< Ezequiel 48 >

1 Esta es una lista de los territorios según los nombres de las tribus. En la frontera norte, el territorio de Dan limita con el camino de Hetlón hacia Lebo-hamat y con Hazar-enan en la frontera de Damasco con Hamat al norte, y se extiende desde el límite oriental del país hasta el occidental.
“Haya ndiyo majina ya makabila na sehemu zao: Kwenye mpaka wa kaskazini, Dani atakuwa na sehemu moja, mpaka huo utafuata barabara ya Hethloni hadi Lebo-Hamathi, Hasar-Enani hata mpaka wa kaskazini wa Dameski karibu na Hamathi utakuwa sehemu ya huo mpaka wake kuanzia upande wa mashariki hadi upande wa magharibi.
2 El territorio de Aser limita con el de Dan de este a oeste.
“Asheri atakuwa na sehemu moja, itapakana na nchi ya Dani kuanzia mashariki hadi upande wa magharibi.
3 El territorio de Neftalí limita con el de Aser de este a oeste.
“Naftali atakuwa na sehemu moja, itapakana na nchi ya Asheri kuanzia mashariki hadi magharibi.
4 El territorio de Manasés limita con el de Neftalí de este a oeste.
“Manase atakuwa na sehemu moja, itapakana na nchi ya Naftali kuanzia mashariki hadi magharibi.
5 El territorio de Efraín limita con el de Manasés de este a oeste.
“Efraimu atakuwa na sehemu moja, itapakana na nchi ya Manase kuanzia mashariki hadi magharibi.
6 El territorio de Rubén limita con el de este a oeste.
“Reubeni atakuwa na sehemu moja, itapakana na nchi ya Efraimu kuanzia mashariki hadi magharibi.
7 El territorio de Judá limita con el de Rubén de este a oeste.
“Yuda atakuwa na sehemu moja, itapakana na nchi ya Reubeni kuanzia mashariki hadi magharibi.
8 Junto a la asignación de Judá, de este a oeste, está la zona especial para la que debes hacer provisión. Tendrá 25.000 codos de ancho y se extenderá la misma longitud que una asignación tribal de este a oeste. El santuario estará en medio de ella.
“Kupakana na nchi ya Yuda kuanzia mashariki mpaka magharibi itakuwa ndiyo sehemu utakayoitoa ili kuwa toleo maalum. Itakuwa na upana wa dhiraa 25,000 na urefu wake kuanzia mashariki mpaka magharibi utakuwa ule ule wa sehemu moja ya kabila, mahali patakatifu patakuwa katikati ya eneo hilo.
9 El territorio especial que hagas será para el Señor y tendrá 25.000 codos por 10.000 codos.
“Hiyo sehemu maalum mtakayotoa kwa Bwana itakuwa na urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000
10 Este será el territorio sagrado para los sacerdotes. Tendrá 25.000 codos de largo en los lados norte y sur, y 11.000 codos de ancho en los lados oeste y este. El santuario estará en medio de él.
Hii itakuwa ni sehemu takatifu kwa ajili ya makuhani. Itakuwa na urefu wa dhiraa 25,000 upande wa kaskazini, upana wa dhiraa 10,000 upande wa magharibi, dhiraa 10,000 upande wa mashariki na urefu wa dhiraa 25,000 upande wa kusini. Katikati yake patakuwa mahali patakatifu pa Bwana.
11 Es para los sacerdotes santos, descendientes de Sadoc, que se mantuvieron fieles y no me abandonaron cuando los israelitas me abandonaron.
Hii itakuwa kwa ajili ya makuhani waliowekwa wakfu, Wasadoki, waliokuwa waaminifu katika kunitumikia nao hawakupotoka kama Walawi walivyofanya wakati Waisraeli walipopotoka.
12 Será una parte especial de la tierra provista para ellos, una asignación santísima junto a la de los levitas.
Itakuwa toleo maalum kwao kutoka sehemu takatifu ya nchi, yaani, sehemu takatifu sana, inayopakana na nchi ya Walawi.
