< 2 Samuel 22 >

1 David cantó las palabras de este cántico al Señor el día en que el Señor lo salvó de todos sus enemigos y de Saúl.
Daudi alimwimbia Bwana maneno ya wimbo huu wakati Bwana alipomwokoa mikononi mwa adui zake wote, na pia mkononi mwa Sauli.
2 Entonces cantó: El Señor es mi roca, mi fortaleza y mi salvador.
Akasema: “Bwana ni mwamba wangu, ngome yangu na mwokozi wangu,
3 Él es mi Dios, mi roca que me protege. Él me protege del mal, su poder me salva, me mantiene seguro. Él es mi protector; es mi salvador; me libra de la violencia.
Mungu wangu ni mwamba wangu, ambaye kwake ninakimbilia, ngao yangu na pembe ya wokovu wangu. Yeye ni ngome yangu, kimbilio langu na mwokozi wangu, huniokoa kutoka kwa watu wenye jeuri.
4 Pido ayuda al Señor, merecedor de alabanza, y me salva de los que me odian.
Ninamwita Bwana, anayestahili kusifiwa, nami ninaokolewa kutoka kwa adui zangu.
5 Las olas de la muerte me arrastran, las aguas de la destrucción me inundan;
“Mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maangamizi yalinilemea.
6 El sepulcro enrolló sus cuerdas en torno a mí; la muerte me tendió trampas. (Sheol h7585)
Kamba za kuzimu zilinizunguka, mitego ya mauti ilinikabili. (Sheol h7585)
7 En mi desesperación invoqué al Señor; clamé a mi Dios. Él escuchó mi voz desde su Templo; mi grito de auxilio llegó a sus oídos.
Katika shida yangu nalimwita Bwana, nilimlilia Mungu wangu. Kutoka Hekaluni mwake alisikia sauti yangu, kilio changu kikafika masikioni mwake.
8 La tierra se estremeció, los cimientos de los cielos temblaron por su cólera
“Dunia ilitetemeka na kutikisika, misingi ya mbingu ikatikisika, vilitetemeka kwa sababu alikuwa amekasirika.
9 Humo salía de sus narices, y fuego de su boca, carbones ardientes que ardían ante él.
Moshi ukapanda kutoka puani mwake, moto uteketezao ukatoka kinywani mwake, makaa ya moto yawakayo yakatoka ndani mwake.
10 Apartó los cielos y descendió, con nubes oscuras bajo sus pies.
Akazipasua mbingu akashuka chini, mawingu meusi yalikuwa chini ya miguu yake.
11 Montado en un ser celestial voló, abalanzándose sobre las alas del viento.
Alipanda juu ya kerubi akaruka, akapaa juu kwa mbawa za upepo.
12 Se escondió en las tinieblas, cubriéndose con negras nubes de lluvia.
Alifanya giza hema lake la kujifunika: mawingu meusi ya mvua ya angani.
13 De su resplandor brotaron carbones ardientes.
Kutokana na mwanga wa uwepo wake mawingu yalisogea, ikanyesha mvua ya mawe na umeme wa radi.
14 El Señor tronó desde el cielo; resonó la voz del Altísimo.
Bwana alinguruma kutoka mbinguni, sauti ya Aliye Juu Sana ilisikika.
15 Disparó sus flechas, dispersando a sus enemigos, los derrotó con sus rayos.
Aliipiga mishale na kutawanya adui, umeme wa radi na kuwafukuza.
16 El Señor rugió, y con el viento del aliento de su nariz se vieron los valles del mar y se descubrieron los cimientos de la tierra.
Mabonde ya bahari yalifunuliwa, na misingi ya dunia ikawa wazi kwa kukaripia kwake Bwana, kwa uvumi wa pumzi kutoka puani mwake.
17 Bajó su mano desde arriba y me agarró. Me sacó de las aguas profundas.
“Alinyoosha mkono kutoka juu na kunishika; alinitoa kutoka kilindi cha maji makuu.
18 Me rescató de mis poderosos enemigos, de los que me odiaban y eran mucho más fuertes que yo.
Aliniokoa kutoka adui wangu mwenye nguvu nyingi, kutoka adui zangu waliokuwa na nguvu nyingi kuliko mimi.
19 Se abalanzaron sobre mí en mi peor momento, pero el Señor me sostuvo.
Walinikabili siku ya msiba wangu, lakini Bwana alikuwa msaada wangu.
20 Me liberó, me rescató porque es feliz conmigo.
Alinileta nje mahali penye nafasi tele, akaniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
21 El Señor me recompensó por hacer lo correcto; me pagó porque soy inocente.
“Bwana alinitendea sawasawa na uadilifu wangu; sawasawa na usafi wa mikono yangu amenilipa.
22 Porque he seguido los caminos del Señor; no he pecado apartándome de mi Dios.
Kwa maana nimezishika njia za Bwana; sijatenda ubaya nikamwacha Mungu wangu.
23 He tenido presente todas sus leyes; no he ignorado sus mandamientos.
Sheria zake zote zi mbele yangu, wala sijayaacha maagizo yake.
24 Soy irreprochable a sus ojos; me guardo de pecar.
Nimekuwa sina hatia mbele zake, nami nimejilinda nisitende dhambi.
25 El Señor me ha recompensado por hacer lo justo. Soy inocente ante sus ojos.
Bwana amenilipa sawasawa na uadilifu wangu, sawasawa na usafi wangu machoni pake.
