< Job 12 >

1 Job contestó:
Ndipo Ayubu akajibu:
2 “Ustedes realmente creen que son personas especiales, ¿no es así? Obviamente, cuando mueran, la sabiduría morirá con ustedes.
“Bila shaka ninyi ndio watu, nayo hekima itakoma mtakapokufa!
3 Pero yo también tengo conocimientos, y ustedes no son mejores que yo. ¿No sabe todo el mundo las cosas que han dicho?
Lakini mimi ninao ufahamu kama ninyi; mimi si duni kwenu. Ni nani asiyejua mambo haya yote?
4 Pero mis amigos se ríen de mí porque invoqué a Dios y él me respondió: el hombre inocente que hace el bien se ha convertido en objeto de burla.
“Nimekuwa mtu wa kuchekwa na rafiki zangu, ingawa nilimwita Mungu naye akanijibu: mimi ni mtu wa kuchekwa tu, ingawa ni mwadilifu na nisiye na hatia!
5 La gente que está bien desprecia a los que tienen problemas; están dispuestos a empujar a los que ya resbalan.
Wanadamu wakiwa katika utulivu huwa na dharau kwa wale wenye msiba kana kwamba ndiyo haki ya wale ambao miguu yao inateleza.
6 Los ladrones viven en paz, y los que hacen enojar a Dios viven seguros, confiando en su propia fuerza como su ‘dios’.
Hema za wanyangʼanyi hazisumbuliwi, wale wanaomghadhibisha Mungu wako salama: wale wamchukuao mungu wao mikononi mwao.
7 “Pero si les preguntas a los animales, ellos te enseñarán; las aves del cielo te lo dirán;
“Lakini ulizeni wanyama, nao watawafundisha, au ndege wa angani, nao watawaambia;
8 pregúntale a la tierra y ella te enseñará; y los peces del mar te lo dirán.
au zungumzeni na dunia, nayo itawafundisha, au acheni samaki wa baharini wawape taarifa.
9 ¿Quién de todos ellos no sabe que el Señor ha hecho esto?
Ni nani miongoni mwa hawa wote asiyejua kwamba mkono wa Bwana ndio uliofanya hili?
10 Él da vida a todo ser viviente, y a toda la humanidad.
Mkononi mwake kuna uhai wa kila kiumbe, na pumzi ya wanadamu wote.
11 El oído distingue palabras como el paladar distingue los alimentos.
Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile ulimi uonjavyo chakula?
12 La sabiduría para distinguir pertenece a los ancianos, y la habilidad para discriminar correctamente pertenece a los que tienen una larga experiencia.
Je, hekima haipatikani katikati ya wazee? Je, maisha marefu hayaleti ufahamu?
13 Dios tiene sabiduría y poder, el consejo y el entendimiento le pertenecen.
“Hekima na nguvu ni vya Mungu; shauri na ufahamu ni vyake yeye.
14 Si derriba algo, nadie puede reconstruirlo. Si encarcela a alguien, nadie podrá liberarlo.
Kile anachokibomoa hakiwezi kujengeka tena; mtu aliyefungiwa naye hawezi kufunguliwa.
15 Si Dios retiene las aguas, todo se seca; si las suelta, la tierra se inunda.
Akizuia maji, huwa pana ukame; akiyaachia maji, huharibu nchi.
16 Él es poderoso y victorioso; tanto los engañadores como los engañados están sometidos a él.
Kwake kuna nguvu na ushindi; adanganywaye na adanganyaye, wote wawili ni wake.
17 Lleva a los consejeros despojados de su sabiduría, convierte a los jueces en necios.
Yeye huwaondoa washauri wakiwa wametekwa nyara, naye huwapumbaza wanaotoa maamuzi.
18 Él le quita a los reyes sus gruesos collares y los hace vestir taparrabos.
Huondoa pingu zilizofungwa na wafalme, na kuwafunga mishipi ya kiunoni.
19 Él expulsa a los sacerdotes, despojados de sus vestimentas religiosas, y derriba a los poderosos.
Huwaondoa makuhani wakiwa wametekwa nyara, na kuwaangusha waliojiimarisha muda mrefu.
20 Quita el consejo de los consejeros fieles, quita el discernimiento de los ancianos.
Hunyamazisha midomo ya washauri wanaoaminika, na kuondoa busara ya wazee.
21 Derrama el desprecio sobre los príncipes y les quita el poder de los fuertes.
Huwamwagia dharau wanaoheshimika, na kuwavua silaha wenye nguvu.
22 Él revela lo que está oculto en las tinieblas, y saca a la luz la sombra de la muerte.
Hufunua mambo ya ndani ya gizani, na kuyaleta nuruni yale yaliyositirika sana.
23 Él engrandece a las naciones y las destruye; expande a las naciones y las arruina.
Huyafanya mataifa yatukuke na kuyaangamiza; hufanya mataifa kuwa makubwa, naye huyatawanya.
24 Él quita el entendimiento de los gobernantes y los hace vagar por el desierto.
Huwaondolea viongozi wa nchi akili zao; huwapeleka watangetange nyikani pasipo na njia.
25 Andan a tientas en la oscuridad, sin luz. Él los hace tambalearse como borrachos”.
Hupapasa gizani pasipokuwa na mwanga; huwafanya wapepesuke kama walevi.

< Job 12 >