13 Los levitas tendrán un área de 25.000 codos por 10.000 codos adyacente a la asignación de los sacerdotes. Su longitud total será de 25.000 codos, y su anchura de 10.000 codos.
“Kando ya nchi ya makuhani, Walawi watakuwa na mgawo wa urefu wa dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000. Urefu wake utakuwa jumla dhiraa 25,000 na upana wa dhiraa 10,000.
14 No se les permite vender a cambio ni transferir nada de ella, porque es la mejor parte de la tierra y es sagrada para el Señor.
Hawataruhusiwa kuuza wala kuibadilisha hata mojawapo. Hii ndiyo sehemu nzuri ya nchi kuliko nyingine zote, hivyo haitakuwa mikononi mwa watu wengine, kwa sababu ni takatifu kwa Bwana.
15 El resto, de 5.000 codos por 25.000 codos, es para uso ordinario de la ciudad para casas y pastos. La ciudad estará en medio de ella,
“Eneo linalobaki lenye upana wa dhiraa 5,000 na urefu wa dhiraa 25,000, litakuwa kwa ajili ya matumizi ya kawaida ya mji, kwa ajili ya ujenzi wa nyumba na malisho. Mji utakuwa katikati yake
16 y estas serán sus medidas 4.500 codos por todos los lados, al norte, al sur, al este y al oeste.
nao utakuwa na vipimo hivi: upande wa kaskazini dhiraa 4,500, upande wa kusini dhiraa 4,500, upande wa mashariki dhiraa 4,500 na upande wa magharibi dhiraa 4,500.
17 Los pastos de la ciudad la rodearán por 250 codos por todos los lados, al norte, al sur, al este y al oeste.
Sehemu ya malisho kwa ajili ya mji itakuwa na eneo la dhiraa 250 upande wa kaskazini, dhiraa 250 upande wa kusini, dhiraa 250 upande wa mashariki na dhiraa 250 upande wa magharibi.
18 Lo que queda de la tierra que bordea el territorio sagrado y que corre a su lado será de 10.000 codos por el lado este y por el lado oeste. Las cosechas que produzca servirán de alimento a los que trabajen en la ciudad.
Eneo linalobaki, linalopakana na sehemu takatifu likiwa na urefu sawa nalo, litakuwa dhiraa 10,000 upande wa mashariki na dhiraa 10,000 upande wa magharibi. Mazao yake yatawapa watumishi wa mji chakula.
19 Los trabajadores que cultiven la tierra serán de todas las tribus israelitas.
Watumishi wa mji wanaolima shamba hili watatoka katika makabila yote ya Israeli.
20 Todoel territorio será un cuadrado de 25.000 codos por 25.000 codos. Debes hacer una provisión para el territorio sagrado, junto con el área para la ciudad.
Eneo lote la hiyo sehemu litakuwa mraba, yaani, dhiraa 25,000 kila upande. Kama toleo maalum mtatenga sehemu takatifu, pamoja na milki ya mji.
21 La tierra que quede a ambos lados del territorio sagrado y del área para la ciudad pertenecerá al príncipe. Esta tierra estará junto a los territorios de las tribus y se extenderá al este desde los 25.000 codos de la sección santa hasta el límite oriental, y al otro lado al oeste desde los 25.000 codos hasta el límite occidental. En medio de ellos estará la sección santa y el santuario del Templo.
“Eneo linalobaki pande zote za eneo linalofanya sehemu takatifu na milki ya mji litakuwa mali ya mkuu atawalaye. Eneo hili litaenea upande wa mashariki kuanzia kwenye dhiraa 25,000 za sehemu takatifu hadi mpaka wa mashariki na kuelekea upande wa magharibi kuanzia kwenye dhiraa 25,000 hadi mpaka wa magharibi. Maeneo yote haya mawili yanayoenda sambamba na urefu wa sehemu za makabila yatakuwa ya mkuu anayetawala, na sehemu ile takatifu pamoja na mahali patakatifu pa Hekalu itakuwa katikati yake.
22 El área de los levitas y el área de la ciudad estarán en medio de la asignación del príncipe, y estarán entre los límites de las asignaciones de Judá y Benjamín.