26 Demuestras tu fidelidad a los que son fieles; demuestras integridad a los que son íntegros,
“Kwa yeye aliye mwaminifu unajionyesha kuwa mwaminifu, kwa asiye na hatia unajionyesha kutokuwa na hatia,
27 Te muestras puro a los que son puros, pero te muestras astuto con los astutos.
kwa aliye mtakatifu unajionyesha kuwa mtakatifu, lakini kwa aliyepotoka unajionyesha kuwa mkaidi.
28 Tú salvas a los humildes, pero tus ojos vigilan a los soberbios para abatirlos.
Wewe huwaokoa wanyenyekevu, lakini macho yako ni juu ya wenye kiburi ili uwashushe.
29 Tú, Señor, eres mi lámpara. El Señor ilumina mis tinieblas.
Wewe ni taa yangu, Ee Bwana. Bwana hulifanya giza langu kuwa mwanga.
30 Contigo puedo abatir una tropa de soldados; contigo, Dios mío, puedo escalar un muro de la fortaleza.
Kwa msaada wako naweza kushinda jeshi, nikiwa pamoja na Mungu wangu nitaweza kuruka ukuta.
31 El camino de Dios es absolutamente correcto. La palabra del Señor es digna de confianza. Es un escudo para todos los que acuden a él en busca de protección.
“Kuhusu Mungu, njia yake ni kamilifu; neno la Bwana halina dosari. Yeye ni ngao kwa wote wanaokimbilia kwake.
32 Porque ¿quién es Dios sino el Señor? ¿Quién es la Roca, sino nuestro Dios?
Kwa maana ni nani aliye Mungu zaidi ya Bwana? Ni nani aliye Mwamba isipokuwa Mungu wetu?
33 Dios me hace fuerte y me mantiene seguro.
Mungu ndiye anivikaye nguvu na kufanya njia yangu kuwa kamilifu.
34 Me hace seguro como el ciervo, capaz de caminar por las alturas con seguridad.
Huifanya miguu yangu kama miguu ya kulungu, huniwezesha kusimama mahali palipo juu.
35 Me enseña a luchar en la batalla; me da la fuerza para tensar un arco de bronce.
Huifundisha mikono yangu kupigana vita; mikono yangu inaweza kupinda upinde wa shaba.
36 Me protege con el escudo de su salvación; su ayuda me ha engrandecido.
Hunipa ngao yako ya ushindi, unajishusha chini ili kuniinua.
37 Me diste espacio para caminar y evitaste que mis pies resbalaran.
Huyapanua mapito yangu, ili miguu yangu isiteleze.
38 Perseguí a mis enemigos y los alcancé. No me devolví hasta haberlos destruido.
“Niliwafuatia adui zangu na nikawaseta, sikurudi nyuma mpaka walipoangamizwa.
39 Los derribé y no pudieron levantarse. Cayeron a mis pies.
Niliwaseta kabisa, nao hawakuweza kuinuka tena; walianguka chini ya miguu yangu.
40 Me hiciste fuerte para la batalla; hiciste que los que se levantaron contra mí se arrodillaran ante mí.
Ulinivika nguvu kwa ajili ya kupigana vita; uliwafanya adui zangu wasujudu miguuni pangu.
41 Hiciste que mis enemigos huyeran; destruí a todos mis enemigos.
Uliwafanya adui zangu wageuke na kukimbia, nami nikawaangamiza adui zangu.
42 Ellos clamaron por ayuda, pero nadie vino a rescatarlos. Incluso clamaron al Señor, pero él no les respondió.
Walipiga yowe, lakini hapakuwepo na yeyote wa kuwaokoa; walimlilia Bwana, lakini hakuwajibu.
43 Los convertí en polvo, como el polvo de la tierra. Los aplasté y los arrojé como lodo en la calle.
Niliwaponda kama mavumbi ya nchi; niliwaponda na kuwakanyaga kama tope barabarani.
44 Me rescataste de los pueblos rebeldes; me mantuviste como gobernante de las naciones: gente que no conocía ahora me sirve.
“Umeniokoa kutokana na mashambulizi ya watu wangu; umenihifadhi mimi kama kiongozi wa mataifa. Watu ambao sikuwajua wananitumikia,
45 Los extranjeros se acobardan ante mí; en cuanto oyen hablar de mí, me obedecen.
nao wageni huja wakininyenyekea, mara wanisikiapo, hunitii.
46 Se desalientan y salen temblando de sus fortalezas.
Wote wanalegea, wanatoka katika ngome zao wakitetemeka.
47 ¡El Señor vive! ¡Bendita sea mi Roca! ¡Alabado sea el Dios que me salva!
“Bwana yu hai! Sifa ni kwa Mwamba wangu! Atukuzwe Mungu, Mwamba, Mwokozi wangu!
48 Dios me vindica, pone a los pueblos bajo mis pies,
Yeye ndiye Mungu anilipiziaye kisasi, ayawekaye mataifa chini yangu,
49 Y me libera de los que me odian. Me mantiene a salvo de los que se rebelan contra mí, me salva de los hombres violentos.
aniwekaye huru toka kwa adui zangu. Uliniinua juu ya adui zangu; uliniokoa toka kwa watu wajeuri.
50 Por eso te alabaré entre las naciones, Señor; cantaré alabanzas sobre lo que tú eres.
Kwa hiyo nitakusifu, Ee Bwana, katikati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
51 Has salvado al rey tantas veces, mostrando tu amor fiel a David, tu ungido, y a sus descendientes por siempre.
Humpa mfalme wake ushindi mkuu; huonyesha fadhili zake kwa mpakwa mafuta wake, kwa Daudi na wazao wake milele.”

< 2 Samuel 22 >