< Job 41 >
1 “¿Puedes sacar a Leviatán con un anzuelo? ¿Puedes atarle la boca?
Je waweza kumvua mamba kwa ndoano ya samaki? Au kumfunga taya zake kwa kamba?
2 ¿Puedes pasar una cuerda por su nariz? ¿Puedes pasarle un anzuelo por la mandíbula?
Je waweza kuweka kamba katika pua zake, au kumtoboa taya yake kwa ndoano?
3 ¿Te rogará que lo dejes ir? ¿O te hablará suavemente?
Je atafanya maombi mengi kwako? Je atazungumza na wewe kwa maneno laini?
4 ¿Hará un contrato contigo? ¿Acepta ser tu esclavo para siempre?
Je atafanya agano na wewe, ili kwamba umchukue kwa ajili ya mtumishi milele?
5 ¿Jugarás con él como con un pájaro? ¿Le pondrás una correa para tus chicas?
Je utacheza pamoja naye kama ambavyo ungecheza na ndege? Je utamfunga kwa ajili ya mtumishi wako wa kike?
6 ¿Decidirán tus socios comerciales un precio para él y lo repartirán entre los mercaderes?
Je makundi ya wavuvi waweza kumfanyia biashara? Je watamgawanya ili kufanya biashara miongoni mwa wafanya biashara?
7 ¿Pueden atravesar su piel con muchos arpones, su cabeza con lanzas de pesca?
Je waweza kuijaza ngozi yake kwa vyusa au kichwa chake kwa mikuki ya kuvulia?
8 Si lo agarraras, ¡imagina la batalla que tendrías! ¡No volverías a hacerlo!
Weka mkono wako juu yake mara moja, nawe utaikumbuka vita na hautaendelea kufanya hivyo tena.
9 Cualquier esperanza de capturarlo es una tontería. Cualquiera que lo intente será arrojado al suelo.
Tazama, matumaini ya kila mtu ambaye hufanya hivyo ni uongo; je si kila mmoja atatupwa chini katika nchi mbele yake?
10 Ya que nadie tiene el valor de provocar al Leviatán, ¿quién se atrevería a enfrentarse a mí?
Hakuna aliye mkali ambaye aweza kuthubutu kumtikisa mamba; Ni nani basi awezaye kusimama mbele yake?
11 ¿Quién se ha enfrentado a mí con alguna reclamación que deba pagar? Todo lo que hay bajo el cielo me pertenece.
Ni nani kwanza aliyenipa kitu chochote ili kwamba niweze kumlipa? Chochote kilicho chini ya anga ni changu.
12 “Permítanme hablarles del Leviatán: sus poderosas patas y sus gráciles proporciones.
Sitanyamaza kimya kuhusu miguu ya mamba, wala kuhusu jambo linalohusu nguvu zake, wala kuhusu umbo lake zuri.
13 ¿Quién puede quitarle la piel? ¿Quién puede penetrar su doble armadura?
Nani awezaye kuiondoa ngozi yake? Nani anaweza kumchoma kwa silaha mara mbili?
14 ¿Quién puede abrir sus mandíbulas? Sus dientes son aterradores.
Nani awezaye kuifungua milango ya uso wake, imezungukwa na meno yake ambayo yanaogofya?
15 Su orgullo son sus hileras de escamas, cerradas con fuerza.
Mgongo wake umefanywa kwa magamba yenye mistari, yamefungwa kwa pamoja kama chapa.
16 Sus escamas están tan juntas que el aire no puede pasar entre ellas.
Moja li karibu na jingine na ya kuwa hakuna hewa inaweza kupita katikati yake.
17 Cada escama se adhiere a la siguiente; se cierran entre sí y nada puede penetrar en ellas.
Yameunganishwa moja kwa jingine; yamegandamana kwa pamoja, ili kwamba hayawezi kutenganishwa.
18 Cuando estornuda, brilla la luz. Sus ojos son como el sol naciente.
Mwanga hung'ara kutoka katika kupumua kwake; macho yake ni kama kope za mapambazuko ya asubuhi.
19 De su boca salen llamas y chispas de fuego.
Ndani ya mdomo wake hutoka miali ya mwanga, chembe za moto huruka nje.
20 De sus fosas nasales sale humo, como el vapor de una caldera sobre un fuego de cañas.
Katika pua zake hutoka moshi kama chungu kinachotokota juu ya moto ambao umechochewa ili uwe na joto sana.
21 Su aliento prende fuego al carbón mientras las llamas salen de su boca.
Pumzi yake huwasha mkaa na kuwa mwali; moto hutoka katika mdomo wake.
22 Su cuello es poderoso, y todos los que se enfrentan a él tiemblan de terror.
Katika shingo yake kuna nguvu, na kitisho hucheza mbele yake.
23 Su cuerpo es denso y sólido, como si estuviera hecho de metal fundido.
Nofu za mwili wake zimeunganishwa pamoja; ziko imara katika yeye; wala haziwezi kuondolewa.
24 Su corazón es duro como una piedra de molino.
Moyo wake ni mgumu kama jiwe - hakika, ni mgumu kama jiwe la chini la kusagia.
25 Cuando se levanta, incluso los poderosos se aterrorizan; retroceden cuando se agita.
Na anaposimama mwenyewe, hata miungu huogopa; hurudi nyuma kwasababu ya hofu.
26 Las espadas rebotan en él, al igual que las lanzas, los dardos y las jabalinas.
Na ikiwa atapigwa kwa upanga, hauwezi kumfanya kitu chochote, wala mkuki, wala mshale, wala aina yoyote ya silaha iliyochongoka.
27 El hierro es como la paja y el bronce es como la madera podrida.
Yeye hufikiri juu ya chuma kana kwamba ni majani makavu na hufikiri juu ya fedha kana kwamba ni ubao uliooza.
28 Las flechas no pueden hacerle huir; las piedras de las hondas son como trozos de rastrojo.
Mshale hauwezi akamfanya akimbie; kwake yeye mawe ya kombeo huwa kama makapi.
29 Los garrotes son también como rastrojos; se ríe del ruido de las lanzas que vuelan.
Marungu huyaangalia kama majani makavu; yeye hucheka juu ya mkuki unaovuma.
30 Sus partes inferiores están cubiertas de puntas afiladas como ollas rotas; cuando se arrastra por el barro deja marcas como un trillo.
Sehemu zake za chini zi kama vipande vilivyochongoka vya vyungu; huacha alama zilizosambaa katika udongo kana kwamba alikuwa ni chombo cha kusagia.
31 Revuelve el mar como el agua en una olla hirviendo, como un cuenco humeante cuando se mezcla el ungüento.
Yeye hukifanya kilindi kichemke kama chungu cha maji ya moto; huifanya bahari kama chungu cha lihamu.
32 Deja tras de sí una estela reluciente, como si el mar tuviera cabellos blancos.
Yeye huifanya njia ing'are nyuma yake; mtu mmoja angedhani kilindi kuwa cheupe.
33 No hay nada en la tierra como él: una criatura que no tiene miedo.
Hakuna cha kumlinganisha juu ya dunia, ambaye yeye alikuwa ameumbwa kuishi pasipo hofu.
34 Mira con desprecio a todas las demás criaturas. Es el más orgulloso de todos”.
Hukiona kila kitu chenye kiburi; yeye ni mfalme juu ya wana wote wa kiburi.”