< 2 Samuel 8 >

1 Poco después de esto, David atacó y subyugó a los filisteos, quitándoles Metheg-ammah.
Baada ya muda, Daudi akawashinda Wafilisti na kuwatiisha, naye akautwaa Metheg-Amma kutoka mikononi mwa Wafilisti.
2 David también derrotó a los moabitas. Los hizo tumbarse en el suelo y los midió con un tramo de cuerda. Midió dos tramos para los que debían morir, y un tramo de cuerda para los que debían vivir. Entonces los sometió bajo su gobierno, y les exigió que pagaran impuestos.
Pia Daudi akawashinda Wamoabu. Akawafanya walale chini kwa mstari akawapima kwa urefu wa kamba. Kila alipopima urefu wa hiyo kamba mara mbili hilo kundi waliuawa na alipopima mara ya tatu aliwaacha hai. Kwa hiyo Wamoabu wakawa chini ya Daudi nao wakamletea kodi.
3 David también derrotó a Hadad-ezer, hijo de Rehob, rey de Soba, cuando intentaba imponer su control a lo largo del río Éufrates.
Zaidi ya hayo, Daudi akapigana na Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba, alipokwenda kurudisha tena utawala wake kwenye eneo la Mto Frati.
4 David capturó 1.000 de sus carros, 7.000 jinetes y 20.000 soldados de a pie. Ató por las patas a todos los caballos que llevaban carros, pero dejó suficientes caballos para 100 carros de guerra.
Daudi akateka magari yake ya vita 1,000, askari wapanda farasi 7,000 na askari 20,000 watembeao kwa miguu. Daudi akawakata wale farasi wote wakokotao magari mishipa ya miguu, isipokuwa farasi 100 hakuwakata.
5 Cuando los arameos de Damasco vinieron a ayudar al rey Hadad-ezer de Soba, David mató a veintidós mil de ellos.
Waaramu wa Dameski walipokuja kumsaidia Hadadezeri mfalme wa Soba, Daudi akawashambulia na kuwaua 22,000 miongoni mwao.
6 Colocó guarniciones en el reino arameo con capital en Damasco, e hizo que los arameos se sometieran a él y les exigió el pago de impuestos. El Señor le daba victorias a David por donde quiera que iba.
Daudi akaweka askari walinzi katika ufalme wa Waaramu huko Dameski, nao Waaramu wakawa watumwa wake na kumlipa ushuru. Bwana akampa Daudi ushindi kote alipokwenda.
7 David tomó los escudos de oro que le pertenecían a los oficiales de Hadad-ezer y los llevó a Jerusalén.
Daudi akazitwaa ngao za dhahabu zilizokuwa za maafisa wa Hadadezeri na kuzileta Yerusalemu.
8 El rey David también tomó una gran cantidad de bronce de Beta y Berotai, ciudades que habían pertenecido a Hadad-ezer.
Kutoka miji ya Beta na Berothai, iliyokuwa miji ya Hadadezeri, Mfalme Daudi akatwaa shaba nyingi sana.
9 Cuando Toi, rey de Hamat, se enteró de que David había destruido todo el ejército de Hadadzer, rey de Soba,
Tou, mfalme wa Hamathi, aliposikia kwamba Daudi amelishinda jeshi lote la Hadadezeri,
10 envió a su hijo Joram a David para que se hiciera amigo de él y lo felicitara por su victoria en la batalla contra Hadad-ezer. Toi y Hadadezer habían estado en guerra con frecuencia. Joram trajo toda clase de regalos de oro, plata y bronce.
akamtuma mwanawe Yoramu kwa Mfalme Daudi kumsalimu na kumpongeza kwa ushindi wake katika vita dhidi ya Hadadezeri, kwa kuwa Hadadezeri alikuwa amepigana vita na Tou. Yoramu akamletea Daudi vyombo vya fedha, dhahabu na shaba.
11 El rey David le dedicó estos regalos al Señor, junto con la plata y el oro que había tomado de todas las naciones que había sometido:
Mfalme Daudi akaviweka vifaa hivi wakfu kwa Bwana, kama vile alivyokuwa amefanya kwa fedha na dhahabu kutoka kwa mataifa yote aliyokuwa ameyashinda:
12 Edom, Moab, los amonitas, los filisteos y los amalecitas; así como el botín tomado a Hadad-ezer, hijo de Rehob, rey de Soba.
yaani Edomu, Moabu, Waamoni, Wafilisti na Waamaleki. Pia akaweka wakfu nyara alizoteka kutoka kwa Hadadezeri mwana wa Rehobu, mfalme wa Soba.
13 David también se dio a conocer cuando regresó tras derrotar a dieciocho mil edomitas en el Valle de la Sal.
Naye Daudi akapata sifa baada ya kurudi kutoka kuwaua Waedomu 18,000 katika Bonde la Chumvi.
14 Colocó guarniciones por todo Edom, y todos los edomitas se sometieron a David. El Señor le dio a David victorias dondequiera que fuera.
Akaweka kambi za askari walinzi katika Edomu yote, nao Waedomu wakawa chini ya Daudi. Bwana alimpatia Daudi ushindi kila alipokwenda.
15 David gobernó sobre todo Israel. Hizo lo que era justo y correcto para todo su pueblo.
Daudi akatawala Israeli yote, akitenda lililo haki na sawa kwa watu wake wote.
16 Joab, hijo de Sarvia, era el comandante del ejército, y Josafat, hijo de Ahilud, llevaba los registros oficiales.
Yoabu mwana wa Seruya alikuwa jemadari wa jeshi; Yehoshafati mwana wa Ahiludi alikuwa mweka kumbukumbu;
17 Sadoc, hijo de Ahitob, y Ahimelec, hijo de Abiatar, eran sacerdotes, mientras que Seraías era el secretario.
Sadoki mwana wa Ahitubu na Ahimeleki mwana wa Abiathari walikuwa makuhani; Seraya alikuwa mwandishi;
18 Benaía, hijo de Joiada, estaba a cargo de los queretanos y peletanos; y los hijos de David eran sacerdotes.
Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa msimamizi wa Wakerethi na Wapelethi; nao wana wa Daudi walikuwa washauri wa mfalme.

< 2 Samuel 8 >