< Éxodo 21 >

1 “Estos son los reglamentos que debe presentarles:
“Hizi ndizo sheria utakazoweka mbele ya Waisraeli:
2 “Si compran un esclavo hebreo, debe trabajar para ustedes durante seis años. Pero en el séptimo año, debe ser liberado sin tener que pagar nada.
“Kama ukimnunua mtumwa wa Kiebrania, atakutumikia kwa miaka sita. Lakini katika mwaka wa saba, atakuwa huru naye atakwenda zake pasipo kulipa chochote.
3 Si era soltero cuando llegó, debe irse soltero. Si tenía una esposa cuando llegó, ella debe irse con él.
Kama akija peke yake, atakwenda huru peke yake, lakini kama akija na mke, ataondoka pamoja naye.
4 Si su amo le da una esposa y ella tiene hijos con él, la mujer y sus hijos pertenecerán a su amo, y sólo el hombre será liberado.
Kama bwana wake alimpatia mke naye akamzalia wana au binti, mwanamke pamoja na watoto wake watakuwa mali ya bwana wake na huyo mwanaume ataondoka peke yake.
5 “Sin embargo, si el esclavo declara formalmente: ‘Amo a mi señor, a mi esposa y a mis hijos; no quiero ser liberado’
“Lakini kama mtumishi akisema, ‘Ninampenda bwana wangu, mke wangu pamoja na watoto na sitaki kuwa huru,’
6 entonces su señor lo llevará ante los jueces. Luego lo pondrá de pie contra la puerta o el poste de la puerta y usará una herramienta de metal para hacerle un agujero en la oreja. Entonces trabajará para su amo de por vida.
ndipo bwana wake atakapolazimika kumpeleka mbele ya waamuzi. Kisha atampeleka kwenye mlango au kizingiti na kutoboa sikio lake kwa shazia. Naye atamtumikia bwana wake maisha yake yote.
7 “Si un hombre vende a su hija como esclava, no será liberada de la misma manera que los esclavos.
“Kama mtu akimuuza binti yake kuwa mtumwa, hataachwa huru kama watumwa wa kiume waachiwavyo.
8 Si el hombre que la eligió para sí no está satisfecho con ella, debe dejar que sea comprada de nuevo. No podrá venderla a los extranjeros, ya que ha sido injusto con ella.
Kama hakumpendeza bwana wake aliyemchagua, huyo bwana atamwacha akombolewe. Hatakuwa na haki ya kumuuza kwa wageni, kwa sababu huyo bwana atakuwa amekosa uaminifu.
9 Si decide dársela a su hijo, debe tratarla como a una hija.
Kama akimchagua aolewe na mwanawe, ni lazima ampe haki za kuwa binti yake.
10 Si toma a otra mujer, no debe reducir los subsidios de comida y ropa, ni los derechos maritales de la primera.
Ikiwa huyo mwana aliyeozwa mtumwa mwanamke ataoa mwanamke mwingine, ni lazima aendelee kumtosheleza huyo mke wa kwanza kwa chakula, mavazi na haki zote za ndoa.
11 Si no le da estas tres cosas, ella es libre de irse sin pagar nada.
Iwapo hatamtosheleza kwa mambo hayo matatu, huyo mke wa kwanza ataondoka na kuwa huru bila malipo yoyote ya fedha.
12 “Todo aquel que golpee y mate a otra persona debe ser ejecutado.
“Yeyote ampigaye mtu na kumuua ni lazima auawe hakika.
13 Sin embargo, si no fue intencional y Dios permitió que sucediera, entonces arreglaré un lugar para ustedes donde puedan correr y estar seguros.
Hata hivyo, kama hakumuua kwa makusudi, lakini Mungu akaruhusu itendeke, basi atakimbilia mahali nitakapomchagulia.
14 Pero si alguien planea deliberadamente y mata a propósito a otro, debe alejarlo de mi altar y ejecutarlo.
Lakini kama mtu akipanga na kumuua mwingine kwa makusudi, mwondoe katika madhabahu yangu na kumuua.
15 “Cualquiera que golpee a su padre o madre debe ser ejecutado.
“Yeyote amshambuliaye baba yake au mama yake ni lazima auawe.
16 Cualquiera que secuestre a alguien más debe ser ejecutado, ya sea que la víctima sea vendida o que aún esté en su posesión.
“Yeyote amtekaye nyara mwingine akamuuza au akamweka kwake, akikamatwa ni lazima auawe.
17 “Cualquiera que desprecie a su padre o a su madre debe ser ejecutado.
“Yeyote atakayemlaani baba yake au mama yake ni lazima auawe.
18 “Si los hombres están peleando y uno golpea al otro con una piedra o con el puño, y el hombre herido no muere pero tiene que permanecer en cama,
“Kama watu wakigombana na mmoja akimpiga mwingine kwa jiwe au kwa ngumi yake na hakufa bali akaugua na kulala kitandani,
19 y luego se levanta y camina afuera con su bastón, entonces el que lo golpeó no será castigado. Aún así, debe compensar al hombre por el tiempo perdido de su trabajo y asegurarse de que esté completamente curado.
yule aliyempiga ngumi hatahesabiwa kuwa na hatia kama mwenzake ataamka na kujikongoja kwa fimbo yake, lakini hata hivyo, ni lazima amlipe fidia ya muda wake aliopoteza na awajibike mpaka apone kabisa.
20 “Cualquiera que golpee a su esclavo o esclava con una vara, y el esclavo muera como resultado, debe ser castigado.
