< Job 26 >

1 Job respondió:
Kisha Ayubu akajibu:
2 “Qué útil has sido para este débil hombre que soy. Qué solidario has sido con el débil.
“Tazama jinsi ulivyomsaidia mtu asiye na uwezo! Jinsi ulivyouokoa mkono ulio dhaifu!
3 Qué buenos consejos le has dado a este ignorante, demostrando que tienes mucha sabiduría.
Ni shauri gani ulilompa yeye asiye na hekima? Nayo ni busara gani kubwa uliyoonyesha!
4 ¿Quién te ayudó a decir estas palabras? ¿Quién te ha inspirado a decir tales cosas?
Ni nani aliyekusaidia kutamka maneno hayo? Nayo ni roho ya nani iliyosema kutoka kinywani mwako?
5 “Los muertos tiemblan, los que están bajo las aguas.
“Wafu wako katika maumivu makuu, wale walio chini ya maji na wale waishio ndani yake.
6 El Seol está desnudo ante Dios, Abadón está descubierto. (Sheol h7585)
Mauti iko wazi mbele za Mungu; Uharibifu haukufunikwa. (Sheol h7585)
7 Extiende el cielo del norte sobre el espacio vacío; cuelga el mundo sobre la nada.
Hutandaza anga la kaskazini mahali patupu; naye huiningʼiniza dunia mahali pasipo na kitu.
8 Recoge la lluvia en sus nubes de tormenta que no se rompen bajo el peso.
Huyafungia maji kwenye mawingu yake, hata hivyo mawingu hayapasuki kwa uzito wake.
9 Él vela su trono; lo cubre con sus nubes.
Huufunika uso wa mwezi mpevu, akitandaza mawingu juu yake.
10 Sobre la superficie de las aguas puso una frontera; fijó un límite que divide la luz de las tinieblas.
Amechora mstari wa upeo juu ya uso wa maji, ameweka mpaka wa nuru na giza.
11 Las columnas del cielo tiemblan; tiemblan de miedo ante su reprimenda.
Nguzo za mbingu nazo zatetemeka, zinatishika anapozikemea.
12 Calmó el mar con su poder; porque sabía qué hacer aplastó a Rahab.
Kwa nguvu zake aliisukasuka bahari; kwa hekima yake alimkata Rahabu vipande vipande.
13 El aliento de su voz embelleció los cielos; con su mano atravesó la serpiente que se desliza.
Aliisafisha anga kwa pumzi yake; kwa mkono wake alimchoma joka aendaye mbio.
14 Esto es sólo un poco de todo lo que hace; lo que oímos de él es apenas un susurro, así que quién puede entender su poder atronador?”
Haya ni mambo madogo tu katika matendo yake; tazama jinsi ulivyo mdogo mnongʼono tunaousikia kumhusu! Ni nani basi awezaye kuelewa ngurumo za nguvu zake?”

< Job 26 >