< Job 5 >

1 “Llama si quieres, pero ¿quién te va a responder? ¿A qué ángel te vas a dirigir?
“Ita kama unataka, lakini ni nani atakayekujibu? Ni yupi kati ya hao watakatifu utakayemgeukia?
2 Ciertamente la ira mata al necio y la envidia al simple.
Kuweka uchungu moyoni humuua mpumbavu, nao wivu humchinja mjinga.
3 He visto a un necio hacerse fuerte, pero enseguida maldije su casa.
Mimi mwenyewe nimemwona mpumbavu akistawi, lakini ghafula nyumba yake ikawa imelaaniwa.
4 Sus hijos nunca están a salvo; son aplastados en el tribunal sin nadie que los defienda.
Watoto wake wako mbali na usalama, hushindwa mahakamani bila mtetezi.
5 El hambriento se come todo lo que cosecha, tomando incluso lo que está protegido por un seto de espinas, mientras otros procuran robar su riqueza.
Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
6 Porque el mal no nace del polvo, ni los problemas crecen de la tierra.
Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
7 Pero los seres humanos nacen para los problemas con la misma certeza que las chispas de un fuego vuelan hacia arriba.
Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
8 “Si fuera yo, iría donde Dios y expondría mi caso ante él.
“Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
9 Él es quien hace cosas asombrosas, increíbles; ¡milagros que no se pueden contar!
Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
10 Él hace llover sobre la tierra y envía agua a los campos.
Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
11 Exalta a los humildes y rescata a los que lloran.
Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
12 Frustra los planes de los astutos para que no tengan éxito.
Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
13 Él atrapa a los sabios en sus propios pensamientos astutos, y los planes de la gente retorcida se ven truncados.
Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
14 De día están a oscuras, y a mediodía tropiezan como si fuera de noche.
Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
15 Pero Dios es el que salva de sus comentarios cortantes, así como salva a los pobres de las acciones de los poderosos.
Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
16 Así los desvalidos tienen esperanza, y los malvados tienen que cerrar la boca.
Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
17 Mira qué feliz es la persona a la que Dios corrige, así que no desprecies la disciplina del Todopoderoso.
“Heri mtu yule ambaye Mungu humrudi; kwa hiyo usidharau adhabu yake Mwenyezi.
18 Porque él causa dolor, pero proporciona alivio; él hiere, pero sus manos curan.
Kwa kuwa hutia jeraha, lakini pia huyafunga; huumiza, lakini mikono yake pia huponya.
19 Él te salvará de muchos desastres; una multitud de males no te afectará.
Kutoka majanga sita atakuokoa; naam, hata katika saba hakuna dhara litakalokupata wewe.
20 En tiempos de hambre te librará de la muerte, y en tiempos de guerra te salvará del poder de la espada.
Wakati wa njaa atakukomboa wewe na kifo, naye katika vita atakukomboa na pigo la upanga.
21 Estarás protegido de la calumnia de lengua afilada; y cuando llegue la violencia no tendrás miedo.
Utalindwa kutokana na kichapo cha ulimi, wala hutakuwa na sababu ya kuogopa maangamizi yatakapokujia.
22 Te reirás de la violencia y del hambre; no tendrás miedo de los animales salvajes,
Utayacheka maangamizo na njaa, wala hutakuwa na sababu ya kuwaogopa wanyama wakali wa mwituni.
23 porque estarás en paz con las piedras del campo y los animales salvajes estarán en paz contigo.
Kwa kuwa utakuwa na agano na mawe ya mashamba, nao wanyama wa mwitu watakuwa na amani nawe.
24 Estarás seguro de que tu casa está a salvo, porque irás a donde vives y no habrá cosa alguna que te falte.
Utajua ya kwamba hema lako li salama; utahesabu mali zako wala hutakuta chochote kilichopungua.
25 También estarás seguro de que tendrás muchos hijos; tu descendencia será como la hierba de la tierra.
Utajua ya kuwa watoto wako watakuwa wengi, nao wazao wako wengi kama majani ya nchi.
26 Vivirás hasta una edad madura como una gavilla de grano cuando se cosecha.
Utaingia kaburini ukiwa na umri wa uzee mtimilifu, kama masuke ya ngano yakusanywapo kwa wakati wake.
27 Mira, lo hemos examinado y es verdad. Escucha lo que te digo y aplícalo a ti mismo”.
“Tumelichunguza hili, nalo ni kweli. Hivyo lisikie na ulitendee kazi.”

< Job 5 >