Kwa hiyo milki ya Walawi na milki ya mji vitakuwa katikati ya eneo lile ambalo ni mali ya mkuu anayetawala. Eneo la mkuu anayetawala litakuwa kati ya mpaka wa Yuda na mpaka wa Benyamini.
23 Estas son las asignaciones para el resto de las tribus: La asignación de Benjamín se extiende desde el límite oriental del país hasta el occidental.
“Kuhusu makabila yaliyobaki: Benyamini atakuwa na sehemu moja, itakayoanzia upande wa mashariki hadi upande wa magharibi.
24 El territorio de Simeón limita con el de Benjamín de este a oeste.
“Simeoni atakuwa na sehemu moja, itakayopakana na nchi ya Benyamini kuanzia mashariki hadi magharibi.
25 El territorio de Isacar limita con el de Simeón de este a oeste.
“Isakari atakuwa na sehemu moja, itakayopakana na nchi ya Simeoni kuanzia mashariki hadi magharibi.
26 El territorio de Zabulón limita con el de Isacar de este a oeste.
“Zabuloni atakuwa na sehemu moja, itakayopakana na nchi ya Isakari kuanzia mashariki hadi magharibi.
27 El territorio de Gad limita con el de Zabulón de este a oeste.
“Gadi atakuwa na sehemu moja, itakayopakana na nchi ya Zabuloni kuanzia mashariki hadi magharibi.
28 El límite sur del territorio de Gad será desde Tamar hasta las aguas de Meribat-Cadés, y luego a lo largo del Wadi de Egipto hasta el Mar Mediterráneo.
“Mpaka wa kusini wa Gadi utapita kusini kuanzia Tamari hadi maji ya Meriba-Kadeshi, kisha kupitia upande wa Kijito cha Misri hadi Bahari Kuu.
29 Esta es la tierra que debes asignar a las tribus de Israel para que la posean y la transmitan como herencia. Estos son los territorios que se les han asignado, declara el Señor Dios.
“Hii ndiyo nchi mtakayogawanya kuwa urithi kwa makabila ya Israeli, nazo zitakuwa sehemu zao,” asema Bwana Mwenyezi.
30 Estas serán las salidas de la ciudad, comenzando por el lado norte, que tiene una longitud de 4.500 codos.
“Haya yatakuwa ndiyo malango ya mji ya kutokea: Kuanzia upande wa kaskazini, ambayo urefu wake ni dhiraa 4,500, utakuwa na malango matatu,
31 Las puertas de la ciudad llevarán los nombres de las tribus de Israel. Habrá tres puertas en el lado norte: las puertas de Rubén, Judá y Leví.
malango hayo ya mji yatapewa majina ya makabila ya Israeli. Malango hayo matatu ya upande wa kaskazini moja litakuwa lango la Reubeni, lango la Yuda na lango la Lawi.
32 Habrá tres puertas en el lado este, (también de 4.500 codos de largo): las puertas de José, Benjamín y Dan.
“Upande wa mashariki, wenye urefu wa dhiraa 4,500, utakuwa na malango matatu: lango la Yosefu, lango la Benyamini na lango la Dani.
33 Habrá tres puertas en el lado sur, (también de 4.500 codos de largo): las puertas de Simeón, Isacar y Zabulón.
“Upande wa kusini, wenye urefu wa dhiraa 4,500, utakuwa na malango matatu: lango la Simeoni, lango la Isakari na lango la Zabuloni.
34 En el lado oeste habrá tres puertas (también de 4.500 codos): la puerta de Gad, la puerta de Aser y la puerta de Neftalí.
“Upande wa magharibi, wenye urefu wa dhiraa 4,500, utakuwa na malango matatu: lango la Gadi, lango la Asheri na lango la Naftali.
35 La distancia alrededor del exterior de la ciudad será de 18.000 codos. Desde ese día el nombre de la ciudad será “El Señor está allí”.
“Urefu wote kuzunguka utakuwa dhiraa 18,000. “Nalo jina la mji huo kuanzia wakati huo na kuendelea litakuwa: Bwana yupo hapa.”

< Ezequiel 48 >