< Job 37 >

1 “Ante esto mi corazón tiembla, latiendo rápidamente dentro de mí.
“Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
2 Escucha con atención la voz atronadora de Dios que retumba al hablar.
Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
3 Lo envía a través del cielo; sus relámpagos brillan hasta los confines de la tierra.
Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
4 Luego viene el estruendo del trueno, su voz majestuosa no se contiene cuando habla.
Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
5 ¡La voz atronadora de Dios es maravillosa! No podemos comprender las grandes cosas que hace.
Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
6 “Ordena que caiga la nieve y que llueva sobre la tierra.
Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
7 Con ello detiene el trabajo de la gente para que todos puedan entender lo que hace.
Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
8 Incluso los animales se refugian y permanecen en sus guaridas.
Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
9 El viento del sur sopla en las tormentas, mientras que el viento del norte sopla cuando hace frío.
Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
10 El aliento de Dios produce hielo, congelando la superficie del agua.
Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
11 Llena las nubes de humedad y esparce desde ellas sus rayos.
Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
12 Se arremolinan bajo su control; se mueven por toda la tierra según sus órdenes.
Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
13 Lo hace para cumplir su voluntad, ya sea para disciplinar o para mostrar su bondad.
Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
14 “Escucha esto, Job. Detente un momento y considera las cosas maravillosas que hace Dios.
“Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
15 ¿Sabes cómo Dios controla las nubes, o cómo hace que sus relámpagos salgan de ellas?
Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
16 ¿Sabes cómo flotan las nubes en el cielo: la maravillosa obra de quien lo sabe todo.
Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
17 Tú sabes que tu ropa gotea de sudor cuando el viento del sur trae un aire caliente y pesado.
Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
18 ¿Puedes martillar el cielo para que sea como un espejo fundido, como hace él?
je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
19 “Entonces, ¿por qué no nos enseñas lo que hay que decirle a Dios? No podemos exponer nuestro caso porque estamos a oscuras!
“Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
20 ¿Hay que decirle a Dios que quiero hablar? Cualquiera que lo quisiera sería destruido!
Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
21 Al fin y al cabo, no podemos mirar al sol cuando brilla en el cielo, después de que el viento haya despejado las nubes.
Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
22 Del norte sale Dios brillando como el oro, rodeado de una majestad impresionante.
Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
23 No podemos acercarnos al Todopoderoso, porque nos supera en poder y justicia, y en hacer el bien.
Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
24 No actúa como un tirano; no es de extrañar que la gente le tema, aunque no valora a los que se creen sabios”.
Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”

< Job 37 >