< Génesis 11 >

1 En ese tiempo se hablaba en todo el mundo un solo idioma y todos usaban palabras con el mismo significado.
Wakati huo dunia yote ilikuwa na lugha moja na msemo mmoja.
2 Al trasladarse hacia el oriente, descubrieron una llanura en la región del Sinar y se asentaron allí.
Watu walipoelekea upande wa mashariki, wakafika kwenye tambarare katika nchi ya Shinari nao wakaishi huko.
3 Y se dijeron unos a otros: “Vengan, juntemos ladrillos y cocinémoslos con fuego”. (Usaron ladrillo en lugar de piedra, y alquitrán en lugar de cemento).
Wakasemezana wao kwa wao, “Njooni, tufyatue matofali na tuyachome vizuri kwa moto.” Walitumia matofali badala ya mawe, na lami kwa ajili ya kushikamanishia hayo matofali.
4 Y entonces dijeron: “Construyamos ahora una ciudad para nosotros mismos con una torre cuya cúspide llegue hasta el cielo. Así lograremos tener una gran reputación y no andaremos dispersos por todo el mundo”.
Ndipo wakasema, “Njooni, tujijengee mji wenye mnara ambao utafika hadi mbinguni, ili tujipatie jina tusije tukatawanyika usoni pa dunia yote.”
5 Pero el Señor descendió para mirar la ciudad y la torre que estas personas estaban construyendo.
Lakini Bwana akashuka ili auone mji na mnara ambao wanadamu waliokuwa wanaujenga.
6 Y el Señor dijo: “Miren cómo estas personas están unidas y hablando el mismo idioma. ¡Si pueden lograr todo esto tan solo comenzando, nada les será imposible si se fijan un propósito!
Bwana akasema, “Ikiwa kama taifa moja wanaozungumza lugha moja wameanza kufanya hili, basi hakuna lolote watakalopanga kufanya ambalo halitawezekana kwao.
7 Necesitamos bajar allí y confundir su idioma para que no puedan entender lo que se dicen unos a otros”.
Njooni, tushuke tuvuruge lugha yao ili wasielewane wao kwa wao.”
8 Y entonces el Señor los expulsó de allí e hizo que se dispersaran por todo el mundo, y dejaron de construir la ciudad.
Hivyo Bwana akawatawanya kutoka mahali pale kwenda katika dunia yote, nao wakaacha kuujenga huo mji.
9 Por eso la ciudad fue llamada Babel, porque el Señor confundió el idioma que se hablaba en el mundo.
Ndiyo maana pakaitwa Babeli, kwa sababu hapo ndipo Bwana alipoivuruga lugha ya dunia nzima. Kutoka hapo Bwana akawatawanya katika uso wa dunia yote.
10 La siguiente es la genealogía de Sem. Cuando Sem tuvo 100 años, nació su hijo Arfaxad. Esto sucedió dos años después del diluvio.
Hivi ndivyo vizazi vya Shemu. Miaka miwili baada ya gharika, Shemu alipokuwa na miaka 100, akamzaa Arfaksadi.
11 Después del nacimiento de Arfaxad, Sem vivió 500 años más y tuvo más hijos e hijas.
Baada ya kumzaa Arfaksadi, Shemu aliishi miaka 500, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
12 Cuando Arfaxad tuvo 35 años, nació su hijo Selaj.
Wakati Arfaksadi alipokuwa na miaka thelathini na mitano, akamzaa Shela.
13 Después del nacimiento de Selaj, Arfaxad vivió 403 años más y tuvo más hijos e hijas.
Baada ya Arfaksadi kumzaa Shela, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
14 Cuando Selaj tuvo 30 años, nació su hijo Éber.
Shela alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Eberi.
15 Después del nacimiento de Éber, Selaj vivió 403 años más y tuvo más hijos e hijas.
Shela baada ya kumzaa Eberi, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
16 Cuando Éber tuvo 34 años, nació su hijo Peleg.
Eberi alipokuwa na miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
17 Después del nacimiento de Peleg, Éber vivió 430 años más y tuvo más hijos e hijas.
Baada ya Eberi kumzaa Pelegi, aliishi miaka 430, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
18 Cuando Peleg tuvo 30 años, nació su hijo Reú.
Pelegi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Reu.
19 Después del nacimiento de Reú, Peleg vivió 209 años más y tuvo más hijos e hijas.
Baada ya Pelegi kumzaa Reu, aliishi miaka 209, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
20 Cuando Reú tuvo 32 años, nació su hijo Serug.
Reu alipokuwa na miaka thelathini na miwili, akamzaa Serugi.
21 Después del nacimiento de Serug, Reú vivió 207 años más, y tuvo más hijos e hijas.
Baada ya Reu kumzaa Serugi, aliishi miaka 207, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
22 Cuando Serug tuvo 30 años, nació su hijo Nacor.
Serugi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Nahori.
23 Después del nacimiento de Nacor, Serug vivió 200 años más y tuvo más hijos e hijas.
Baada ya Serugi kumzaa Nahori, aliishi miaka 200, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
24 Cuando Nacor tuvo 29 años, nació su hijo Téraj.
Nahori alipokuwa na miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
25 Después del nacimiento de Téraj, Nacor vivió 119 años más, y tuvo más hijos e hijas.
Baada ya Nahori kumzaa Tera, aliishi miaka 119, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
26 Cuando Téraj tuvi 70 años, nacieron sus hijos Abram, Nacor y Harán.
Tera alipokuwa na miaka sabini, akamzaa Abramu, Nahori na Harani.
27 Esta es la genealogía de Téraj. Téraj fue el padre de Abram, Nacor y Harán. Harán fue el padre de Lot.
Hawa ndio wazao wa Tera. Tera aliwazaa Abramu, Nahori na Harani. Harani akamzaa Loti.
28 Sin embargo, Harán murió cuando si padre Téraj aún vivía en Ur de los caldeos, la tierra donde nació.
Tera alipokuwa bado hai, Harani akafa huko Uru ya Wakaldayo, nchi alimozaliwa.
29 Tanto Abram como Nacor se casaron. La esposa de Abram se llamaba Sarai, y la esposa de Nacor se llamaba Milca. (Milca era hija de Harán, quien era padre tanto de Milca como de Jiscá).
Abramu na Nahori walioa. Mke wa Abramu aliitwa Sarai, na mke wa Nahori aliitwa Milka; Milka na Iska walikuwa watoto wa Harani.
30 Sarai no podia quedar embarazada, por lo tanto no tenía hijos.
Sarai alikuwa tasa, hakuwa na watoto.
31 Téraj tomó a su hijo Abram, a su nieto Lot, (quien era el hijo de Arám), a su nuera Sarai, (que era la esposa de su hijo Abram), y se fue de Ur de los caldeos para mudarse a Canaán. Llegaron hasta Harán y se quedaron a vivir allí.
Tera akamchukua Abramu mwanawe, Loti mwana wa Harani mwanawe, na Sarai mkwewe, mke wa Abramu mwanawe, wakatoka kwa pamoja katika Uru ya Wakaldayo kwenda nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani, wakaishi huko.
32 Téraj vivió 205 años y murió en Harán.
Tera alikufa huko Harani akiwa na miaka 205.

< Génesis 11 >