“Kama mtu akimpiga mtumwa wake wa kiume au wa kike kwa fimbo na mtumwa huyo akafa papo hapo, ni lazima aadhibiwe
21 Sin embargo, si después de un día o dos el esclavo mejora, el dueño no será castigado porque el esclavo es de su propiedad.
lakini ikiwa mtumwa ataamka baada ya siku moja au mbili, hataadhibiwa, kwa sababu yule mtumwa ni mali yake.
22 “Si los hombres que están peleando golpean a una mujer embarazada para que dé a luz prematuramente, pero no se produce ninguna lesión grave, debe ser multado con la cantidad que el marido de la mujer demande y según lo permitan los jueces.
“Ikiwa watu wawili wanapigana na wakamuumiza mwanamke mjamzito, naye akazaa kabla ya wakati lakini hakuna majeraha makubwa, mhalifu atatozwa mali kiasi cha madai ya mume wa yule mwanamke, na jinsi mahakama itakavyoamua.
23 Pero si se produce una lesión grave, entonces debe pagar una vida por otra vida;
Lakini kukiwa na jeraha kubwa, ni lazima ulipe uhai kwa uhai,
24 ojo por ojo, diente por diente, mano por mano, pie por pie,
jicho kwa jicho, jino kwa jino, mkono kwa mkono, mguu kwa mguu,
25 quemadura por quemadura, herida por herida y moretón por moretón.
kuchomwa moto kwa kuchomwa moto, jeraha kwa jeraha, mchubuko kwa mchubuko.
26 “El que golpee a su esclavo o esclava en el ojo y lo ciegue, debe liberar al esclavo como compensación por el ojo.
“Ikiwa mtu atampiga mtumwa mwanaume au mwanamke kwenye jicho na kuliharibu, ni lazima amwache huru yule mtumwa kama fidia ya hilo jicho.
27 El que golpee el diente de su esclavo o esclava debe liberar al esclavo como compensación por el diente.
Kama akimvunja jino mtumwa wa kiume au wa kike, ni lazima amwache huru huyo mtumwa kwa kufidia hilo jino.
28 “Si un buey usa sus cuernos para matar a un hombre o una mujer, el buey debe ser apedreado hasta morir, y su carne no debe ser comida. Pero el dueño del buey no será castigado.
“Kama fahali akimuua mwanaume au mwanamke kwa kumpiga kwa pembe, fahali huyo ni lazima auawe kwa kupigwa mawe, na nyama yake haitaliwa. Lakini mwenye fahali huyo hatawajibika.
29 Pero si el buey ha herido repetidamente a la gente con sus cuernos, y su dueño ha sido advertido pero aún no lo tiene bajo control, y mata a un hombre o una mujer, entonces el buey debe ser apedreado hasta morir y su dueño también debe ser ejecutado.
Lakini hata hivyo, ikiwa huyo fahali amekuwa na tabia ya kupiga kwa pembe, na mwenyewe ameonywa na hakutaka kumfungia naye akamuua mwanaume au mwanamke, huyo fahali ni lazima auawe kwa mawe na mwenye fahali pia auawe.
30 Pero si en lugar de ello se exige el pago de una indemnización, el propietario puede compensar su vida pagando la totalidad de la indemnización exigida.
Lakini ikiwa malipo yatatakiwa kwake, basi anaweza kulipa kinachodaiwa ili kuukomboa uhai wake.
31 Pero si en lugar de ello se exige el pago de una indemnización, el propietario puede salvar su vida pagando la totalidad de la indemnización exigida.
Sheria hii pia itatumika ikiwa fahali atampiga kwa pembe mwana au binti.
32 Si el buey usa sus cuernos y mata a un esclavo o esclava, el propietario del buey debe pagar treinta siclos de plata al amo del esclavo, y el buey debe ser apedreado hasta la muerte.
Ikiwa fahali atampiga mtumwa wa kike au wa kiume, mwenye fahali atalipa shekeli thelathini za fedha kwa bwana mwenye mtumwa, na fahali ni lazima auawe kwa mawe.
33 “Si alguien quita la tapa de una cisterna o cava una y no la cubre, y un buey o un asno cae en ella,
“Kama mtu akiacha shimo wazi, ama akachimba shimo kisha asilifukie, na ngʼombe au punda akatumbukia ndani yake,
34 el dueño de la fosa debe pagar una compensación al dueño del animal y quedarse con el animal muerto.
mwenye shimo ni lazima alipe hasara iliyotokea; ni lazima amlipe mwenye mnyama. Mnyama aliyekufa atakuwa wake.
35 “Si el buey de alguien hiere al de otro y éste muere, debe vender al buey vivo y compartir el dinero recibido; también debe compartir al animal muerto.
“Kama fahali wa mtu fulani atamuumiza fahali wa mtu mwingine na akafa, watamuuza yule aliye hai na wagawane sawa fedha pamoja na mnyama aliyekufa.
36 Pero si se sabe que el buey ha herido repetidamente a personas con sus cuernos, y su dueño ha sido advertido pero aún no lo tiene bajo control, debe pagar una compensación completa, buey por buey; pero el dueño puede quedarse con el animal muerto”.
Hata hivyo, kama ikifahamika kwamba fahali huyo alikuwa na tabia ya kupiga kwa pembe na mwenyewe hakumfunga, ni lazima mwenye fahali alipe mnyama kwa mnyama, na mnyama aliyekufa atakuwa wake.

< Éxodo 21 >