< Job 6 >

1 Entonces Job respondió:
Kisha Ayubu akajibu:
2 “Si se pudiera pesar mi dolor y poner mis problemas en una balanza
“Laiti uchungu wangu ungeweza kupimwa, nayo taabu yangu yote ingewekwa kwenye mizani!
3 serían más pesados que la arena del mar. Por eso hablé tan precipitadamente.
Kwa kuwa hakika ingekuwa nzito kuliko mchanga wa bahari zote, kwa hiyo si ajabu maneno yangu yamekuwa ya haraka.
4 Porque las flechas del Todopoderoso están en mí; su veneno mina mi espíritu. Los terrores de Dios están alineados contra mí.
Mishale ya Mwenyezi iko ndani yangu, roho yangu inakunywa sumu yake; vitisho vya Mungu vimejipanga dhidi yangu.
5 ¿No rebuznan los burros salvajes cuando se les acaba la hierba? ¿No gime el ganado cuando no tiene comida?
Je, punda-mwitu hulia akiwa na majani, au ngʼombe dume hulia akiwa na chakula?
6 ¿Se puede comer sin sal algo que no tiene sabor? ¿Tiene algún sabor la clara del huevo?
Je, chakula kisicho na ladha huliwa bila chumvi, au upo utamu katika ute mweupe wa yai?
7 No puedo tocar ningún alimento, ¡la sola idea me hace sentir enfermo!
Ninakataa kuvigusa; vyakula vya aina hii hunichukiza.
8 ¡Oh, si pudiera tener lo que realmente quiero, que Dios me diera lo que más deseo!
“Laiti ningepata haja yangu, kwamba Mungu angenijalia hilo nililotarajia,
9 ¡Que Dios estuviera dispuesto a aplastarme hasta la muerte, que me dejara morir!
kwamba Mungu angekuwa radhi kuniponda, kuuachia mkono wake na kunikatilia mbali!
10 Pero aún me consuela saber, haciéndome feliz a través del dolor interminable, que nunca he rechazado las palabras de Dios.
Ndipo bado ningekuwa na hii faraja, furaha yangu katika maumivu makali: kwamba sikuwa nimeyakana maneno yake yeye Aliye Mtakatifu.
11 “¿Por qué debo seguir esperando si no tengo fuerzas? ¿Por qué debo seguir adelante si no sé lo que me va a pasar?
“Ninazo nguvu gani, hata niendelee kutumaini? Matazamio yangu ya mbele ni nini, hata niendelee kuwa mvumilivu?
12 ¿Acaso soy fuerte como una roca? ¿Acaso soy de bronce?
Je, mimi nina nguvu za jiwe? Je, mwili wangu ni shaba?
13 ¿Cómo puedo ayudarme a mí mismo ahora que cualquier posibilidad de éxito ha desaparecido?
Je, ninao uwezo wowote wa kujisaidia mimi mwenyewe, wakati ambapo mafanikio yamefukuziwa mbali nami?
14 Quien no es amable con un amigo ha dejado de respetar al Todopoderoso.
“Mtu anayekata tamaa angetazamia moyo wa kujitoa wa rafiki zake, hata kama akiacha uchaji wa Mwenyezi.
15 Mis hermanos han actuado con el mismo engaño que un arroyo del desierto, aguas caudalosas en el desierto que se desvanecen.
Lakini ndugu zangu sio wa kutegemewa, ni kama vijito vya msimu, ni kama vijito ambavyo hufurika
16 El arroyo se desborda cuando está lleno de hielo oscuro y nieve derretida,
wakati vimefunikwa barafu iyeyukayo, ambavyo hujazwa na theluji inayoyeyuka,
17 pero con el calor se seca y desaparece, esfumándose de donde estaba.
lakini hukauka majira ya ukame, na wakati wa hari hutoweka katika mikondo yake.
18 Las caravanas de camellos se apartan para buscar agua, pero no la encuentran y mueren.
Misafara hugeuka kutoka njia zake; hukwea kwenda kwenye nchi ya ukiwa na kuangamia.
19 Las caravanas de Tema buscaron, los viajeros de Saba se confiaron,
Misafara ya Tema inatafuta maji, wafanyabiashara wa Sheba wanaosafiri hutazama kwa matarajio.
20 pero sus esperanzas se desvanecieron: llegaron y no encontraron nada.
Wamedhikika, kwa sababu walikuwa na matumaini; wanafika huko, lakini wanahuzunika kwa kukosa walichotarajia.
21 “Ahora no ayudan en nada. Así de simple: ven mi problema y tienen miedo.
Sasa nanyi mmethibitika kwamba hamna msaada wowote; mnaona jambo la kutisha, nanyi mnaogopa.
22 ¿Les he pedido algo? ¿Acaso les he pedido que sobornen a alguien a mi favor, usando su propio dinero?
Je, nimewahi kusema, ‘Toeni kitu kwa ajili yangu, au mnilipie fidia kutoka mali zenu,
23 ¿Les he pedido que me rescaten de un enemigo? ¿Les he pedido que me salven de mis opresores?
au niokoeni mikononi mwa adui, au nikomboeni kutoka makucha ya wasio na huruma’?
24 Explíquenme esto y me callaré. Muéstrenme en qué me equivoco.
“Nifundisheni, nami nitanyamaza kimya; nionyesheni nilikokosea.
25 Las palabras sinceras son dolorosas, ¿pero qué prueban sus argumentos?
Tazama yalivyo ya kuumiza maneno ya kweli! Lakini mabishano yenu yanathibitisha nini?
26 ¿Van a discutir sobre lo que he dicho, cuando las palabras de alguien desesperado deberían dejar que el viento se las lleve?
Je, mna maana ya kuyasahihisha ninayosema, na kuyafanya maneno ya mtu anayekata tamaa kama upepo?
27 ¡Son capaces de jugar a los dados para ganarle un huérfano, así como son capaces de regatear con su amigo!
Mngeweza hata kupiga kura kwa ajili ya yatima, na kubadilishana rafiki yenu na mali.
28 ¡Mírenme a los ojos y digan si les miento en la cara!
“Lakini sasa kuweni na huruma mkaniangalie mimi. Je, ningeweza kusema uongo mbele zenu?
29 ¡No hablen así! ¡No sean injustos! Lo que digo es correcto.
Tulizeni hasira, msiwe wadhalimu; angalieni tena, kwa maana nimehatarisha uadilifu wangu.
30 No estoy diciendo mentiras. ¿Acaso no sabría yo mismo si me equivoco?”
Je, pana uovu wowote midomoni mwangu? Je, kinywa changu hakiwezi kupambanua hila?

< Job 6 >