori (katika Nafoth-Dori) mmoja mfalme wa Goimu katika Gilgali mmoja
24 El rey de Tirsa. El total de todos los reyes es de 31.
mfalme wa Tirsa mmoja wafalme jumla yao ilikuwa thelathini na mmoja.