< Job 40 >

1 Dios siguió hablando a Job.
Bwana akamwambia Ayubu:
2 “¿Todavía vas a pelear con el Todopoderoso y tratar de enderezarlo? Quien discute con Dios debe dar alguna respuesta”.
“Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
3 Job respondió al Señor:
Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
4 “Yo no soy nada. No tengo respuestas. Pongo mi mano delante de mi boca.
“Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
5 Ya he dicho demasiado y no diré nada más”.
Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
6 Entonces el Señor respondió a Job desde el torbellino:
Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
7 “Prepárate, sé fuerte, porque voy a interrogarte y debes responderme.
“Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
8 “¿De verdad vas a decir que mis decisiones están equivocadas? ¿Vas a condenarme para tener razón?
“Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
9 ¿Eres tan poderoso como yo? ¿Truena tu voz como la mía?
Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
10 ¿Por qué no te vistes de majestad y dignidad, y te revistes de gloria y esplendor?
Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
11 Da rienda suelta a tu feroz ira. Humilla a los soberbios con una mirada.
Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
12 Derriba a los soberbios con tu mirada; pisotea a los malvados allí donde están.
mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
13 Entiérralos en el polvo; enciérralos en la tumba.
Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
14 Entonces también estaré de acuerdo en que tu propia fuerza puede salvarte.
Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
15 “Considera a Behemot, una criatura que hice igual que a ti. Come hierba como el ganado.
“Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
16 Mira sus poderosos lomos, los músculos de su vientre.
Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
17 Dobla su cola como un cedro; los tendones de sus muslos son fuertes.
Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
18 Sus huesos son como tubos de bronce, sus miembros como barras de hierro.
Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
19 Es el ejemplo más importante de lo que Dios puede hacer; sólo el que lo hizo puede acercarse a él con una espada.
Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
20 Las colinas producen alimento para él, y todos los animales salvajes juegan allí.
Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
21 Se encuentra bajo el loto; se esconde en los juncos del pantano.
Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
22 El loto la cubre de sombra; los sauces del valle la rodean.
Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
23 Aunque el río se desborde, no se preocupa; permanece en calma cuando el río Jordán se agita contra él.
Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
24 Nadie puede atraparlo mientras mira, ni perforar su nariz con un lazo”.
Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?

< Job 40 >