< Génesis 7 >

1 El Señor le dijo a Noé: “Entra al arca con toda tu familia. Porque he visto que eres un hombre íntegro, que vive una vida moral en medio de la gente de esta generación.
Ndipo Bwana akamwambia Noa, “Ingia katika safina wewe na jamaa yako yote, kwa sababu katika kizazi hiki nimeona ya kuwa wewe ni mwenye haki.
2 Toma contigo siete parejas - macho y hembra - de cada especie de animal limpio; y un par - macho y hembra - de cada especie de animal impuro.
Uchukue wanyama saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, na wanyama wawili wawili wa kila aina walio najisi wa kiume na wa kike.
3 Además, toma siete parejas - macho y hembra - de todas las aves, para que todas las especies de toda la tierra puedan sobrevivir.
Pia uchukue ndege saba walio safi wa kila aina, wa kiume na wa kike, ili kuhifadhi aina zao mbalimbali katika dunia yote.
4 En siete días hare llover por cuarenta días y cuarenta noches. Voy a erradicar de la superficie de la tierra a todos los seres que he creado”.
Siku saba kuanzia sasa nitaleta mvua juu ya nchi kwa siku arobaini usiku na mchana, nami nitafutilia mbali kutoka uso wa nchi kila kiumbe hai nilichokiumba.”
5 Y Noé hizo exactamente lo que el Señor le ordenó que hiciera.
Noa akafanya yote kama Bwana alivyomwamuru.
6 Noé tenía 600 años cuando las aguas inundaron la tierra.
Noa alikuwa na miaka 600 gharika ilipokuja juu ya dunia.
7 Noé entró al arca, junto con su esposa y sus hijos, y las esposas de sus hijos, por causa del diluvio.
Noa na mkewe na wanawe na wake zao wakaingia katika safina ili waepuke ile gharika.
8 Animales puros e impuros, aves y reptiles,
Jozi ya wanyama walio safi na walio najisi, ndege na viumbe vitambaavyo,
9 entraron en el arca que construyó Noé.
wa kiume na wa kike, walikuja kwa Noa wakaingia katika safina kama Mungu alivyomwamuru Noa.
10 Después de siete días, las aguas cayeron sobre la tierra.
Baada ya siku saba, maji ya gharika yakaja juu ya dunia.
11 Noé había cumplido 600 años, cuando en el día número diecisiete del segundo mes, todas las aguas que estaban debajo de la tierra estallaron y atravesaron el suelo, y una fuerte lluvia cayó del cielo.
Katika siku ya kumi na saba ya mwezi wa pili mwaka wa 600 wa kuishi kwake Noa, siku hiyo ndipo chemchemi zote hata zilizo chini sana ya ardhi zilibubujika kwa nguvu, na malango ya mafuriko ya mbinguni yakafunguliwa.
12 La lluvia siguió cayendo sobre la tierra durante cuarenta días y cuarenta noches.
Mvua ikanyesha juu ya nchi siku arobaini usiku na mchana.
13 Ese fue el día en que el Noé, su esposa, sus hijos Sem, Cam y Jafet, junto a sus esposas, entraron en el arca.
Siku hiyo Noa, na mkewe, na wanawe Shemu, Hamu na Yafethi pamoja na wake zao wakaingia katika ile safina.
14 Con ellos entró toda especie de animales salvajes, ganado, reptiles y aves, así como todo animal alado.
Nao walikuwa pamoja na kila mnyama wa mwituni kufuatana na aina yake, wanyama wote wafugwao kufuatana na aina zao, kila kiumbe kitambaacho juu ya ardhi kwa aina yake, na kila ndege kufuatana na aina yake, naam kila kiumbe chenye mabawa.
15 Todos entraron con Noé al arca; todos los seres vivos, y en pares.
Viumbe vyote vyenye pumzi ya uhai ndani yake vikaja kwa Noa viwili viwili, vikaingia katika safina.
16 De cada criatura entró el macho con su hembra, tal como Dios le dijo a Noé. Entonces el Señor cerró la puerta.
Wanyama walioingia katika safina walikuwa wa kiume na wa kike, wa kila kiumbe chenye uhai kama Mungu alivyomwamuru Noa, ndipo Bwana akamfungia ndani.
17 Y la lluvia cayó sobre la tierra por cuarenta días, haciendo flotar el arca por encima del suelo.
Kwa siku arobaini mafuriko yaliendelea kujaa duniani na maji yalivyozidi kuongezeka, yaliinua safina juu sana kutoka kwenye uso wa nchi.
18 Las aguas subieron cada vez más y se hacían profundas, pero el arca flotaba en la superficie.
Maji yakajaa na kuongezeka sana juu ya nchi, na safina ikaelea juu ya uso wa maji.
19 Finalmente, el agua aumentó tanto de nivel que hasta las montañas más altas quedaron cubiertas, y solo se podía ver el cielo.
Maji yakazidi kujaa juu ya nchi, yakaifunika milima yote mirefu chini ya mbingu yote.
20 El agua subió tanto, que sobrepasó la altura de las montañas hasta quince codos más.
Maji yakaendelea kujaa yakaifunika milima kwa kina cha zaidi ya dhiraa kumi na tano.
21 Y todo lo que habitaba sobre la tierra pereció: las aves, el ganado, los animales salvajes, todos los reptiles, y todas las personas también.
Kila kiumbe hai kitambaacho juu ya nchi kikaangamia: Ndege, wanyama wa kufugwa, wanyama pori, viumbe vyote juu ya nchi na wanadamu wote.
22 Murió todo ser vivo que estaba sobre la tierra y que podía respirar.
Kila kiumbe juu ya nchi kavu chenye pumzi ya uhai kikafa.
23 El Señor exterminó a todo ser viviente: desde los seres humanos, hasta el ganado, los reptiles y las aves. Todos murieron y solo sobrevivieron los que estaban con Noé en el arca.
Kila kitu chenye uhai juu ya uso wa nchi kilifutiliwa mbali, watu, wanyama, viumbe vitambaavyo na ndege warukao angani wakafutiliwa mbali toka duniani. Waliobaki ni Noa peke yake na wale waliokuwa pamoja naye ndani ya safina.
24 Y la tierra permaneció inundada por 150 días.
Maji yakaifunika dunia kwa siku 150.

< Génesis 7 >

The Great Flood
The Great Flood