< Job 10 >

1 ¡Odio mi vida! Permíteme hablar libremente de mis quejas; no puedo guardarme mi amargura.
“Nayachukia sana haya maisha yangu; kwa hiyo nitatoa malalamiko yangu kwa wazi bila kujizuia, nami nitanena kutokana na uchungu wa moyo wangu.
2 Le diré a Dios: “No te limites a condenarme; dime qué tienes contra mí.
Nitamwambia Mungu: Usinihukumu, bali niambie una mashtaka gani dhidi yangu.
3 ¿Te gusta acusarme? ¿Por qué me rechazas a mí, a quien has creado con tus propias manos, y sin embargo te alegras de las maquinaciones de los malvados?
Je, inakupendeza wewe kunionea, kuikataa kwa dharau kazi ya mikono yako, huku wewe ukitabasamu juu ya mipango ya waovu?
4 ¿Tienes ojos humanos? ¿Ves como los seres humanos?
Je, wewe una macho ya kimwili? Je, wewe huona kama mwanadamu aonavyo?
5 ¿Es tu vida tan corta como la de los mortales? ¿Son tus años tan breves como los de la humanidad,
Je, siku zako ni kama zile za mwanadamu, au miaka yako ni kama ile ya mtu,
6 para que tengas que examinar mis males e investigar mis pecados?
ili kwamba utafute makosa yangu na kuichunguza dhambi yangu;
7 Aunque sabes que no soy culpable, nadie puede salvarme de ti.
ingawa wajua kuwa mimi sina hatia, na hakuna awezaye kunitoa mkononi mwako?
8 Me hiciste y me diste forma con tus propias manos, y sin embargo me destruyes.
“Mikono yako ndiyo iliyoniumba na kunifanya. Je, sasa utageuka na kuniangamiza?
9 Recuerda que me diste forma como a un pedazo de arcilla; ¿vas a volver a convertirme en polvo?
Kumbuka kuwa ulinifinyanga kama udongo wa mfinyanzi. Je, sasa utanifanya kuwa mavumbi tena?
10 Me derramaste como la leche, me cuajaste como el queso.
Je, wewe hukunimimina mimi kama maziwa, na kunigandisha kama jibini,
11 Me vestiste de piel y carne; tejiste mi cuerpo con huesos y músculos.
ukanivika ngozi na nyama, na kuniunga pamoja kwa mifupa na mishipa?
12 Me diste vida y me mostraste tu bondad; me has cuidado mucho.
Umenipa uhai na kunitendea wema, katika uangalizi wako umeilinda roho yangu.
13 “Pero guardaste estas cosas en tu corazón. Sé que tu propósito era
“Lakini hili ndilo ulilolificha moyoni mwako, nami ninajua kuwa hili lilikuwa katika nia yako:
14 vigilarme, y si pecaba, entonces no perdonarías mis males.
Kama nilifanya dhambi, ungekuwa umeniona, wala usingeacha kosa langu lipite bila kuadhibiwa.
15 Si soy culpable, estoy en problemas; si soy inocente, no puedo mantener la cabeza en alto porque estoy totalmente deshonrado al ver mis sufrimientos.
Kama nina hatia, ole wangu! Hata kama ningekuwa sina hatia, siwezi kukiinua kichwa changu, kwa kuwa nimejawa na aibu, na kuzama katika mateso yangu.
16 Si mantengo la cabeza alta me persigues como un león, mostrando lo poderoso que eres para herirme.
Kama nikiinua kichwa changu juu, unaninyatia kama simba, na kuonyesha tena uwezo wa kutisha dhidi yangu.
17 Repites tus argumentos contra mí, derramas más y más tu ira contra mí, envías nuevos ejércitos contra mí.
Wewe waleta mashahidi wapya dhidi yangu na kuzidisha hasira yako juu yangu; nazo nguvu zako zinanijia wimbi moja baada ya jingine.
18 “¿Por qué me dejaste nacer? Ojalá hubiera muerto y nadie me hubiera visto nunca.
“Kwa nini basi ulinitoa tumboni? Ninatamani ningekufa kabla jicho lolote halijaniona.
19 Hubiera sido mejor que nunca hubiera existido, llevado directamente del vientre a la tumba.
Laiti nisingekuwako kamwe, au ningekuwa nimechukuliwa moja kwa moja kutoka tumboni kwenda kaburini!
20 Sólo me quedan unos días, así que ¿por qué no me dejas en paz para que pueda tener un poco de paz
Je, siku zangu chache si zimekaribia kuisha? Niachie ili niweze kupata muda mfupi wa kufurahi
21 antes de ir al sitio de donde nunca volveré, la tierra de las tinieblas y la sombra de la muerte?
kabla sijaenda mahali ambapo hakuna kurudi tena, katika nchi ya giza na uvuli wa mauti,
22 La tierra de la oscuridad total donde se encuentra la sombra de la muerte, un lugar de caos donde la luz misma es oscuridad”.
nchi ya giza kuu sana, yenye uvuli wa giza na machafuko, mahali ambapo hata nuru ni giza.”

< Job 10 >