< 2 Reyes 24 >

1 Durante el reinado de Joaquim, Nabucodonosor, tipo de Babilonia, invadió el país y Joaquim se sometió a él. Pero después de tres años Joaquim se rebeló contra Nabucodonosor.
Wakati wa utawala wa Yehoyakimu, Nebukadneza mfalme wa Babeli aliishambulia nchi, naye Yehoyakimu akawa mtumwa wake kwa miaka mitatu. Lakini hatimaye akabadili mawazo yake na kuasi dhidi ya Nebukadneza.
2 Entonces el Señor envió bandas de asaltantes contra Judá para destruirlos. Vinieron de Babilonia, Harán, Moab y Amón, tal como el Señor había dicho por medio de sus siervos los profetas.
Bwana akatuma wavamiaji wa Wakaldayo, Waaramu, Wamoabu na Waamoni ili kumshambulia. Aliwatuma kuiangamiza Yuda sawasawa na neno la Bwana lililosemwa na watumishi wake manabii.
3 El Señor habló contra Judá para desterrarlos de su presencia a causa de todos los pecados que Manasés había cometido y de la gente inocente que había matado,
Hakika mambo haya yalitokea Yuda kulingana na agizo la Bwana, ili kuwaondoa kutoka machoni pake kwa sababu ya dhambi za Manase na yote aliyoyafanya,
4 llenando Jerusalén con su sangre. El Señor no estaba dispuesto a perdonar esto.
ikiwa ni pamoja na kumwaga damu isiyo na hatia. Kwa kuwa aliijaza Yerusalemu kwa damu isiyo na hatia, naye Bwana hakuwa radhi kusamehe.
5 El resto de lo que sucedió en el reinado de Joaquim, y todo lo que hizo, está registrado en el Libro de las Crónicas de los Reyes de Judá.
Matukio mengine ya utawala wa Yehoyakimu na yote aliyoyafanya, je, hayakuandikwa katika kitabu cha kumbukumbu za wafalme wa Yuda?
6 Joaquim murió, y su hijo Joaquim lo sucedió como rey.
Yehoyakimu akalala pamoja na baba zake. Naye Yehoyakini mwanawe akawa mfalme baada yake.
7 El rey de Egipto no volvió a salir de su país, pues el rey de Babilonia se había apoderado de todo el territorio que le pertenecía, desde el Wadi de Egipto hasta el río Éufrates.
Mfalme wa Misri hakutoka tena katika nchi yake, kwa sababu mfalme wa Babeli alikuwa ameitwaa himaya yake yote, kuanzia Kijito cha Misri hadi Mto Frati.
8 Joaquim tenía dieciocho años cuando llegó a ser rey, y reinó en Jerusalén durante tres meses. Su madre era Nejustá, hija de Elnatán. Ella era de Jerusalén.
Yehoyakini alikuwa na miaka kumi na minane alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miezi mitatu. Jina la mama yake aliitwa Nehushta binti Elnathani kutoka Yerusalemu.
9 Joaquim hizo lo malo a los ojos del Señor, tal como lo había hecho su padre.
Akafanya maovu machoni pa Bwana, kama vile baba yake alivyokuwa amefanya.
10 En aquel tiempo los oficiales de Nabucodonosor, rey de Babilonia, atacaron Jerusalén y la sitiaron.
Wakati huo, maafisa wa Nebukadneza mfalme wa Babeli walikuja ili kuishambulia Yerusalemu, nao wakaizunguka kwa jeshi.
11 Entonces Nabucodonosor, rey de Babilonia, vino en persona mientras sus oficiales estaban sitiando la ciudad.
Nebukadneza mwenyewe akaupandia mji wakati maafisa wake walipokuwa wameuzunguka kwa jeshi.
12 Joaquim, rey de Israel, se rindió al rey de Babilonia, junto con su madre, sus oficiales, sus comandantes y sus funcionarios. Fue en el octavo año de su reinado cuando Nabucodonosor capturó a Joaquim.
Yehoyakini mfalme wa Yuda, mama yake, wahudumu wake, wakuu na maafisa wake wote wakajisalimisha kwa Nebukadneza. Katika mwaka wa nane wa utawala wa mfalme wa Babeli, akamchukua Yehoyakini kuwa mfungwa.
13 Nabucodonosor tomó todos los tesoros del Templo del Señor y del palacio real, y cortó todos los objetos de oro que Salomón, rey de Israel, había hecho para el Templo del Señor, como el Señor había dicho que sucedería.
Kama vile Bwana alivyokuwa amesema, Nebukadneza akaondoa hazina yote kutoka Hekalu la Bwana na kutoka jumba la mfalme, akavichukua vyombo vyote vya dhahabu ambavyo Solomoni mfalme wa Israeli alikuwa amevitengeneza kwa ajili ya Hekalu la Bwana.
14 Deportó a toda Jerusalén, a todos los comandantes y a los soldados experimentados, a todos los artesanos y a los trabajadores del metal, un total de diez mil prisioneros. Sólo quedó la gente muy pobre del país.
Akawachukua watu wa Yerusalemu wote kwenda uhamishoni: yaani maafisa wote na mashujaa, watu wenye ustadi na ufundi, jumla yao watu elfu kumi. Watu maskini sana ndio tu waliobaki katika nchi.
15 Se llevó a Joaquim al exilio en Babilonia, así como a la madre del rey y a las esposas del rey y a sus funcionarios y a los principales hombres del país, a todos los deportó de Jerusalén a Babilonia.
Nebukadneza akamchukua mateka Yehoyakini hadi Babeli. Pia akawachukua utumwani kutoka Yerusalemu hadi Babeli mama yake mfalme, wake zake, maafisa wake, na viongozi wote wa nchi.
16 El rey de Babilonia también deportó a Babilonia a los siete mil hombres de combate y a los mil artesanos y metalúrgicos, todos ellos fuertes y preparados para la batalla.
Mfalme wa Babeli pia akawahamishia Babeli mashujaa elfu saba, wenye nguvu na wanaofaa kupigana vita, na watu wenye ustadi na mafundi elfu moja.
17 El rey de Babilonia nombró rey a Matanías, tío de Joaquim, en su lugar, y le cambió el nombre por el de Sedequías.
Akamfanya Matania, ndugu wa baba yake Yehoyakini, kuwa mfalme mahali pake, na akalibadilisha jina lake kuwa Sedekia.
18 Sedequías tenía veintiún años cuando llegó a ser rey, y reinó en Jerusalén durante once años. Su madre se llamaba Jamutal, hija de Jeremías.
Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja alipoanza kutawala, naye akatawala huko Yerusalemu miaka kumi na mmoja. Jina la mama yake aliitwa Hamutali binti Yeremia, kutoka Libna.
19 Sus hechos fueron malos a los ojos del Señor, tal como los de Joaquim.
Alifanya maovu machoni pa Bwana, kama alivyofanya Yehoyakimu.
20 Todo esto sucedió en Jerusalén y en Judá, a causa de la ira del Señor, hasta que finalmente los desterró de su presencia. Sedequías se rebeló contra el rey de Babilonia.
Ilikuwa ni kwa sababu ya hasira ya Bwana haya yote yalitokea Yerusalemu na Yuda, naye mwishoni akawaondoa mbele zake. Basi, Sedekia akaasi dhidi ya mfalme wa Babeli.

< 2 Reyes 24 >